Mwanamke kumuambia mwanaume anavyotongozwa

Freyzem

JF-Expert Member
Jun 29, 2013
10,061
24,484
Kuna hili suala la wanawake kutongozwa kisha kumwambia mwanaume kuwa ametongozwa na flani na ameahidiwa kitu gani.

Binafsi limenitokea mara kadhaa, kuna wanawake ambao ni marafiki tu wa kawaida ninakuwa nao wamekuwa wakinieleza pale wanapotokewa na wanaume.

Takribani asilimia kubwa hata kama ni marafiki wapya wa kike nimekutana na hili jambo, hivi nia kubwa inakuwa ni nini? Halafu imekuwa kwamba yule anayetongozwa anasema amemkataa huyo aliyemtongoza na anakuwa anamponda.

Sasa humu bila shaka kuna wenye tabia hiyo, hivi huwa nia ya mwanamke kutongozwa na kimwambia mwanaume ambaye hata siyo mume/mchumba au hajawahi kukutaka ni nini? Wanaume mliokutana na hili suala kama mpo mlichukuliaje?
 
hapo mkuu ni kweli.. kama kati yao hujatafuna basi wamekuona hauna madhara hivyo wanaona mnafanana tu kijinsia... fanya uwatafune ulinde heshima..!
 
Anakuona NYUKI WA MASHINENI AU NYOKA WA KIBISA HAUNA MADHARA HATA AKIKWAMBIA....Ndio haohao watakuja kukuharibia baadae ukiloba step..Chunga sana..kaa nao mbali
 
ukiona unaambiwa maneno hayo alaf huyo mwanamke sio mpenzi wako

ujue una tabia za umbea umbea wanawake wanakuona kama shosti yao ndio mana wanakwambia hiyo ipo siku watakuagiza vitunguu na nyanya
Siyo kweli kiongozi...
 
nishauri wakuu tuwe tunapunguza makali ya maneno aisee... wengine wanakuja na ishu seriously sasa tukiwa na majibu ya chooni kama haya hatutayajenga humu!
 
Back
Top Bottom