Leo nina zawadi mbili (Moja ni hii na ya pili itafata) kutoka kiumeni kwenda kwa wake zetu vipenzi, kwenda kwa dada zetu, kwenda kwa mama zetu kwenda kwa walezi wetu wa kike. Leo nawasemea Wanawake kwa ujumla wao. Hakika hali wa shani Mwanamke hawezi kuvumilia kuishi na mwanaume anaye mnyanyasa.
1. Hata ukiwa tajiri kumzidi Mansa Kan Kan Musa mtawala wa Mali, mja ambaye aliyepewa utajiri wa dhahabu na akazigawa kama pipi kwa watu wenye kuhitajia, aliishi karne ya 13 Miladia mja huyu. Ukimnyanyasa lazima atakuacha na utajiri wako na kwenda sehemu isiyo na manyanyaso.
2. Hata ukiwa mzuri kumzidi nabii Yusufu (Japo hakuna aliye mzidi mja huyu) maadamu utamnyanyasa tu mwanamke, basi kaa ukijua lazima atakuacha na uzuri wako.
3. Hata uwe Mfalme wa kutawala majini na watu (Japo hakuna kwa leo hii) ila mwana wa Daudi yule "The King of the Vast Kingdom" namzungumzia nabii Suleyman, maadamu utamnyanyasa mwanamke, jua mwanamke huyo atashika njia na kukuacha na ufalme wako.
Juu ya nukta hizo tatu kuna mifano mingi, sababu jambo hili liko wazi, hakuna haja ya kuhudhurisha mifano hiyo.
Tuwapende wake zetu na tusiwanyanyase, japo kati yao na sisi,sisi ndiyo tunapenda zaidi kuliko wao, ndiyo maana majukumu ya kuwatunza na kuwalisha na kuwasimamia tukapewa sisi.
Kibwagizo
Wanaume tunasifiwa kuoa wake wengi na hatusifiwi ushupavu wala hela sababu hivi tunavitafuta, kwani wapo wenye hela wana mke mmoja kama tochi (Wana waogopa wake zao kama ukoma) sijui likizima ataenda kuazima kwa jirani,mpaka lije kuwaka nanga isha paa na jua limekucha.
1. Hata ukiwa tajiri kumzidi Mansa Kan Kan Musa mtawala wa Mali, mja ambaye aliyepewa utajiri wa dhahabu na akazigawa kama pipi kwa watu wenye kuhitajia, aliishi karne ya 13 Miladia mja huyu. Ukimnyanyasa lazima atakuacha na utajiri wako na kwenda sehemu isiyo na manyanyaso.
2. Hata ukiwa mzuri kumzidi nabii Yusufu (Japo hakuna aliye mzidi mja huyu) maadamu utamnyanyasa tu mwanamke, basi kaa ukijua lazima atakuacha na uzuri wako.
3. Hata uwe Mfalme wa kutawala majini na watu (Japo hakuna kwa leo hii) ila mwana wa Daudi yule "The King of the Vast Kingdom" namzungumzia nabii Suleyman, maadamu utamnyanyasa mwanamke, jua mwanamke huyo atashika njia na kukuacha na ufalme wako.
Juu ya nukta hizo tatu kuna mifano mingi, sababu jambo hili liko wazi, hakuna haja ya kuhudhurisha mifano hiyo.
Tuwapende wake zetu na tusiwanyanyase, japo kati yao na sisi,sisi ndiyo tunapenda zaidi kuliko wao, ndiyo maana majukumu ya kuwatunza na kuwalisha na kuwasimamia tukapewa sisi.
Kibwagizo
Wanaume tunasifiwa kuoa wake wengi na hatusifiwi ushupavu wala hela sababu hivi tunavitafuta, kwani wapo wenye hela wana mke mmoja kama tochi (Wana waogopa wake zao kama ukoma) sijui likizima ataenda kuazima kwa jirani,mpaka lije kuwaka nanga isha paa na jua limekucha.

