JUSTIN MPOTWA
Member
- Jan 16, 2013
- 16
- 11
Ndugu watanzania,
Zimebaki siku kadhaa kutimiza mwaka mmoja toka pale ndugu yetu Daudi Mwangosi alipouawa na polisi kwa bomu pale kijijini Nyololo.
Mwangosi aliuawa tar 02/09/2012 na hii ina maana tar 02/09/2013 ndio itakuwa ni siku ya kumkumbuka.
CHADEMA wilaya ya mufindi tumeandaa shughuli mbalimbali kumkumbuka ndugu yetu. Jimbo la Mufindi Kusini wanaratibu shughuli hizo.
Kutakuwa na matukio makubwa mawili
1. Uzinduzi wa mnara wa kumbukumbu ya mwangosi ambao utasimikwa na katibu mkuu wa CHADEMA taifa ndg dr. Wilbrod Slaa.
2. Harambee ya kuchangia familia ya Mwangosi mchango ambao utawasilishwa kwa mjane wa marehemu siku hiyo.
3. Mkutano wa hadhara utakao fanyika Nyololo na Igowole
Tunapenda kuwashirikisha wale wote ambao wangependa kuchangia shughuli zote hizo.
Tunatoa namba za simu za makamanda wanaohusika na uratibu wa shughuli hizo
a. Katibu jimbo, Emmanuel Ngwalanje 0787797950
b. Katibu mwenezi jimbo, Elisha Msemwa 0755733918
c. Mhazini jimbo, Carolina Kidenya 0768757447
Karibuni wote
============
Zimebaki siku kadhaa kutimiza mwaka mmoja toka pale ndugu yetu Daudi Mwangosi alipouawa na polisi kwa bomu pale kijijini Nyololo.
Mwangosi aliuawa tar 02/09/2012 na hii ina maana tar 02/09/2013 ndio itakuwa ni siku ya kumkumbuka.
CHADEMA wilaya ya mufindi tumeandaa shughuli mbalimbali kumkumbuka ndugu yetu. Jimbo la Mufindi Kusini wanaratibu shughuli hizo.
Kutakuwa na matukio makubwa mawili
1. Uzinduzi wa mnara wa kumbukumbu ya mwangosi ambao utasimikwa na katibu mkuu wa CHADEMA taifa ndg dr. Wilbrod Slaa.
2. Harambee ya kuchangia familia ya Mwangosi mchango ambao utawasilishwa kwa mjane wa marehemu siku hiyo.
3. Mkutano wa hadhara utakao fanyika Nyololo na Igowole
Tunapenda kuwashirikisha wale wote ambao wangependa kuchangia shughuli zote hizo.
Tunatoa namba za simu za makamanda wanaohusika na uratibu wa shughuli hizo
a. Katibu jimbo, Emmanuel Ngwalanje 0787797950
b. Katibu mwenezi jimbo, Elisha Msemwa 0755733918
c. Mhazini jimbo, Carolina Kidenya 0768757447
Karibuni wote
============
![]()
Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk.Willbrod Slaa
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Wilaya ya Mufindi, mkoani Iringa kimepanga kujenga mnara wa kumbukumbu katika kijiji cha Nyololo ili kumuenzi aliyekuwa mwandishi wa habari wa Channel Ten, Daudi Mwangosi, aliyeuwawa katika kijiji hicho.
Mwangosi aliuwawa katika kijiji hicho Septemba 2, mwaka jana kwa kulipuliwa na kitu kinachodaiwa kuwa bomu baada ya kutokea vurugu kati ya wafuasi wa CHADEMA na polisi.
Katibu wa CHADEMA jimbo la MufindiKusini, Emmanuel Ngwalanje, akizungumza na NIPASHE jana alisema mnara huo ambao utagharimu kiasi cha Sh. 3,500,000 utaanza kujengwa Agosti 20 na kukamilika Agosti 28, mwaka huu na kuwaomba wadau kusaidia fedha kufanikisha ujenzi huo.
Ngwalanje alisema mmiliki wa eneoalipouwawa Mwangosi amekubali kutoa kibali cha kujengwa mnara huo, hivyo baada ya ujenzi kukamilika Septemba 2, mwaka huuambayo ni siku aliyouwawa, Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk.Willbrod Slaa,ataweka jiwe la msingi na kuzungumza na wananchi.
Alisema siku hiyo pia kutafanyika harambee ya kuchangisha fedha kwa ajili ya kusaidia mjane wa Mwangosi na watoto wake.
Katibu huyo aliwataka wadau kusaidia kuchangia gharama za ujenzi wa mnara huo ili ujenzi uanzeharaka na kukamilika kwa wakati.
Mwangosi ambaye pia alikuwa Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Iringa, anadaiwa kuwawa wakati polisi walipofyatua mabomu wakati CHADEMA wakiwa katika harakati zakufungua tawi la chama hicho katika kijiji cha Nyololo.
Kabla ya kuuawa kwa mwanahabarihuyo, mabomu yalipigwa eneo hilo ili kuwatawanya wafuasi wa CHADEMA ambao walikuwa wakigoma kutawanyika eneo hilo na kuamua kukaa chini kuwa hawapo tayari kuondoka katika ofisiyao.
CHANZO: NIPASHE