Muda huu tunapoongelea uhuru wa miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika, kuna mwanamke hapa Chan'ombe Dodoma limemshuka, tena looooooooooooooote! Ameolewa ana miaka 9 ktk ndoa yake ingawa hajabahatika kuzaa ktk ndoa yake hii. Mumewe siku zote hakujua kuwa kabla ya kuoana alishazaa mtoto wa 'ujanani'. Hakumueleza mumewe wakati wa urafiki, uchumba na baada ya ndoa. Juzi huyo mtoto wake wa ujanani alokuwa akiishi na bibi alifariki hapa dodoma, hivyo ilibidi mama na mumewe waje dodoma, huku mume akijua kuwa mtoto aliyefariki alikuwa ni wa kaka wa mkewe. Hakukuwa na jipya lililoendelea zaidi ya hali ya majonzi miongoni mwa wafiwa.
Hali libadilika leo asubuhi wakati wa maandalizi ya kwenda kuzika wakati wa kuaga mwili. Mama alipoenda kwa jeneza, si ndo akaanza kulia kwamba anamuachia upweke kwani yeye ndiye alikuwa mwanawe pekee, ataishije bila kuwa na mtoto. Siku zote alikuwa akijivunia kuwa mzazi sababu ya yeye ingawa alikuwa akisemwa hazai na watu na majirani. Minong'ono ikawa mingi pale msibani baada ya kuona ameng'ang'ania kwa jeneza zaidi ya dk 5 ambapo ililazimu watu waende kumuondoa ili taratibu za mazishi ziende kama ilivyopangwa.
wakati minong'ono ikiendelea ndipo mumewe alipojua na kuthibitish kwamba kumbe mtoto aliyekuwa akimjua kama mpwa wa mkewe, ukweli alikuwa ni mtoto wa mkewe. Jamaa alimaindi sana, na nusura aondoke msibani ila busara ya wazee ilisaidia jamaa abaki msibani na kuendelea na mazishi. Ajabu mara baada ya kurudi mazishini, pamoja na juhudi za wazee na ndugu kumuomba baki ili waliongelee hilo, jamaa alifungasha vitu vyake na kurudi dar, pamoja na juhudi za mkewe kumsihi ili wamalize issue hii kabla ya kurudi zao dar na mumewe. Hakuna nayejua nini kitafuatia baada ya 'aibu' hii kujulikana.
My take: Chondechonde kina dadana wanaume pia, kama mtu kakupenda epuka kumdanganya issue ambazo ziko wazi kama hii au kabila yako. Mambo hayo hayana kificho yatakuja julikana tu. Na ukweli utakapojulikana utakosa pa kuuficha uso wako.
Mie nawataja kama wataniua waniue ila ukweli ndio huo..... Wanawake wa kabila la kirangi wengi wana hiyo tabia sana ya kuficha watoto...ni makabila gani yanaongoza kwa kuficha ukweli? hili ni muhimu kulifahamu ili mtu unapotafuta mchumba ukidondokea kwenye hilo kabila ufanye full check up....nyumbakubwa tufahamishe pls..
Mie nawataja kama wataniua waniue ila ukweli ndio huo..... Wanawake wa kabila la kirangi wengi wana hiyo tabia sana ya kuficha watoto...
Back to topick: ni ulimbukeni wa hali ya juu na naungana na aliyesema kuwa ni kumnyima mtoto haki yake ya msingi...kama mwanaume kakupenda hata ukimwambia umezaa watoto 10 hawezi kukuacha, kwani kuwa na mtoto/watoto ni dhambi kwenye jamii? Tena basi hakuna dhambi mbaya kama mwanamke mzima na akili zako unabeba mimba miezi 9 kisha unazaa kwa uchungu afu eti unakutana na mtoto wa mwanamke mwenzio unamkana mwanao loooh.... Ni aibu kumtelekeza mtoto kijijini kwa bibi na kumlazimisha akuite shangazi/ dada/ mamdogo n.k..
Huyo mwanaume nae hovyoooo......kususa msibani maana yake nini sasa?? Au alidhani yale aloambiwa ndo yatageuka miujiza?? Atleast hata mwanamke hakughasi kwa malezi, kuna mijanaume mingine inasubiri mpaka ikishakuweka ndani ndo unaanza kuletewa orodha ya watoto, mmoja baada ya mwingine utadhani unasajili wacheza mpira bana!!! Sio issue kabisa waungwana, kutakiana lawama tu!
