Salary Slip
Platinum Member
- Apr 3, 2012
- 52,643
- 164,790
Muda mfupi uliopia nilikuwa natazama kipindi cha "Jicho letu ndani ya habari" kinachorushwa na star tv.
Kama kawaida, kipindi hiki kilikuwa kinajadili namna magazeti yalivyoripoti habari za wiki nzima na kwa wiki hii mjadala mkubwa ulikuwa ni kuhusu kuhojiwa na Tume ya Maadili kwa mama Tibaijuka na mwenzake Andrew Chenge.
Waalikwa katika kipindi hicho walikuwa ni mhariri Balile na mwanahabari Simon Simalenga kwa upande wa studio za Dar-es-salaam.Na kwa upande wa Mwanza, wageni walikuwa ni wanafunzi wawili wanaosomea uandishi wa habari katika chuo cha SAUT Mwanza.
Kauli ya mama Tibaijuka kuwa alitumia shilingi milioni 10 kununulia mboga ilichukua nafasi katika mazungumzo hayo kwani iliripotiwa sana na vyombo vya habari.
Ilipofika zamu ya mwandishi Simalenga kutakiwa kutoa maoni yake juu ya kauli hiyo ya mama Tibaijuka,kwanza alianza kwa kurejea kauli za kejeli zilizopaswa kutolewa na viongozi wengine siku za nyuma ambapo aliitaja kauli ya Mramba kuwa hata watanzani wakila nyasi lazima ndege ya raisi lazima inunuliwe;kauli ya Andrew Chenge, kuwa mabilioni yale ni vijisenti na kauli hii mpya ya mama Tibaijuka.
Cha ajabu,alianza kwa kusema yeye huwa haamini maneno ya kusikia mpaka ashuhudie mwenyewe akimanisha kuwa haamimi kama kauli hizo ziliwahi kutolewa na viongozi hao.Huo ulikuwa ni kama utangulizi tu.
Aliponishangaza zaidi mwandishi huyu ni pale alipojaribu kuetetea kauli ya mama Tibaijuka kuwa, milioni 10 ilikuwa ni hela ya mboga tu kwa kusema "inawezekana hiyo milioni 10 mama Tibaijuka alitumia kununulia mboga kwa ajili ya shule anayomiliki".
Yaani hapa mwandishi huyu alikuwa anajaribu kutuambia kuwa, alichomanisha prof.Tibaijuka ni kuwa, milioni 10 zile labda alizitumia kununulia mboga kwa ajili ya wanafunzi wa shule yake na kwamba waandishi wenzake walitakiwa wachunguze kauli ile kabla ya kuiripoti tu kama ilivyotolewa.
Swali;
Je,inawezekana mwanahabari huyu yuko sahihi na kwamba waandishi wenzake walitakiwa kuifanyia utafiti kauli ile kwanza kabla ya kuiripoti?
Kama kawaida, kipindi hiki kilikuwa kinajadili namna magazeti yalivyoripoti habari za wiki nzima na kwa wiki hii mjadala mkubwa ulikuwa ni kuhusu kuhojiwa na Tume ya Maadili kwa mama Tibaijuka na mwenzake Andrew Chenge.
Waalikwa katika kipindi hicho walikuwa ni mhariri Balile na mwanahabari Simon Simalenga kwa upande wa studio za Dar-es-salaam.Na kwa upande wa Mwanza, wageni walikuwa ni wanafunzi wawili wanaosomea uandishi wa habari katika chuo cha SAUT Mwanza.
Kauli ya mama Tibaijuka kuwa alitumia shilingi milioni 10 kununulia mboga ilichukua nafasi katika mazungumzo hayo kwani iliripotiwa sana na vyombo vya habari.
Ilipofika zamu ya mwandishi Simalenga kutakiwa kutoa maoni yake juu ya kauli hiyo ya mama Tibaijuka,kwanza alianza kwa kurejea kauli za kejeli zilizopaswa kutolewa na viongozi wengine siku za nyuma ambapo aliitaja kauli ya Mramba kuwa hata watanzani wakila nyasi lazima ndege ya raisi lazima inunuliwe;kauli ya Andrew Chenge, kuwa mabilioni yale ni vijisenti na kauli hii mpya ya mama Tibaijuka.
Cha ajabu,alianza kwa kusema yeye huwa haamini maneno ya kusikia mpaka ashuhudie mwenyewe akimanisha kuwa haamimi kama kauli hizo ziliwahi kutolewa na viongozi hao.Huo ulikuwa ni kama utangulizi tu.
Aliponishangaza zaidi mwandishi huyu ni pale alipojaribu kuetetea kauli ya mama Tibaijuka kuwa, milioni 10 ilikuwa ni hela ya mboga tu kwa kusema "inawezekana hiyo milioni 10 mama Tibaijuka alitumia kununulia mboga kwa ajili ya shule anayomiliki".
Yaani hapa mwandishi huyu alikuwa anajaribu kutuambia kuwa, alichomanisha prof.Tibaijuka ni kuwa, milioni 10 zile labda alizitumia kununulia mboga kwa ajili ya wanafunzi wa shule yake na kwamba waandishi wenzake walitakiwa wachunguze kauli ile kabla ya kuiripoti tu kama ilivyotolewa.
Swali;
Je,inawezekana mwanahabari huyu yuko sahihi na kwamba waandishi wenzake walitakiwa kuifanyia utafiti kauli ile kwanza kabla ya kuiripoti?