Mwanasheria Mkuu wa Serikali(AG), Waziri wa Sheria na hawa wajiuzulu mara moja

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Kutokana na sakata la kikatiba lililopata tiba ya tabu, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Ndugu George Mcheche Masaju; Waziri wa Sheria na Katiba Dr. Harrison Mwakyembe; Mshauri wa Rais wa Mambo ya Kisheria na timu nzima ya washauri wa Rais wanapaswa kujiuzulu.

Rais hakupaswa kuucheza mchezo alioucheza wa kumteuwa Dr. Possi kuwa Balozi. Rais hakupaswa 'kusimangwa' na kuzungumzwa vile ikiwa amezungukwa na wasomi wengi tu wa Sheria, tena wenye jukumu la kumshauri na kumuongoza Rais kwenye mambo ya kisheria.

Pamoja na kwamba Dr. Possi, kwa kuteuliwa Ubalozi, ameshapoteza sifa za kuwa Mbunge hata kama hatajiuzulu rais hakupaswa kushiriki kwenye mchezo mgumu kama ule kama angeshauriwa vyema. Masaju, Mwakyembe na wengineo wanapaswa kuwajibika au kuwajibishwa.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali ndiye Mshauri mkuu wa mambo ya kisheria kwa Serikali inayoongozwa na Rais. Alikuwa wapi? Waziri Mwakyembe,mbobezi wa sheria, na Waziri mwenye dhamana ya kulinda Katiba na Sheria alikuwa wapi? Washauri wa pale Ikulu walikuwa wapi?

Lazima wajiuzulu au waondolewe. Hakuna namna nyingine.

Mwafaaaa!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Arusha)
 
Hawawezi kujiuzulu hao jamaa na wala Bosi hao hawezi kuwatumbua kutokana na sakata hilo......

Kwa kuwa upo uwezekano mkubwa kuwa hao jamaa waliamua kuwa 'mabubu' na kutotoa ushauri wowote wa kisheria kwa Bosi wao kutokana na kujua hulka ya Bosi wao kuwa haambiliki wala hashauriki!

FULL STOP.
 
Rais anapoteua mawaziri anashaurina na PM pekee kwa mujibu wa katiba yetu, waziri/mwanasheria hashirikishwi hata kidogo
 
Kutokana na sakata la kikatiba lililopata tiba ya tabu, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Ndugu George Mcheche Masaju; Waziri wa Sheria na Katiba Dr. Harrison Mwakyembe; Mshauri wa Rais wa Mambo ya Kisheria na timu nzima ya washauri wa Rais wanapaswa kujiuzulu.

Rais hakupaswa kuucheza mchezo alioucheza wa kumteuwa Dr. Possi kuwa Balozi. Rais hakupaswa 'kusimangwa' na kuzungumzwa vile ikiwa amezungukwa na wasomi wengi tu wa Sheria, tena wenye jukumu la kumshauri na kumuongoza Rais kwenye mambo ya kisheria.

Pamoja na kwamba Dr. Possi, kwa kuteuliwa Ubalozi, ameshapoteza sifa za kuwa Mbunge hata kama hatajiuzulu rais hakupaswa kushiriki kwenye mchezo mgumu kama ule kama angeshauriwa vyema. Masaju, Mwakyembe na wengineo wanapaswa kuwajibika au kuwajibishwa.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali ndiye Mshauri mkuu wa mambo ya kisheria kwa Serikali inayoongozwa na Rais. Alikuwa wapi? Waziri Mwakyembe,mbobezi wa sheria, na Waziri mwenye dhamana ya kulinda Katiba na Sheria alikuwa wapi? Washauri wa pale Ikulu walikuwa wapi?

Lazima wajiuzulu au waondolewe. Hakuna namna nyingine.

Mwafaaaa!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Arusha)
Kuna wengine wako njiani kutoka ndio sababu ya kuteuliwa hao wa juzi. Lakini tunamshukuru Mkapa kwa kuokoa jahazi. Hata wakisema mazungumzo yalihusu burundi. Hapa ni akili ya Mkapa tu
 
Inawezekana walimshauri lakini kama mnavyojua umimi,ubabe,kupenda kujiona yeye ndoanajua kuliko mtu yoyote yule,kutokupenda kutii sheria japo anachokifanya anakijua ni makosa wanaomjua vizuri hili watakubaliana na mimi,hashauriki kwalolote lile wameona yanini bora aamue anachotaka
 
Kutokana na sakata la kikatiba lililopata tiba ya tabu, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Ndugu George Mcheche Masaju; Waziri wa Sheria na Katiba Dr. Harrison Mwakyembe; Mshauri wa Rais wa Mambo ya Kisheria na timu nzima ya washauri wa Rais wanapaswa kujiuzulu.

Rais hakupaswa kuucheza mchezo alioucheza wa kumteuwa Dr. Possi kuwa Balozi. Rais hakupaswa 'kusimangwa' na kuzungumzwa vile ikiwa amezungukwa na wasomi wengi tu wa Sheria, tena wenye jukumu la kumshauri na kumuongoza Rais kwenye mambo ya kisheria.

Pamoja na kwamba Dr. Possi, kwa kuteuliwa Ubalozi, ameshapoteza sifa za kuwa Mbunge hata kama hatajiuzulu rais hakupaswa kushiriki kwenye mchezo mgumu kama ule kama angeshauriwa vyema. Masaju, Mwakyembe na wengineo wanapaswa kuwajibika au kuwajibishwa.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali ndiye Mshauri mkuu wa mambo ya kisheria kwa Serikali inayoongozwa na Rais. Alikuwa wapi? Waziri Mwakyembe,mbobezi wa sheria, na Waziri mwenye dhamana ya kulinda Katiba na Sheria alikuwa wapi? Washauri wa pale Ikulu walikuwa wapi?

Lazima wajiuzulu au waondolewe. Hakuna namna nyingine.

Mwafaaaa!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Arusha)


Nadhani serikali hii ya kutumbua jambo kama hili haliwezi kupita hivi hivi. ni jambo la muhimu sana kwa mkuu kumuwajibisha mhusika aliyetakiwa kumshauri kuhusu jambo hili ili kutoa dira kwa watendaji wa serikali kwa ujumla.

watu wanasoma mitahasari ya mambo hawasomi kwa undani kuchunguza kila kifungu kinachohusika katika jambo alilopewa dhamana na matokeo yake ni ni kama haya.

cha kujifunza kwa kiongozi wetu ni kuwa yapo mambo mengi sana wananchi wanaumia inawezekana ni kwa makosa kama haya. Watu wanapolalamika hali mbaya mitaani basi watu wakae chini watafute kuna tatizo wapi maana mambo kama haya huwezi kuyaona kwenye vifungu vya sheria kulinganisha kama hivi bali ni mrejesho wake ni wananchi ambao serikali inatakiwa kuwahudumia kuwaletea unafuu wa maisha wanapoanza kulalamika kuwa kinachofanyika kinaongeza ugumu wa maisha.
 
Ngoja...kwani Rais sinilisikia katika teuzi za wabunge alizidisha na akawa wamesigina katiba badala ya kuteu wabunge 5 akateua 6?labda nikatika hali yakuweka sawa 5/5
 
Hakika sio kweli kuwa Rais anashauriana na PM tu, itakuwaje akateua mtu uwaziri wakati sio mbunge!
 
Yaani awamu hii ni uhovyo tu ndo umetawala. Katiba umewekwa kapuni na badala yake kinatumika kitabu cha ilani ya uchaguzi ya CCM.
 
Back
Top Bottom