Mwanamke wa sasa!

Bazazi

JF-Expert Member
Aug 18, 2008
2,806
3,476

Wazo letu la sasa juu ya wanawake ni kuwa mtaalamu, mtemedeni, mrembo na maridadi. Hukaidi ukubwa na utawala wa mwanaume katika mambo yote ya maisha. Hushindana na mwanaume kwa ajili ya uhuru wa maslahi na uchumi. Kinyume cha mwanamke wa zamani aliyekuwa mtumwa na mtumishi wa kazi ngumu kama kibarua. Mwanamke wa zamani alionekana mchana na usiku nyumbani na jikoni, kuzaa na kulea umati wa watoto, na mwenye lazima ya kufanya kazi ya kuangalia faraja ya bwana: mume wake.


Walakini mambo yamebadilika sasa. Kazi ya mwanamke sio utii. Hutaka usawa wa cheo na wa haki. Mwanamke wa sasa ni asi. Si vibaya kwa kadri mambo yaendeleavyo, lakini kujichukulia kibubusa – kama kipofu – kila litendwalo na mwanaume ili kuonyesha ulimwengu kuwa ana usawa ni upuzi pengine. Wanawake wameanza kuvuta sigara kwa sababu wanaume wanavuta. Huvaa suruali na mashati kwa sababu wanaume huvaa. Matokeo yake ni fujo kubwa. Hujui nani mwanaume au nani mwanamke!


Mipaka ya nguvu za mwanamke, hali hafifu, kuchoka upesi na moyo dhaifu humfanya hafai kwa kazi ngumu. Mwanamke ni malaika wa roho. Na apate usawa wa haki na wa cheo, lakini daraka lake katika maisha ni la Mapenzi, Huruma, Sanaa na hifadhi.
NB

  1. mtemedeni = aliyestaarabika, aliyeendelea
  2. asi = kutotii
  3. kibubusa = kipumbavu, kipofu, kama kipofu.


Shaaban Robert (1967). Diwani ya Shaaban 5: Insha na Mashairi. Thomas Nelson and Sons Ltd. Dar es Salaam. 105pp.
 
Hahahaaaaaaa! Bazazi kwanza nikupongeze kwa LUGHA SAFIII ULIYOTUMIA (NAMASHAKA UMECHAKACHUA NA KAMUSI PEMBENI) Ila kwa unadhifu wako na ufasahaa naomba nikupongeze kwa KAHAWA NA KASHATA KAMA KIBURUDISHO CHETU ASILI CHA WATU WA PWANI!!!!

Back to topic!!!! Napingana na wewe 100% sibishii msuli, ila nabishia logic!

1. Zamani MWANAMKE PAMBO TU YEYE NA KULETEWA TUU (GOAL KEEPER) ndo maana alishinda jikoni sababu alijua KATU JIKO HALITANUNA yakheeeee! Ila hizi zama za kina Kibelaaaaaa! Hamueleweki atiii! Ukijifanya Goalkeeper mbona utadaka nyavuuu! Hali yatufanya tutafute position maishani, Wajikuta mchezeshaji kiungo ili mambo ya balance, wengine wanaojasiria miili, wameamua kuwa MASTRAIKA atiii! Nyumbani tumemuachia Dada kama Beki tatu kuweka ulinzi golini!

2. Sasa kama na mie FIGHTER basi haki ziongezekeee! Na mie niafaidi jasho langu! Twarudi wote saa 1 usiku wewe umetoka Bank mie Skuliii kufundisha, Wote tumeingiza siku atiii, afu wataka nianze kuwasha mkaa we umeketi wasoma zako gazeti? La hashaaa! Katu haikubaliki!

3. Utemi saingine GENES tuu, wengine sie vizazi vya hawa wafuatao

Rahabu! (Alichomtenda mjeda mwakijua)
Mke wa isaka ( Alivowachakachua wanawe)
Esther! ( Alivomuingiza KING mfalme myahudi, mzima mzima)
Delila ( Alichomfanyia Samsoni)
Mke mpya wa Herode (Alivomwmbia bintie aombe kichwa cha Yohane!!!!)
Cleopatra ( Alivomtenda Kaisari wa watu.)

Yaani hata HISTORY inaonesha kuna PERCULIAR species za kike ambazo currently researchers wamezipa chromosome XXX badala ya XX ambazo ni NOMAAAAAAAA!!!!
 
Hahahaaaaaaa! Bazazi kwanza nikupongeze kwa LUGHA SAFIII ULIYOTUMIA (NAMASHAKA UMECHAKACHUA NA KAMUSI PEMBENI) Ila kwa unadhifu wako na ufasahaa naomba nikupongeze kwa KAHAWA NA KASHATA KAMA KIBURUDISHO CHETU ASILI CHA WATU WA PWANI!!!!

Back to topic!!!! Napingana na wewe 100% sibishii msuli, ila nabishia logic!

1. Zamani MWANAMKE PAMBO TU YEYE NA KULETEWA TUU (GOAL KEEPER) ndo maana alishinda jikoni sababu alijua KATU JIKO HALITANUNA yakheeeee! Ila hizi zama za kina Kibelaaaaaa! Hamueleweki atiii! Ukijifanya Goalkeeper mbona utadaka nyavuuu! Hali yatufanya tutafute position maishani, Wajikuta mchezeshaji kiungo ili mambo ya balance, wengine wanaojasiria miili, wameamua kuwa MASTRAIKA atiii! Nyumbani tumemuachia Dada kama Beki tatu kuweka ulinzi golini!

2. Sasa kama na mie FIGHTER basi haki ziongezekeee! Na mie niafaidi jasho langu! Twarudi wote saa 1 usiku wewe umetoka Bank mie Skuliii kufundisha, Wote tumeingiza siku atiii, afu wataka nianze kuwasha mkaa we umeketi wasoma zako gazeti? La hashaaa! Katu haikubaliki!

3. Utemi saingine GENES tuu, wengine sie vizazi vya hawa wafuatao

Rahabu! (Alichomtenda mjeda mwakijua)
Mke wa isaka ( Alivowachakachua wanawe)
Esther! ( Alivomuingiza KING mfalme myahudi, mzima mzima)
Delila ( Alichomfanyia Samsoni)
Mke mpya wa Herode (Alivomwmbia bintie aombe kichwa cha Yohane!!!!)
Cleopatra ( Alivomtenda Kaisari wa watu.)

Yaani hata HISTORY inaonesha kuna PERCULIAR species za kike ambazo currently researchers wamezipa chromosome XXX badala ya XX ambazo ni NOMAAAAAAAA!!!!

ich liebe die! :poa:poa:poa Kaizer njoo utafsiri!:A S-coffee:
 
Last edited by a moderator:
Bazazi una mambo! Nimefurahishwa na ubunifu wako kwa kuleta thread kwa staili tofauti kidogo.
Anyway kwa kuwa haya ni mashairi ya Shaaban Robert na tafiti zake, nisingependa kuongeza neno.
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom