Mwanaume usimwachie mkeo hela chumbani

Mwanaume usimwachie mkeo hela chumbani

madeinmusoma

JF-Expert Member
Joined
Jan 7, 2014
Posts
326
Reaction score
391
MWACHIE MBELE YA WATOTO NA UMWAMBIE NA MATUMIZI YAKE, NA WATOTO WASIKIE, USIJE KUISHI MAISHA YA UPWEKE UZEENI.



MWANAUME
Unamwachia mkeo hela ya chakula chumbani. Mke anatoka na kapu, anaenda kununua chakula. Anapika, anawaambia watoto, "njooni wanangu mle. Nimewapikia chakula kitaaamu!" Watoto wakishakula Wanasema "Asante Mama".

MWANAUME
Unamwachia mkeo hela ya nguo za sikukuu chumbani,
Kesho yake anatoka kwenda kununua nguo. Akirudi anawaambia, "wanangu nimewanunulieni nguo za sikukuu, njooni mjipimie!" Watoto wakishajipima, anawaambia, "Wanangu mmependeza eeeh! Si mnaona ninavyowapenda!?" Watoto wanafurahi na kusema, "Asante Mama".

MWANAUME
Kila aina ya pesa ya matumizi unamwachia mkeo chumbani...

MWANANUME
Ukifika muda wa kutoa ada unamkabidhi mkeo hela chumbani. Kesho yake mkeo anawaambia watoto kuwa anaenda kuwalipia ada ya shule. Akirudi anawaambia, "Wanangu nimeshawalipia ada, na gari za shule zitakua zinawapitia. Nataka msome wanangu ili baadae mje mnitunze". Watoto wanasema, "Asante Mama".

KIBAYA ZAIDI:
Ukifika muda wa kutoa adhabu, mkeo yeye hatoi adhabu. Anawaambia Watoto, "ngoja baba yenu arudi!" Na wewe ukirudi unaelezwa na mkeo matatizo ya wanao. Unachukua bakora unawaadhibu watoto bila kujua kuwa unazidi kujenga uhusiano M'BAYA na Wanao.

NGUMU KUMEZA
Ukifika uzeeni, watoto wako hawana KUMBUKUMBU yoyote Ya mema uliyowafanyia.

NA UKUMBUKE KUWA:
MTOTO ANAANZA KULISHWA SUMU YA MANENO KUTOKA KWA MAMAYAKE KUANZIA UMRI WA MIAKA 9 HADI 15.

MWANAUME KUWA MAKINI SANA

ZINGATIA HAYO KWA MAISHA YA UZEENI.
 
MWACHIE MBELE YA WATOTO NA UMWAMBIE NA MATUMIZI YAKE, NA WATOTO WASIKIE, USIJE KUISHI MAISHA YA UPWEKE UZEENI.



MWANAUME
Unamwachia mkeo hela ya chakula chumbani. Mke anatoka na kapu, anaenda kununua chakula. Anapika, anawaambia watoto, "njooni wanangu mle. Nimewapikia chakula kitaaamu!" Watoto wakishakula Wanasema "Asante Mama".

MWANAUME
Unamwachia mkeo hela ya nguo za sikukuu chumbani,
Kesho yake anatoka kwenda kununua nguo. Akirudi anawaambia, "wanangu nimewanunulieni nguo za sikukuu, njooni mjipimie!" Watoto wakishajipima, anawaambia, "Wanangu mmependeza eeeh! Si mnaona ninavyowapenda!?" Watoto wanafurahi na kusema, "Asante Mama".

MWANAUME
Kila aina ya pesa ya matumizi unamwachia mkeo chumbani...

MWANANUME
Ukifika muda wa kutoa ada unamkabidhi mkeo hela chumbani. Kesho yake mkeo anawaambia watoto kuwa anaenda kuwalipia ada ya shule. Akirudi anawaambia, "Wanangu nimeshawalipia ada, na gari za shule zitakua zinawapitia. Nataka msome wanangu ili baadae mje mnitunze". Watoto wanasema, "Asante Mama".

KIBAYA ZAIDI:
Ukifika muda wa kutoa adhabu, mkeo yeye hatoi adhabu. Anawaambia Watoto, "ngoja baba yenu arudi!" Na wewe ukirudi unaelezwa na mkeo matatizo ya wanao. Unachukua bakora unawaadhibu watoto bila kujua kuwa unazidi kujenga uhusiano M'BAYA na Wanao.

NGUMU KUMEZA
Ukifika uzeeni, watoto wako hawana KUMBUKUMBU yoyote Ya mema uliyowafanyia.

NA UKUMBUKE KUWA:
MTOTO ANAANZA KULISHWA SUMU YA MANENO KUTOKA KWA MAMAYAKE KUANZIA UMRI WA MIAKA 9 HADI 15.

