Mwampamba Amjibu Dr Slaa

Mwampamba Amjibu Dr Slaa

ibange

JF-Expert Member
Joined
Dec 31, 2010
Posts
1,543
Reaction score
553
Hawa vijana walikuwa wameandaliwa sana na CCM kumwangamiza Dr Slaa na CHADEMA. Angalia majibu yake kweye FB yake. Ila kwa kweli hakuna madhara yeyote CHADEMA itapata kutokana na wasaliti hawa zaidi tu itazidi kujiimarisha. RIP Mwampamba, Shonza et al

MAJIBU YA DR.SLAA DHIDI YA UBADHILIFU WA MILLIONI 140

"Hoja ya kujikopesha kwa sura ya ufisadi ni "mfu" nimetamka nilikopa 20 kwa kuwa watumishi wa vyama hawawezi kukopa kwingine. Aidha siyo 140 Million. Zote 20 m zililipwa awamu ya mwisho June 2012. Hivyo hakuna deni la chama tena.
2. Josephine hajawahi kulipwa hata senti mmoja na chama kwa ziara za Mikoani, wala kwa shughuli yeyote ile isipokuwa wakati wa kesi Arusha alipokuwa na mtoto wa miezi 3 na tulihitaji yaya"

... SWALI
Wewe Mzee hoja siyo kwamba umekopa na kurudisha, hoja hapa ni je kwa mujibu wa Katiba, Kanuni, Miongozo na Taratibu za Chama cha CHADEMA kuna utaratibu wa mwanachama au Kiongozi kukopo na kisha kurejesha? kama upo ni acha wanachama wa kawaida je ni Viongozi wangapi wameshawahi kukopesha na CHADEMA kisha wakarejesha? weka wazi hapa na siyo kulete hadithi za ni kweli nilikopa sasa nimerudisha hiyo siyo hoja. Hoja hapa umetumia Ibara ya ngapi ya Katiba ya CHADEMA kukopa? au umetumia Kanuni namba ngapi ya Kanuni za CHADEMA kukopa, au umetumia kipengele cha ngapi cha Taratibu au Miongozo ya CHADEMA kukopa?.

Lakini pili unaposemanimetamka nilikopa 20 kwa kuwa watumishi wa vyama hawawezi kukopa kwinginesikuelewi, hivi hakuna Taasisi za kukuwezesha wewe kukopa? Mbona Mwenyekiti wako Mbowe alikopa NSSF. Kuna Mabenki, kuna SACCOS n.k lakini hizo zote haziwezi kukukopesha ila umeona CHADEMA ndiyo inaweza kukukopesha eti?
Ni aibu kubwa sana kwa Kiongozi anayesema ni mtetezi wa kupiga ufusadi wewe ndo umekuwa mstari wa mbele kuchochea ufisadi. Ufisadi siyo kuiba pesa tu hata kuzitumia au kukopeshwa kinyume na Taratibu zozote hata kama umezirejesha.

NATAKA KUKUONA UNATOKA HADHARANI na kuwaambia wanachama wako kuwa umekiuka Katiba, Kanuni, Taratibu na Miongozo ya CHADEMA.Ninaposema CHADEMA ni NGO unaweza kusimama na kusema siyo hivyo? kama siyo NGO au SACCOS unawezaje kwenda kukopa kwenye Chama cha Siasa. Hivi kumbe CHADEMA ni CHAMA CHA MAENDELEO NA DEMOKRASIA kwa maana ya kuweza kukopeshana?

Wanachama wa CHADEMA amkeni hizi ni zile kidogo zilizojulikana hiyo mijihela ya M4C waulize inakwenda wapi? Tazama na hii unayomtetea Mzinifu mwenzako Josephine"isipokuwa wakati wa kesi Arusha alipokuwa na mtoto wa miezi 3 na tulihitaji yaya" haya ni mambo ya Kitoto ambayo hayatakiwi kufanywa na Kiongozi wa ngazi ya juu kama wewe. kwa hiyo Katiba au Taratibu za Malipo za CHADEMA zinasemaje kwa mtu ambaye siyo Kiongozi wa chama lakini mume au mkewe ni Kiongozi wa Chama. Kama mtu huyo siyo Kiongozi eti kwa sababu ana mtoto na kwa kuwa anahudhuria kesi basi alipwe pesa na CHADEMA kwa kuwa mumewe ni Kiongozi ili aweze kuhudhuria kesi? HUU NI UPUUZI MWINGINE wa matumizi mabaya ya Fedha za Chama
 
Kijana acha kuweweseka, hakuna jambo la ajabu lililofanyika hapo kwa kiongozi kukopeshwa, umeshafuatilia na vyama vingine ukajua hali ya kifedha ikoje? Usipige kelele bila sababu, Acha Mzee awatumikie watanzania, kama unatamani kuhujumu chama sidhani kama utafanikiwa kwa hili, sana wewe ni msaliti!
 
