Jayfour_King
JF-Expert Member
- Nov 15, 2009
- 1,135
- 128
Hizi zote ni kelele tu za kuelekea kwenye majimbo ya uchaguzi hakuna kipya. Nchi kimaadili ya uongozi iko taabani. Nakumbuka wakati taarifa hii (Richmond) inatolewa kwa mara ya kwanza pale bungeni nilijua sasa nchi imeamka ki maadili. Lakini kumbe si lolote si chochote tuko palepale.
Kelele zote tunazopiga ni sawa na za mbwa asiye na kucha wala meno, inashangaza kuona jinsi serikali inavyocheka na wezi huku ikiwa imetumia pesa za walipa kodi wa nchi hii kutafuta habari ambayo baada ya ukweli kujulikana hakuna hatua yoyote iliyo na inayo chukuliwa, huu ni usaliti dhidi ya ustaarabu kimaadili ya uongozi.
Kelele zote tunazopiga ni sawa na za mbwa asiye na kucha wala meno, inashangaza kuona jinsi serikali inavyocheka na wezi huku ikiwa imetumia pesa za walipa kodi wa nchi hii kutafuta habari ambayo baada ya ukweli kujulikana hakuna hatua yoyote iliyo na inayo chukuliwa, huu ni usaliti dhidi ya ustaarabu kimaadili ya uongozi.