Muda huu tunapoongelea uhuru wa miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika, kuna mwanamke hapa Chan'ombe Dodoma limemshuka, tena looooooooooooooote! Ameolewa ana miaka 9 ktk ndoa yake ingawa hajabahatika kuzaa ktk ndoa yake hii. Mumewe siku zote hakujua kuwa kabla ya kuoana alishazaa mtoto wa 'ujanani'. Hakumueleza mumewe wakati wa urafiki, uchumba na baada ya ndoa. Juzi huyo mtoto wake wa ujanani alokuwa akiishi na bibi alifariki hapa dodoma, hivyo ilibidi mama na mumewe waje dodoma, huku mume akijua kuwa mtoto aliyefariki alikuwa ni wa kaka wa mkewe. Hakukuwa na jipya lililoendelea zaidi ya hali ya majonzi miongoni mwa wafiwa.
Hali libadilika leo asubuhi wakati wa maandalizi ya kwenda kuzika wakati wa kuaga mwili. Mama alipoenda kwa jeneza, si ndo akaanza kulia kwamba anamuachia upweke kwani yeye ndiye alikuwa mwanawe pekee, ataishije bila kuwa na mtoto. Siku zote alikuwa akijivunia kuwa mzazi sababu ya yeye ingawa alikuwa akisemwa hazai na watu na majirani. Minong'ono ikawa mingi pale msibani baada ya kuona ameng'ang'ania kwa jeneza zaidi ya dk 5 ambapo ililazimu watu waende kumuondoa ili taratibu za mazishi ziende kama ilivyopangwa.
wakati minong'ono ikiendelea ndipo mumewe alipojua na kuthibitish kwamba kumbe mtoto aliyekuwa akimjua kama mpwa wa mkewe, ukweli alikuwa ni mtoto wa mkewe. Jamaa alimaindi sana, na nusura aondoke msibani ila busara ya wazee ilisaidia jamaa abaki msibani na kuendelea na mazishi. Ajabu mara baada ya kurudi mazishini, pamoja na juhudi za wazee na ndugu kumuomba baki ili waliongelee hilo, jamaa alifungasha vitu vyake na kurudi dar, pamoja na juhudi za mkewe kumsihi ili wamalize issue hii kabla ya kurudi zao dar na mumewe. Hakuna nayejua nini kitafuatia baada ya 'aibu' hii kujulikana.
My take: Chondechonde kina dadana wanaume pia, kama mtu kakupenda epuka kumdanganya issue ambazo ziko wazi kama hii au kabila yako. Mambo hayo hayana kificho yatakuja julikana tu. Na ukweli utakapojulikana utakosa pa kuuficha uso wako.
Kuna kabila moja so far ndio nimekuja ku conclude wana hiyo tabia saaana. Wakizaa ujanani wanaficha kuanzia mimba mpaka mtoto. Jirani yetu alikuja kujua mtoto wa mkewe siku binti anafunga ndoa; MC akasema mama wa bibi harusi, kasimama mama ambaye sote tulijua ni dada yake na ndo alomlea watu wakabaki midomo wazi. From there ndo tukajua kumbe alikuwa mtoto wake. Mumewe alimind kishenzi ila ndio hivyo walishakaa kwenye ndoa more than 20 years na wana watoto wengine.
Nina rafiki yangu nae watu wanasema chini chini (wamejua from reliable source) ana mtoto alimzaa akiwa form two; nayo ni siri sirini. Na alikuja kuolewa na kuachika bila ku mention kuwa ana mtoto. Sasa ana mtoto mmoja kwa ex hubby wake.
BUT it is not fair kwa hao watoto wanaonyimwa haki ya kuita mama zao "Mama" very selfish behavior indeed!
Mie nawataja kama wataniua waniue ila ukweli ndio huo..... Wanawake wa kabila la kirangi wengi wana hiyo tabia sana ya kuficha watoto...
Back to topick: ni ulimbukeni wa hali ya juu na naungana na aliyesema kuwa ni kumnyima mtoto haki yake ya msingi...kama mwanaume kakupenda hata ukimwambia umezaa watoto 10 hawezi kukuacha, kwani kuwa na mtoto/watoto ni dhambi kwenye jamii? Tena basi hakuna dhambi mbaya kama mwanamke mzima na akili zako unabeba mimba miezi 9 kisha unazaa kwa uchungu afu eti unakutana na mtoto wa mwanamke mwenzio unamkana mwanao loooh.... Ni aibu kumtelekeza mtoto kijijini kwa bibi na kumlazimisha akuite shangazi/ dada/ mamdogo n.k..
kwa hiyo sijapatia...?mkuu hitimisho linalotokana na hisia halina mashiko ndugu
Uongo ndio tatizo. . . wengi hawajali kulea/ matumizi wanajali kutokuambiwa ukweli.Hivi mtu anakudanganya kuwa alikua na mtoto unakuja kugundua unakasirika vibaya,tatizo linakua hasa wapi?Uongo uliolishwa au ni mtoto uliekua hata humlei?Au ni mazoea?
Hivi mtu anakudanganya kuwa alikua na mtoto unakuja kugundua unakasirika vibaya,tatizo linakua hasa wapi?Uongo uliolishwa au ni mtoto uliekua hata humlei?Au ni mazoea?