Chakaza
Platinum Member
- Mar 10, 2007
- 41,009
- 74,643
Hivi ni kweli alikuwa msanii?
Yap! Ni kweli. Ni wale wale akina Kingwendu na the company. Sasa anadhani kila mahala ni maigizo.
Hivi ni kweli alikuwa msanii?
aliyekwambia huyu mwanahabari nani? mimi nammjua kama msanii wa maigizo
Ukiandika vizuri tu utapeli weka bila kuweka haya sijui trite 'mafumbo'!Mdomo Wake Tu Umekaa Kichuchunge Na Macho Yake Nayo Yamekaa Kisanii Sanii Je Wewe Ulitegemea Mbichwa Wake Utoe Madini Kama Ya Mtani Wangu Balile? Na Ili Kudhihirisha Kuwa Huyo Sina Malengo Ni POPOMA Unaambiwa Eti Yeye Ndiyo Afisa Uhusiano Wa Ile Redio Iliyouzwa Iitwayo Njia Ya Kwenda Mbinguni Na Nadhani Uliona Jinsi Balile Na Wale Wanafunzi Akina Mansoor Na Juma Walivyomdharau Na Kiukweli Leo Sina Malengo Ameumbuka Na Amejiaibisha. Huyo Ndiyo Mwanadiplomasia Wetu Siku Za Baadae.
Je Ulisikia Lile Dongo La Mwisho Ambalo Balile Alimtupia Sina Malengo? Siku Nyingine Akijua Kuwa Anakwenda Studio Halafu Mgeni Mwingine Ni Balile Awe Anachomoa Tu Kwani Napenda Mno Balile Alivyokuwa Akimdhihaki Kidiplomasia Kwa Mfano Kuna Sehemu Balile Alimwambia Kuwa Hicho Chuo Cha Diplomasia Unachosoma Wewe Sasa Mimi Nimesoma Hapo Miaka 11 Iliyopita. Hapo Sina Malengo Nilimwona Alivyonywea Kwani Kiuwezo Kumpambanisha Ktk Vipindi Vya Hoja Balile Na Sina Malengo Wa Mawingu Iliyouzwa Ni Sawa Na Kumpambanisha Daniel Sturridge Wa Liverpool FC Na Juma Javu Wa Yanga FC.
Muda mfupi uliopia nilikuwa natazama kipindi cha "Jicho letu ndani ya habari" kinachorushwa na star tv.
Kama kawaida, kipindi hiki kilikuwa kinajadili namna magazeti yalivyoripoti habari za wiki nzima na kwa wiki hii mjadala mkubwa ulikuwa ni kuhusu kuhojiwa na Tume ya Maadili kwa mama Tibaijuka na mwenzake Andrew Chenge.
Waalikwa katika kipindi hicho walikuwa ni mhariri Balile na mwanahabari Simon Simalenga kwa upande wa studio za Dar-es-salaam.Na kwa upande wa Mwanza, wageni walikuwa ni wanafunzi wawili wanaosomea uandishi wa habari katika chuo cha SAUT Mwanza.
Kauli ya mama Tibaijuka kuwa alitumia shilingi milioni 10 kununulia mboga ilichukua nafasi katika mazungumzo hayo kwani iliripotiwa sana na vyombo vya habari.
Ilipofika zamu ya mwandishi Simalenga kutakiwa kutoa maoni yake juu ya kauli hiyo ya mama Tibaijuka,kwanza alianza kwa kurejea kauli za kejeli zilizopaswa kutolewa na viongozi wengine siku za nyuma ambapo aliitaja kauli ya Mramba kuwa hata watanzani wakila nyasi lazima ndege ya raisi lazima inunuliwe;kauli ya Andrew Chenge, kuwa mabilioni yale ni vijisenti na kauli hii mpya ya mama Tibaijuka.
Cha ajabu,alianza kwa kusema yeye huwa haamini maneno ya kusikia mpaka ashuhudie mwenyewe akimanisha kuwa haamimi kama kauli hizo ziliwahi kutolewa na viongozi hao.Huo ulikuwa ni kama utangulizi tu.
Aliponishangaza zaidi mwandishi huyu ni pale alipojaribu kuetetea kauli ya mama Tibaijuka kuwa, milioni 10 ilikuwa ni hela ya mboga tu kwa kusema "inawezekana hiyo milioni 10 mama Tibaijuka alitumia kununulia mboga kwa ajili ya shule anayomiliki".
Yaani hapa mwandishi huyu alikuwa anajaribu kutuambia kuwa, alichomanisha prof.Tibaijuka ni kuwa, milioni 10 zile labda alizitumia kununulia mboga kwa ajili ya wanafunzi wa shule yake na kwamba waandishi wenzake walitakiwa wachunguze kauli ile kabla ya kuiripoti tu kama ilivyotolewa.
Swali;
Je,inawezekana mwanahabari huyu yuko sahihi na kwamba waandishi wenzake walitakiwa kuifanyia utafiti kauli ile kwanza kabla ya kuiripoti?
Hayo ni makosa ya Star TV. Huwezi kuleta mjadala mkubwa unaogusa jamii halafu ukaalika watu wenye uelewa finyu wa mambo kujadili kama huyo Simalenga. Alichokisema Simalenga ndio mwisho wa uwezo wake katika kuchambua unategemea nini zaidi? Kama kituo cha TV kinachotazamwa na watu wengi tena wengine wenye uelewa mkubwa lazima utafute Watu Bora wa kujadili sio bora watu, maana nia ya kupata majawabu ya kusudio yatapotea kabisa.
Mfano unaleta mada "Kwa nini Tanzania pamoja na rasilimali ilizo nazo bado inaendelea kuwa masikini?" Halafu wachangiaji wa mada hiyo unamuweka Nape Nnauye au Livingstone Lusinde unategemea kupata nini zaidi ya kuharibika kwa mjadala? Star TV wanapaswa kuliangalia hilo maana wamekuwa na tabia hiyo mara nyingi sana ya kuleta mada ya msingi ila watu wasio kidhi vigezo kujadili.
Mleta mada ungeandika "mwanafunzi huyu" ndo ungekuwa sahihi zaidi kwani aliyekuwa anahojiwa ni mwanafunzi wa uandishi wa habari na si mwanahabari, lakini ukweli lipo tatizo katika uandaaji wa vipindi vya star tv, utakuta mwandaaji na wongozaji wa kipindi wote mbugila sasa unategemea nini?
Ukiandika vizuri tu utapeli weka bila kuweka haya sijui trite 'mafumbo'!
Ukiandika vizuri tu utaeleweka bila kuweka 'mafumbo'Sijauelewa Utumbo Wako Hebu Urudie Tena.