Mwanae hanitaki kabisa, nifanyeje?

sheikh yasin

Member
Joined
Aug 6, 2015
Posts
61
Reaction score
50
Wakuu,

Kuna huyu mama wa makamo ana 51 kwa sasa, kuna kazi ya matibabu nilimfanyia, huwa anasumbuliwa sana na mgongo, na mimi ni Herbalist, nina kijifrem changu Mwanza ambapo nafanya shughuli hizi.

Sasa huyu mama baada ya kufahamiana kwa muda tukajikuta tumekuwa wapenzi na baadae akaniomba nihamie kwake tuweze kuishi pamoja, kwamba yeye kwa makamo yale hawezi kuhamia kwangu, nikakubali nikahamia kwake, yupo vizuri sana kwa kweli, anaishi na watoto wake hapo, mmoja wa kiume 21 na mwingine 19 wa kike, kuna aliyeolewa yupo kwake.

Sasa huyu wa kiume yaani hanipendi kama nini sijui, hanisalimii wakati namzidi mbali nina 34, nikitoka na gari la mama yake ananitazama kama mtu ameona mavi. Ni mwanachuo, akiwa anamuomba mama yake pesa akinyimwa anakosa adabu kabisa na kumjibu kwamba mbona huyo mtu wako unampa hela.

Wakati yule binti mwingine wala hana neno na mimi, ananiamkia na kuniheshimu na huwa tunatoka nae outing mara kadhaa na mama yake.

Huyu kijana amekuwa akinizungumza vibaya hata kwa ndugu wengine wanaokuja nyumbani, imekua ni kero sana.

Naomba mawazo yenu
 
You're dating his mother, not him. Mwambie mama yake. Kama amemshindwa, kubali tu. It goes with the territory.
 
Kuna huyu mama wa makamo ana 51 kwa sasa,Mimi Nina 34,
hivi mkuu utakuheshimu vipi wakati unatembea na mtu
ambaye yey anamlinganisha na rika la bibi (kumbuka mtoto wake
mwingine kaolewa).
Pia hesabu za chekechea , fanya hivi.
Kikongwe 51-34 = 17 (variance na kikongwe)
34-21 =13 (variance na kijana).
34-19 =15 (viarance na binti).
je, unadhani hapo utaheshimika vipi hapo...?
 
I feel sorry for the boy! Anajua na ana akili, anajua wewe ni Mario tu huna lolote. Huwezi kumpenda mama yake mwenye miaka 51 ukaacha wasichana/wanawake level yako. Anajua umefuata hela za mama yake tu,tena huyo kijana ni mstaarabu wengine wangekufanyia, useless opportunist.
 
sijui nikuulizeje juu ya izo maaandishi rangi nyekundu
 
Hata ungekuwa ww ndio mama yako huyo nahic ungefanya zaidi ya hilo..
 
Ila mkuu, huyo mama ni kwamba umemwoa au tuuite vipi hayo mahusiano na wewe kwenda kuhamia kwake. Mi sioni kama kuna future yoyote kati yenu, labda useme umeamua kula tu maisha na huyo mama
 
Duh....sijui nichangie nini maana nimesoma mpaka mwisho still bado natafakari..hila poa ngoja niache tu
 
ingekuwaje kama wewe ndo kijana halafu unamuona mama yako anaingiza serengetiboy ndani ??...halafu wewe ni kama kaka yake tu maana kwa makamo yako wala haujamuacha mbali na isitoshe anaona unalelewa tu hadi unamzibia matumizi yake.jiongeze wewee
 
Huna sifa za kuwa baba ndo maana anakudharau. Kilichokupeka kwa huyo kikongwe ni njaa zako kwa ukitaka kuendelea kuishi hapo jitahidi kumnyenyekea huyo dogo
 
Wewe si bure umelogwa, ujasiri huo umeupata wapi? Au fedha ndio zimikuvuta? Naamini unam beep is lael akupigie ktk ya barabara. Jiandae kupoteza uhai. Fedha hazitafutwi kwa njia ya mtelemko
 

Attachments

  • ImageUploadedByJamiiForums1447941190.648669.jpg
    34.8 KB · Views: 801
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…