Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,322
- 33,126
Mama afariki, mtoto aokolewa
Mwanamke mmoja amefariki dunia Jijini Dar es Salaam baada ya kunywa sumu ya panya ambayo pia alimnyesha mwanae mwenye umri wa miaka sita.
Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, Faustine Shilogile amesema, tukio hilo la kuhuzunisha lilitokea jana mishale ya saa 8:00 mchana.
Amemtaja mwanamke huyo ambaye hivi sasa ni marehemu kuwa ni Samia Mwambata, 36, mkazi Ilala Mchikichini.
Akisimulia tukio hilo, Kamanda Shilogile amesema mwanamke huyo alikunywa sumu hiyo ya panya Septemba 26 mwaka huu, na kisha akamnywesha mwanae aitwaye Leice Gerard, 6, kwa nia ya kumuua.
Amesema baada ya tukio hilo, mwanamke huyo na mwanae walikimbizwa katika hospitali ya Amana kwa ajili ya matibabu.
Hata hivyo amsema ilipofika jana mishale ya saa 8:00 mchana, mwanamke huyo alifariki dunia.
Amesema mwanae Leice, alitibiwa na kuruhusiwa kurudi nyumbani siku hiyo hiyo aliyonyweshwa sumu na mama yake.
Kamanda Shilogile amesema sababu za kifo hicho ni mwanamke huyo kuambiwa na ndugu zake kuwa ana tabia mbaya.
Amesema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Amana na Polisi wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.
http://ippmedia.com/
Mwanamke mmoja amefariki dunia Jijini Dar es Salaam baada ya kunywa sumu ya panya ambayo pia alimnyesha mwanae mwenye umri wa miaka sita.
Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, Faustine Shilogile amesema, tukio hilo la kuhuzunisha lilitokea jana mishale ya saa 8:00 mchana.
Amemtaja mwanamke huyo ambaye hivi sasa ni marehemu kuwa ni Samia Mwambata, 36, mkazi Ilala Mchikichini.
Akisimulia tukio hilo, Kamanda Shilogile amesema mwanamke huyo alikunywa sumu hiyo ya panya Septemba 26 mwaka huu, na kisha akamnywesha mwanae aitwaye Leice Gerard, 6, kwa nia ya kumuua.
Amesema baada ya tukio hilo, mwanamke huyo na mwanae walikimbizwa katika hospitali ya Amana kwa ajili ya matibabu.
Hata hivyo amsema ilipofika jana mishale ya saa 8:00 mchana, mwanamke huyo alifariki dunia.
Amesema mwanae Leice, alitibiwa na kuruhusiwa kurudi nyumbani siku hiyo hiyo aliyonyweshwa sumu na mama yake.
Kamanda Shilogile amesema sababu za kifo hicho ni mwanamke huyo kuambiwa na ndugu zake kuwa ana tabia mbaya.
Amesema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Amana na Polisi wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.
http://ippmedia.com/