Mwana jf, busara yako hapa ni muhimu sana!

MAKOLE

JF-Expert Member
Feb 5, 2012
618
280
Kwa muda mrefu sasa waajiri wangu walinipa kibarua na kufanya kazi peke yangu hadi nikafikiria kuomba msaada kutoka kwa mabosi wangu watafute namna ya kuongeza wafanyakazi ili pindi ninapochoka au kuugua (kwa maana mimi ni mwanadamu) wafanye kazi badala yangu.

Kwa kweli waajiri wangu walikataa kata kata kuajiri wafanyakazi wengine hapa ofisini lakini mimi nikalazimisha hata wakakubali ingawa kwa shingo upande. Waliajiriwa watumishi wengi katika ofisi hii ambayo shughuli yetu kubwa ni kuendesha chombo baharini. Nimeshindwa kabisa kujizuia na nimejikuta nikiwa chanzo cha migogoro mingi hapa ofisini.

Yaelekea uzee nao unachamgia kwani waajiriwa wapya wengi ni vijana ambao wanao uwezo wa kwenda kasi sawa na mawimbi ya bahari yaendavyo. Najihisi sasa nimekuwa kikwazo. Wakati mwingine nalazimika kuwafitinisha hawa waajiriwa wenzangu kwa muajiri wetu ili nionekane bado nahitajika na nina umuhimu sana chomboni, hivyo hawa waajiriwa wenzangu hukabiliana na matatizo na wanatazamwa kwa jicho baya na hawa waajiri wetu.

Katika hali ya kawaida ndugu zangu wana JF, natakiwa kufanya nini ili walau basi nami nitazamike mwenye busara pamoja na mvi zangu nilizonazo kichwani?

Msaada tafadhali!
 
Mkuu kama tayari unajijua una tatizo, unataka nini tena? Tatizo huwa ni tatizo kama wewe mwenye nalo hujijui kama una tatizo, lakini kwa kuwa tayari umeshalijua, na tayari unajijua kwamba ni mkosefu, tubu mbele za Mungu na mbele za marafiki zako, halafu uache mara moja kuwaharibia wenzako. Siku wakigundua watakuzamisha baharini, take care!
 
Ikiwa kuna shughuli nyingine nje ya kuendesha chombo majini waambie mabosi wako wakuhamishishie huko, au omba uwe mkuu wa usimamizi wa hao waajiliwa vijana maana uzee wako ndio busara ya uratibu wa mambo!

Kama hakuna njia basi tafuta kazi nyingine nje ya hapo!
 
Mkuu tumia busara kuishi na hao vijana, hizo fitna zinamwisho. Ukweli ni kwamba your time soon will be come, nikimaanisha kuwa your knowledge itakuwa invaluable. Inatakiwa uonyeshe hekima yako, ninaamini utakuwa wewe ni more experience than them kikazi zaidi, use them wisely utaheshimika na utakuwa na nafasi yako.

Halafu acha hizo fitna, rizki atoa mungu bwana!
 
kama umefika muda wa kustaafu fanya hivyo au unahitajika kubadilika na kwenda na kasi ya vijana,sa ingine jishushe tu kama vitu huvijui au umesahau,relax,
 
Acha kazi, umeshakuwa 'obsolete item'
na wazee wengi wako hivi ofisini sijui tatizo ni nini, wanaichukia damu changa sana.

Bora kajiajiri, hata ukipewa kuwasimamia utawafrustrate tu, maana wao wanakuja na mawazo mapya wakati mwingine compitent kuliko wewe.

Huna miradi yako ukasimamie? Hata kama ni ufugaji wakuku?
 
Ha ha ha, Makole, I hate you for this.
You will surely pay big tym.

Kongosho, Mamzalendo, Madamex, Yericko Nyerere na Lukolo, thanks wpte na ninyi ni vichwa. Kwa ambaye atauchukulia huu uzi kijuu juu atashindwa kunielewa. hili ni fumbo na ninyi mmefumbua ingawa hamjafika ninapotaka. Mmeweza kuishauri C.C.M njia nzuri ya kuamua. hayo mliyoyasema yatawafaa C.C.M kwa maana huyo mzee ni C.C.M yetu. Ahsanteni sana.
 
Back
Top Bottom