Kwanza hawa jamaa walituambia ni milioni 140, huwaoni hapo wanajichanganya kwa kushupalia jambo wasilolijua/ ama kuwa na uhakika nalo? Kama walikuwa hawana hakika na kiasi hiki, tutamwamini vipi katika malalamiko yao mengine yenye utata pia?. Hapo sasa naanza kuamini kuwa hawa jamaa walitumwa kuwachafua viongozi wao na chama chao.
 
acheni ----- wenu nchi ina mambo mengi ya maana ya kujadili au ndo mnatumika!!!
 
Mwampamba kweli wewe ni kijana makini majibu yako ni kisu kwa Dr Slaa na wafuasi wake wote.

kama ni kijana makini na anaona kukopa ni ufisadi ampeleke mahakamani.vinginevyo itakuwa ni njaa tu inamsumbuwa.
 
Hawa vijana walikuwa wameandaliwa sana na CCM kumwangamiza Dr Slaa na Chadema. Angalia majibu yake kweye FB yake. Ila kwa kweli hakuna madhara yeyote chadema itapata kutokana na wasaliti hawa zaidi tu itazidi kujiimarisha. RIP Mwampamba, Shonza et al

MAJIBU YA DR.SLAA DHIDI YA UBADHILIFU WA MILLIONI 140

"Hoja ya kujikopesha kwa sura ya ufisadi ni "mfu" nimetamka nilikopa 20 kwa kuwa watumishi wa vyama hawawezi kukopa kwingine. Aidha siyo 140 Million. Zote 20 m zililipwa awamu ya mwisho June 2012. Hivyo hakuna deni la chama tena.
2. Josephine hajawahi kulipwa hata senti mmoja na chama kwa ziara za Mikoani, wala kwa shughuli yeyote ile isipokuwa wakati wa kesi Arusha alipokuwa na mtoto wa miezi 3 na tulihitaji yaya"

... SWALI
Wewe Mzee hoja siyo kwamba umekopa na kurudisha, hoja hapa ni je kwa mujibu wa Katiba, Kanuni, Miongozo na Taratibu za Chama cha Chadema kuna utaratibu wa mwanachama au Kiongozi kukopo na kisha kurejesha? kama upo ni acha wanachama wa kawaida je ni Viongozi wangapi wameshawahi kukopesha na CHADEMA kisha wakarejesha? weka wazi hapa na siyo kulete hadithi za ni kweli nilikopa sasa nimerudisha hiyo siyo hoja. Hoja hapa umetumia Ibara ya ngapi ya Katiba ya CHADEMA kukopa? au umetumia Kanuni namba ngapi ya Kanuni za CHADEMA kukopa, au umetumia kipengele cha ngapi cha Taratibu au Miongozo ya CHADEMA kukopa?.

Lakini pili unaposemanimetamka nilikopa 20 kwa kuwa watumishi wa vyama hawawezi kukopa kwinginesikuelewi, hivi hakuna Taasisi za kukuwezesha wewe kukopa? Mbona Mwenyekiti wako Mbowe alikopa NSSF. Kuna Mabenki, kuna SACCOS n.k lakini hizo zote haziwezi kukukopesha ila umeona CHADEMA ndiyo inaweza kukukopesha eti?
Ni aibu kubwa sana kwa Kiongozi anayesema ni mtetezi wa kupiga ufusadi wewe ndo umekuwa mstari wa mbele kuchochea ufisadi. Ufisadi siyo kuiba pesa tu hata kuzitumia au kukopeshwa kinyume na Taratibu zozote hata kama umezirejesha.

NATAKA KUKUONA UNATOKA HADHARANI na kuwaambia wanachama wako kuwa umekiuka Katiba, Kanuni, Taratibu na Miongozo ya CHADEMA.Ninaposema CHADEMA ni NGO unaweza kusimama na kusema siyo hivyo? kama siyo NGO au SACCOS unawezaje kwenda kukopa kwenye Chama cha Siasa. Hivi kumbe CHADEMA ni CHAMA CHA MAENDELEO NA DEMOKRASIA kwa maana ya kuweza kukopeshana?

