Mwanaume aliemwagia mchepuko wake Tindikali afariki Dunia

Mwanaume aliemwagia mchepuko wake Tindikali afariki Dunia

Frank Wanjiru

JF-Expert Member
Joined
Apr 12, 2012
Posts
25,443
Reaction score
46,198
images-166.jpg

Elvis Opiyo, Mwanaume aliyekuwa akikabiliwa na tuhuma za kuhusika katika kupanga shambulio la tindikali dhidi ya Mwimbaji wa Nyimbo za Injili Mary Clare Ochieng, ameripotiwa kufariki dunia katika eneo la Umoja, Nairobi.

Opiyo alikuwa nje kwa dhamana wakati akiendelea kukabiliwa na tuhuma kwamba alihusika kumlipa Mwanaume mwingine ili kumshambulia Clare kwa tindikali. Shambulio hilo lilimwacha Mwimbaji huyo akiwa na majeraha makubwa ya kuungua usoni na kwenye macho, hali iliyohitaji matibabu maalum.⁠

Tukio hilo lilitokea Machi 17, 2026, eneo la Kibera, ambapo Clare alishambuliwa alipokuwa akielekea nyumbani. Mshukiwa mwingine, Lucas Ochieng’, alidaiwa kumwambia Clare kwamba alikuwa ametumwa kufanya shambulio hilo na Opiyo.

Opiyo alikamatwa Machi 22 na kufikishwa katika Mahakama ya Kibera, huku uchunguzi ukiendelea kuhusu nafasi yake katika shambulio hilo.

Kifo chake kimeibua maswali mapya kuhusu kesi hiyo, ambayo ilikuwa bado haijafikia hitimisho la kisheria.

Viongozi wa Lamb’s Ministers wamethibitisha kifo chake na kutoa salamu za rambirambi, wakimtaja Opiyo kama mwenzao katika huduma ya Mungu na “ndugu katika Kristo.” Pia wametuma pole kwa familia na jumuiya ya Lighthouse Ministries.

Wakati huo huo, Mary Clare anaendelea kupatiwa matibabu kutokana na madhara makubwa aliyoyapata baada ya kushambuliwa kwa tindikali. Familia yake imekuwa ikitafuta msaada kwa ajili ya matibabu na upasuaji wa kurekebisha madhara yaliyosababishwa na shambulio hilo.
images-165.jpg
 
Back
Top Bottom