Mwambe kugombea uenyekiti CHADEMA sio alitafuta sababu ya kuondokea?

jd41

JF-Expert Member
Aug 23, 2015
3,756
4,842
Wanabodi salaam!.

Naomba niende moja kwa moja kwenye mada yangu ambayo imekuja kwa mtindo wa swali. Hii ni kutokana na uungwaji mkono wa Mbowe kwa wajumbe wengi wa mkutano mkuu wa CHADEMA kwa kupata ushindi mzito, kweli Mwambe hakuifahamu nguvu ya mshindani wake mkuu?, au aliifahamu ila akaamua kujitumbukiza huko makusudi ili akishindwa apate sababu ya kuondokea?.

Pia, kauli iliyowahi kutolewa na mwenyekiti wa CCM kumkaribisha Mwambe arudi nyumbani, naona kama Mwambe aliamua kutafuta sababu ya 'kijanja' zaidi
kuondokea CHADEMA na isionekane ni kwasababu ya ushawishi aliopewa na mwenyekiti wa CCM, ili kuficha ukweli uliowazi kwamba ni salama zaidi kwake kugombea jimbo lake kupitia tiketi ya CCM alipokaribishwa na mwenyekiti wake kuliko kubakia CHADEMA ambapo nafasi ya ushindi ni finyu kutokana na tuliyoyashuhudia kwenye chaguzi ndogo zilizopita miaka ya karibuni.

Kutokana na taarifa zilizopo, Mwambe hakuwepo ukumbini wakati wa kumtangaza mshindi, licha kuitwa mara tatu lakini hakuweza kuonekana. Hii inaweza kuwa ni kwasababu alishapenyezewa matokeo, lakini kiungwana kwasababu aliamua kwa utashi wake kugombea, bila kushawishiwa na yeyote, nilitegemea angekuwepo mpaka mwisho wa uchaguzi kutangazwa matokeo ili nae kama mshindani aweze kutoa salamu zake. Hii inadhihirisha kumbe Mwambe hana ujasiri huo aliokuwa anajinasibu nao wakati wa kampeni, kama angepewa chama angeweza vipi kukiongoza, kama jambo dogo tu la kuvumilia kutangazwa matokeo lilimshinda?!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwani kaondoka ?

Kumuandama hivi Cecil Mwambe baada ya kugombea uenyekiti kunahalalisha madai ya wale wanaosema uenyekiti wa Mbowe CDM ni wa wakudumu na kwamba anayediriki kugombea anashughulikiwa.

Nyie vijana wa BAVICHA mmejifunza wapi siasa nyie mbona mnathinking capacity ndogo sana sometimes ?

Ningewaona wa maana sana kama mngempongeza Mwambe kwa kuonyesha nia ya kuongoza chama kikuu cha upinzani nchini na kukaa kimya, kama kweli yeye ni pandikizi muda utasema.

Siasa ni strategy siyo makelele ya kipuuzi kama haya baada ya uchaguzi badala ya nyinyi kuendelea kujadili mustakbali mpya wa chama nyinyi mko busy kumzodoa Mwambe.

Hovyo kabisa. jd41,
 
Mamluki wa Lumbumba huyo - mwache aende kama mwenzake alivyotoka nduki na kura zake za HAPANA huku akiwa mgombea pekee. haijaahi kutokea ni record aisee yaani upo peke yako watu bado wanakugomea..!!
 
Leo kumpongeza mshindi imegeuka ushujaa, kumbe inauma kususiwa pongezi na washindani wako.... mara ngapi tumeshuhudia wagombea wa CHADEMA wakisusa kuhudhuria hafla za uapisho wa washindi Ikulu..?
 
Alafu unataka kabisa system nzima ya tz ikae iamue kuwapa nchi chadema?

Ujinga mwingine bwana.

Sent using Jamii Forums mobile app
Wana ccm uchaguzi wa Chadema umeisha na wenyewe wameridhika na ulivyo endeshwa. Mbona mnanung'unika kama vile uchaguzi wa mwenyekiti ulikuwa Chadema VS CCM na faulu zimefanyika kuionea CCM?
Nendeni mkajiulize mnakosea wapi hadi mnaporomoka ushawishi kwa kasi ya Nazi mtini? Kwa nini pamoja na vitisho, mauaji na kujeruhiwa Chadema inazama mioyoni mwa RAIA? Wapi mnakosea? Jibu mnalo wenyewe na gundu lenu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wana ccm uchaguzi wa Chadema umeisha na wenyewe wameridhika na ulivyo endeshwa. Mbona mnanung'unika kama vile uchaguzi wa mwenyekiti ulikuwa Chadema VS CCM na faulu zimefanyika kuionea CCM?
Nendeni mkajiulize mnakosea wapi hadi mnaporomoka ushawishi kwa kasi ya Nazi mtini? Kwa nini pamoja na vitisho, mauaji na kujeruhiwa Chadema inazama mioyoni mwa RAIA? Wapi mnakosea? Jibu mnalo wenyewe na gundu lenu!

Sent using Jamii Forums mobile app
Hawa ni machangudoa wa kisiasa tuwadharau tu makahaba.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kilichotokea mlimani city 18/12/2019 hata marekani na uingereza wamebaki mdomo wazi wakijiuliza "how is it possible?"

Marekani ipi na Uingereza ipi iliyojiuliza hilo swali? Kwani wametoa official statement mahala? Kwani walihudhuria uchaguzi? Au wametweet mahali?

Come with FACTS not FICTIONS
 
Kwani kaondoka ?

Kumuandama hivi Cecil Mwambe baada ya kugombea uenyekiti kunahalalisha madai ya wale wanaosema uenyekiti wa Mbowe CDM ni wa wakudumu na kwamba anayediriki kugombea anashughulikiwa.

Nyie vijana wa BAVICHA mmejifunza wapi siasa nyie mbona mnathinking capacity ndogo sana sometimes ?

Ningewaona wa maana sana kama mngempongeza Mwambe kwa kuonyesha nia ya kuongoza chama kikuu cha upinzani nchini na kukaa kimya, kama kweli yeye ni pandikizi muda utasema.

Siasa ni strategy siyo makelele ya kipuuzi kama haya baada ya uchaguzi badala ya nyinyi kuendelea kujadili mustakbali mpya wa chama nyinyi mko busy kumzodoa Mwambe.

Hovyo kabisa. jd41,
Usiwe mkali sana mkuu japo naihisi ukweli flaani hivi kwenye maelezo yako.
Ukweli ni kwamba Mwambe aliamua hasa kuogelea dimbwini ila tu alisahau kazi ya kupiga mikambi na mitindo yake, akashindwa kuonekana upande wa pili.
 
Marekani ipi na Uingereza ipi iliyojiuliza hilo swali? Kwani wametoa official statement mahala? Kwani walihudhuria uchaguzi? Au wametweet mahali?

Come with FACTS not FICTIONS
Hata wasiposema popote, ni viburi vyao tu ila ukweli ndo huo.
 
Back
Top Bottom