Wanachama wa CDM amkeni hizi ni zile kidogo zilizojulikana hiyo mijihela ya M4C waulize inakwenda wapi?Tazama na hii unayomtetea Mzinifu mwenzako Josephine"isipokuwa wakati wa kesi Arusha alipokuwa na mtoto wa miezi 3 na tulihitaji yaya" haya ni mambo ya Kitoto ambayo hayatakiwi kufanywa na Kiongozi wa ngazi ya juu kama wewe. kwa hiyo Katiba au Taratibu za Malipo za CHADEMA zinasemaje kwa mtu ambaye siyo Kiongozi wa chama lakini mume au mkewe ni Kiongozi wa Chama. Kama mtu huyo siyo Kiongozi eti kwa sababu ana mtoto na kwa kuwa anahudhuria kesi basi alipwe pesa na CHADEMA kwa kuwa mumewe ni Kiongozi ili aweze kuhudhuria kesi? HUU NI UPUUZI MWINGINE wa matumizi mabaya ya Fedha za Chama[/QUOT
Umefika wakati vijana tufanya kazi kwa nguvu zote il kukidhi mahitaji yetu. Kelele zote hizi za Mwampamba ni kwa sasababu ya njaa. Hivi wewe tangu umekuwa mwanachama ushakichangia chama shilling ngap? Ndo tabu wa kuwapatia vyeo watu wasiokuwa na input yoyote kwenye chama zaidi ya kutafuta namna wanavyoweza kujinuifaisha na chama. Dr.we nikiboko, umewabana kona zote wakashindwa kufuja mali za chama sasa wanapiga mikelele! Usiwasikilize, we piga kazi tu. MUNGU yuko upande wako.
 
Mwampamba ana kura ngapi? Kama unamsikiliza huyu nawe pia utakuwa mpuuzi

Tatizo siyo kumsikiliza Mwampamba tatizo kwa nini Dr Slaa akope pesa za ruzuku katibu ya Chadema inasemaje.
 
Bahati mbaya sana kwa kijana kama huyu kukubali kutumiwa, na sasa siasa itamshinda mapema. Kila mtu anafahamu CDM inatafutwa kila dakika na wanaotumiwa ni wale waliondani ya CDM ambao njaa zinawasumbua kama huyu kijana. Lakini kila mnapogundulika ndo hivyo tena mnafukuzwa na kazi yenu ndiyo imeisha!
 
Hapa ishu sio masalia wala nini. CHADEMA inapaswa kutoa majibu ya kisomi kama tunavyoamini kuwa ni chama makini.

Kuna wale ambao wamekuwa mahiri ku quote vifungu vya katiba kama akina Ben Saanane, Shardcole na Molemo. Hebu saidieni umma ni utaratibu upi wa CDM unaruhusu kukopa ndani ya CHADEMA?

Ikigundulika kama taratibu zilifuatwa, hapatokuwa na isuue na hawa wanaoitwa masalia watapuuzwa. Kushindwa kufanya hivyo, ni kuthibitisha kwamba huo ni ufisadi kama ulivyo ufisadi mwingine.
 
Madogo na staili yao ile ile imechosha na imepoteza mvuto kuamini kuwa kuna mantiki yoyote wanayojenga,
mwanzoni mliwatushtua baadhi ya watu lakini sio baada ya Ben kupasua pazia la hekalu lenu....
Hangaikeni na maisha mengine achananeni na CDM kama kweli kipo kama mnavyotaka watu wawaamini
 
Mbona swali la kitoto? Kwani mkopo unatolewa kwa asiyeomba? Ndo kilichomwondoa cdm? Si angemwuliza hayo akiwa huko? SITAKI NCHEKE.
 
Vijana mnaendelea kuonyesha mnavyotumika na Magamba, hasa Habibu Mchange, Mwampamba na huyo dada aliyejiunga na Chadema kwa maelekezo ya CCM. Mmekwama harakisheni kuwafuata Masalia wenzenu
CHADEMA inasonga mbele hamna ubavu wa kuizuia
 
Mdogo wangu Mwampamba Pole sana, maisha nje ya chama ( cdm ) kwako wewe ni sawa na maisha ya Dagaa Mchele nje ya Bahari , huna uwezo wa kubomoa Cdm , hukuwahi kuwa na uwezo huo , na wala hautakuja kuwa nao , wakati CDM inaanzishwa , namaanisha siku zile za miaka ileee , kama ungekuwa demu basi ningesema kwamba ulikuwa bado hata ' hujavunja ungo ' , Najua kwamba Maisha yako ni magumu sana , kwa vile huna kazi ! Bali hiyo kazi uliyojipa tegemea kudhalilika zaidi ! Nakushauri achana na hao wanaokutumia , soon watakutupa kwenye pipa la taka , tafuta kazi , hata kama wewe ni mwalimu wa Civics , usione aibu , bado utaitwa mwalimu tu , lakini ukubali kwenda shule zetu za kata kule Nanjilinji maana kwa mujibu wa Mh .Amim a.k.a Mulugo ni kwamba nafasi za mjini zimejaa .
 
Back
Top Bottom