Mwacheni RA Aseme, kabla na yeye..

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Sakata la Richmond na mtikisiko wake bado havijaisha Bungeni. Kuna kila dalili kuwa yaliyotokea Bungeni mwezi wa pili na kusababisha kujiuzulu kwa Waziri Mkuu na kuvunjika kwa baraza la Mawaziri hayakuwa mwisho. Kuna kila dalili kuwa kuna baadhi ya watu ambao waliumizwa na hadi hivi sasa hawajakubali "yaishe"


2008-04-13T21_38_36-07_00.jpg
Miongoni mwa watu ambao kwa hakika waliumizwa hisia zao, hadhi na sifa zao ni Mbunge wa Igunga Mhe. Rostam Aziz (CCM) ambaye wakati wa matukio hayo alidai kuwa ripoti iliyosomwa na Mwenyekiti wa Kamati Teule ya Bunge Mhe. Harrison Mwakyembe (Kyela - CCM) haikuwa sahihi na akadai kama vile wengine kuwa hakutendewa haki.

Juhudi za kujisafisha kwa wahusika mbalimbali wa Richmond zimekuwa zikiendelea na kwa namna fulani jukumu kubwa zaidi linamuangukia Bw. Rostam ambaye aidha kwa kujitwisha mwenyewe au kukubali kutumika inaonekana amekuwa akitumia kila aina ya njia upande mmoja kujibu mashambulizi ya wapinzani kwa kutumia vyombo vyake vya habari na upande wa pili kutilia shaka utendaji mzima wa Kamati Teule na hivyo kujaribu kuhoji maamuzi yote yaliyotolewa Bungeni

Katika kikao kinachoendelea cha Bunge alitakiwa aje kutoa maelezo yake na kujibu hoja za Wabunge na kutoa utetezi wake. Mwishoni mwa juma alikuwa amejiandaa kutoa utetezi huo lakini kwa kile kinachodaiwa kuwa ni "unyeti" wa utetezi wake basi imeonekana si vyema kwa Bw. Rostam kujitetea Bungeni kwani italeta msukosuko mwingine nchini

Kama hilo ni kweli au ni mojawapo ya karata za CCM binafsi siamini kuwa Rostam anaweza kusema chochote kile ambacho kinaweza kutuyumbisha kama Taifa na ambacho hatuwezi kukihimili. Tumeweza "kuchafuka kwa hali ya kisiasa Zanzibar", tumeweza kuhimila msiba wa Sokoine, tumeweza kuhimili "mizengwe" ya Kizota na kifo cha Katibu Mkuu Kolimba na kwa hakika tumeweza kuhimila kujiuzulu kwa WAziri Mkuu

Naamini nchi yetu inaweza kuhimili msuko suko wowote ule wa kisiasa hata kama ni kujiuzulu kwa Rais aliyeko madarakani! Hata ikibidi Bunge zima kujiuzulu au kuvunjwa na kuitisha uchaguzi mwingine, TAifa letu lina uwezo wa kuhimili mambo hayo kwani Taifa ni kubwa zaidi kuliko kikundi fulani cha wanasiasa.

Wito wangu leo ni kuwa kama Rostam analo la kusema na aliseme sasa asinyamazishwe tena wala kupigwa mkwara na chama chake. Kamas anaona hakutendewa haki yeye kama Raia basi anayo haki ya kujisafisha hadharani badala ya kulazimika kukaa kimya. Asije akafikiri kuwa ana mpango wa kuzungumza "huko mbeleni" lakini ikatokea kuwa yeye na utetezi wake wakanyamaza "milele" kama alivyonyamaza Bi. Amina Chifupa ambaye naye alitaka kupewa nafasi ya kujitetea lakini akazibwa mdomo. Natoa wito; kama Rostam unaamini una hoja SIMAMA JITETEE NA JIELEZE usikubali kufungwa na Ibara ya 15:1 ya Katiba ya CCM

Lakini swali kubwa ni Rostam ana nini ambacho kinampa nguvu ya kutia mwashawasha Bungeni? Je anatikisha kiberiti kuona kama kimejaa
 
Sakata la Richmond na mtikisiko wake bado havijaisha Bungeni. Kuna kila dalili kuwa yaliyotokea Bungeni mwezi wa pili na kusababisha kujiuzulu kwa Waziri Mkuu na kuvunjika kwa baraza la Mawaziri hayakuwa mwisho. Kuna kila dalili kuwa kuna baadhi ya watu ambao waliumizwa na hadi hivi sasa hawajakubali "yaishe"


2008-04-13T21_38_36-07_00.jpg
Miongoni mwa watu ambao kwa hakika waliumizwa hisia zao, hadhi na sifa zao ni Mbunge wa Igunga Mhe. Rostam Aziz (CCM) ambaye wakati wa matukio hayo alidai kuwa ripoti iliyosomwa na Mwenyekiti wa Kamati Teule ya Bunge Mhe. Harrison Mwakyembe (Kyela - CCM) haikuwa sahihi na akadai kama vile wengine kuwa hakutendewa haki.

