Tabia ya wanawake kuwa wasagaji au angalau bi-sexual imekuwa ni kubwa sana Tanzania, na wengi wana wake zao au girl friend zao ambao hawajui ukweli huu kwani wanawake wengi wanaogopa kwamba wanaume wao wata waacha mara watakapogundua hilo. Kwa wale wenye uelewa au uzoefu wa suala hili, iwapo ni wewe, reaction yako ya kwanza itakuwa ni nini hasa iwapo umekuja kubaini suala hili baadae sana na baada ya yeye kuamua kuwa muwazi kwako kwamba anapenda jinsia zote huku tayari mkiwa ndani ya mapenzi moto moto ambayo hukuona kabisa dalili ya suala hili. Kina dada pia nahitaji mawazo na ushauri wenu.
Pia nini ni madhara ya kutoka na mwanamke msagaji? Na je kuna faida zozote pia tofauti na mwanamke ambae ni heterosexual? Mhusika (mwanamke) ni mpenzi wa wanawake zaidi kuliko wanaume lakini kwa kweli ananipenda ajabu na background yake ni kwamba yeye na familia yake ilikuwa abused sana na baba wa kambo wakiwa wadogo. Tukirudi kwenye mada kuu, anasema kwamba yupo tayari kuanza kuniletea mwanamke yoyote ninayemtaka (YOYOTE NCHINI) kisha tujumuike wote watatu (three some) ilimradi/badala ya mimi kutoka nje ya uhusiano kivyangu vyangu, yani nisim cheat.
Historia yangu
Nilikuwa natoka na single mother, nimeachana nae miezi kama nane iliyopita (kwa sasa ni marafiki zaidi huku tukipeana mchezo mara moja moja kutegemeana na mazingira), na nikampata mwanamke mwingine ambae sio single mother, mid 20s, mtanzania 100%, digital kidogo, na nikaanza kuendeleza uhusiano nae na baada ya miezi kama sita, ndio nimekutana na hili.