MWANAUME KUWA MAKINI SANA

ZINGATIA HAYO KWA MAISHA YA UZEENI.
Nakubaliana na wewe, nina ushuhuda mi mwenyewe
 
Mimi mama yangu alikuwa anasema kabisa baba yenu kaacha pesa ya hiki na hiki hivyo akirudi jioni shart kwenda kusema asante kuhusu fimbo maza kanichapa sana kuliko hata mzee mwenyewe

Me katika maisha yangu nimeadhibiwa na mzee mara moja tu ila mama alinichakaza kwa vipigo na vifinyo
 
Sijui kwanini mwanamke ni mbinafsi ila ndio hivyo tuishi nao kwa akili tu

Nimeshuhudia mara nyingi sana watoto wakikuwa wakubwa wanavyolishwa maneno na mama zetu kuhusu makosa ya baba na yanapangiliwa vizuri kweli kiasi ukiwa na akili ndogo unamchukia mzee wako

NB: Kwa sisi wa kiume na wewe utakuwa baba alafu utaona anachopitia baba yako na wewe lazima kikukute tu
 
Inashauriwa kuwashirikisha watoto ambao tayari wamekua na wana uelewa kwenye mipango ya familia, hii inahusisha kuanzia kwenye kupanga bajeti ya matumizi ya nyumbani, ada za shule na mengineyo, ni vizuri pia wakishiriki kwenye manunuzi ya Sokoni na hata kwenye kusimamia utekelezaji wa bajeti ya familia, endapo watashirikishwa watajifunza yafuatayo:

1. Umuhimu wa kupanga bajeti kulingana na kipato

2. Nidhamu ya matumizi ya hela

3. Watajua mbinu na umuhimu wa ku bargain bei kabla ya kuamua kufanya manunuzi

4. Watajua faida na umuhimu wa kushirikishana kwenye mipango ya familia toka wakiwa wadogo

Endapo kwenye familia kuna uwazi na ushirikishwaji wa wanafamilia wote , hiyo hofu ya mleta mada itakuwa haina nafasi
 
Nachochukia ni kwamba mama sometimes huwa anakwazana na majirani (nadhani mnajua mambo ya wanawake). Hasa nikirudi likizo utakuta ananikataza ah usiombe au uazime hiki.
Me huwa nashangaa as long as hawa majirani huwa wanani treat vizuri tu.
Basi me huwa sishtuki huwa namuambia mama hiyo ni wewe & wao sio mimi & wao.
 
Hii mada nimeipenda sana, ngoja nisubiri comments za wadau huenda nikatoka na kitu
 
Nachochukia ni kwamba mama sometimes huwa anakwazana na majirani (nadhani mnajua mambo ya wanawake). Asa nikirudi likizo utakuta ananikataza ah usiombe au uazime hiki.
Me huwa nashangaa as long as hawa majirani huwa wanani treat vizuri tu.
Basi me huwa sishtuki huwa namuambia mama hiyo ni wewe & wao sio mimi & wao.
Acha ubishi adui wa rafiki yako ni adui yako na rafiki wa adui yako ni adui yako. Sasa we nenda ukipewa sumu huko uje unalialia.
 
Ilitakiwa usioe mwanamke mwenye roho mbaya. Kama mwanamke hana roho mbaya na wewe unajiamini roho yako sio mbaya huwezi kupata watoto wanaomkumbuka mama tu.

Mwanamke asiye na roho mbaya analea watoto sio kibinafsi bali kindugu, kiupendo hata wakikua wanashikamana. Kuchapa ni kawaida tu kwanza ndio ina balance tabia ya mtoto..

Baba anamnyoosha mtoto, mama anamdekeza hapo mtoto anakuwa na tabia iliyo balanced. Mtoto hakuchukii sababu unamchapa HAPANA. Hivi mtoto amrushie mwenzake kisu etu simchapi sababu atampenda mama ake sana Nooooo kwanza wengi wetu sisi bila bakora tusingekuwa hapa.

Mtoto alelewe kwa upendo na njia rahisi ya kufanya hivyo ni kupata mwanamke mwenye upendo na roho nzuri.Unaoa mwanamke mkipishana kidogo anatukana watoto siku nzima
 
Hlf ishu ya mtoto kumpendelea mama ni kawaida sababu hata sisi wanaume mtoto wa kiume una treat kibandidu wa kike unalegezea ..

Kuna zile imani kwamba mwanaume anaweza kustaimili wakati mwanamke hawezi. Mwanaume ameumbwa kutoa wakati mwanamke kupokea haya yote yanachangia kwanini mzazi wa kike anapata sana kuliko wa kiume..
 
Back
Top Bottom