Mwakyembe amehamishwa yeye na Treni yake

Mwakyembe amehamishwa yeye na Treni yake

K.Msese

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2012
Posts
2,385
Reaction score
3,032
Ni kawaida yetu Waafrika tulio wengi, mzazi anapofariki (kama ana miliki biashara), basi na biashara alioiacha nayo itakufa! Dalili zimeshaanza kuonyesha, kuhamishwa kwa Mh. Mwakyembe kwenda wizara nyingine, kutafifisha miradi na sera zake zote.....na pengine kumvunja moyo huyu muheshimiwa!

Ni siku ya pili leo tangia Mh. Mwakyembe awe ameanza kufanya kazi katika Wizara yake Mpya, lakini pia ni siku ya pili leo tangu Treni ya abiria inayofanya shughuli zake za kubeba abiria kati ya Stesheni na Ubungo kutofanya hivyo, tena bila maelezo yeyote kwa wateja wake!

Ukiziona nyuso za abiria wanaosubiri treni hiyo kwa usafri, hakika ni za uzuni mkubwa sana! Na hawana imani tena juu ya ubunifu huu wa Mwakyembe kwa swala la treni, kama utadumu! Mh. Mwakyembe alikuwa mkali sana kuhakikisha huduma hii ya kuwakomboa wananchi wengi wa jiiji la Dar es Salaam na adha ya usafiri inasimama imara, hivyo siamini kabisa kama Mh. Sitta ataweza kufanya the same!

Sisi wapenzi wa soka, tunafananisha kitendo cha kumwamisha Harrison Mwakyembe kutoka Wizara ya Uchukuzi na kwenda Wizara ya Africa Mashariki ni sawa na kumwambia Critiano Ronaldo aache kushambulia na kufunga mabao, na aende golini kudaka kuwa kipa!
 
Hii kitu imenilazimisha kurudi kwenye foleni niliyokuwa nishaisahau kwa kipindi kirefu.
 
Poleni sana wakuu,tuungane pamoja kuiondoa serikali isiyo sikivu ya ccm.
 
Tuone mzee wa kasi na viwango. Isije ikawa kasi na viwango vya kujaza tumbo lake. Kajichokea baada ya sumu ya Katiba ya vijisenti
 
Hivi usimamizi wa treni lazima umuhitaji Mwakyembe pekee?

Kama ni hivyo basi Watanzania tutaendelea kuwa watumwa wa wanasiasa...

Na hata suala la maendeleo endelevu litakuwa ni ndoto kwetu...
 
Tuone mzee wa kasi na viwango. Isije ikawa kasi na viwango vya kujaza tumbo lake. Kajichokea baada ya sumu ya Katiba ya vijisenti

Mzee Sita yy ni Mnoko lakini Si Mchapa kazi atakachofanya ni kupiga dili tu na kila atakayefurukuta ni kufutwa kazi , na huenda Bandari ikaludi kuwa mbaya na wizi kurejea kwa kasi ya Hatari .
 
ujinga mtu sasa huko afrika mashariki anaenda kuongoza nn...amemtoa sehemu ya maana kampeleka sehemu ya kibwege huyu mzee anatutia sana aibu watu wa pwani
 
Mlipenda sana wakati mafisadi wanachochea moto nikaona na wenzangu na mie hapa nao wanapiga siasa eti Jk mvivu,habadilishi mawaziri Mara hop,hamkujua ukianza na moja mbili na moja ipo karibu ..msubiri myaone matunda yenu ya kuondoa mawaziri,tulieni hivyo hivyo ili utamu uwakolee
 
Back
Top Bottom