Juhudi za kujisafisha kwa wahusika mbalimbali wa Richmond zimekuwa zikiendelea na kwa namna fulani jukumu kubwa zaidi linamuangukia Bw. Rostam ambaye aidha kwa kujitwisha mwenyewe au kukubali kutumika inaonekana amekuwa akitumia kila aina ya njia upande mmoja kujibu mashambulizi ya wapinzani kwa kutumia vyombo vyake vya habari na upande wa pili kutilia shaka utendaji mzima wa Kamati Teule na hivyo kujaribu kuhoji maamuzi yote yaliyotolewa Bungeni

Katika kikao kinachoendelea cha Bunge alitakiwa aje kutoa maelezo yake na kujibu hoja za Wabunge na kutoa utetezi wake. Mwishoni mwa juma alikuwa amejiandaa kutoa utetezi huo lakini kwa kile kinachodaiwa kuwa ni "unyeti" wa utetezi wake basi imeonekana si vyema kwa Bw. Rostam kujitetea Bungeni kwani italeta msukosuko mwingine nchini

Kama hilo ni kweli au ni mojawapo ya karata za CCM binafsi siamini kuwa Rostam anaweza kusema chochote kile ambacho kinaweza kutuyumbisha kama Taifa na ambacho hatuwezi kukihimili. Tumeweza "kuchafuka kwa hali ya kisiasa Zanzibar", tumeweza kuhimila msiba wa Sokoine, tumeweza kuhimili "mizengwe" ya Kizota na kifo cha Katibu Mkuu Kolimba na kwa hakika tumeweza kuhimila kujiuzulu kwa WAziri Mkuu

Naamini nchi yetu inaweza kuhimili msuko suko wowote ule wa kisiasa hata kama ni kujiuzulu kwa Rais aliyeko madarakani! Hata ikibidi Bunge zima kujiuzulu au kuvunjwa na kuitisha uchaguzi mwingine, TAifa letu lina uwezo wa kuhimili mambo hayo kwani Taifa ni kubwa zaidi kuliko kikundi fulani cha wanasiasa.

Wito wangu leo ni kuwa kama Rostam analo la kusema na aliseme sasa asinyamazishwe tena wala kupigwa mkwara na chama chake. Kamas anaona hakutendewa haki yeye kama Raia basi anayo haki ya kujisafisha hadharani badala ya kulazimika kukaa kimya. Asije akafikiri kuwa ana mpango wa kuzungumza "huko mbeleni" lakini ikatokea kuwa yeye na utetezi wake wakanyamaza "milele" kama alivyonyamaza Bi. Amina Chifupa ambaye naye alitaka kupewa nafasi ya kujitetea lakini akazibwa mdomo. Natoa wito; kama Rostam unaamini una hoja SIMAMA JITETEE NA JIELEZE usikubali kufungwa na Ibara ya 15:1 ya Katiba ya CCM

Lakini swali kubwa ni Rostam ana nini ambacho kinampa nguvu ya kutia mwashawasha Bungeni? Je anatikisha kiberiti kuona kama kimejaa

ningependa kudiffer, mshawasha huo hautokani na wabunge, bali na media inayoshawishi na kufanya watu waone vitu ndivyo sivyo !
 
ningependa kudiffer, mshawasha huo hautokani na wabunge, bali na media inayoshawishi na kufanya watu waone vitu ndivyo sivyo !

Heshima mbele mkuu,
Siku nyingine uwambie wakati mkiwa vikaoni wanakupa tabu sana kuwatetea, maana kabla hili halijaisha wanaibua lingine kiasi kwamba unakuwa ujui uanzie wapi kuwatetea. waeleze ukweli wapunguze japo kidogo.
 
Heshima mbele mkuu,
Siku nyingine uwambie wakati mkiwa vikaoni wanakupa tabu sana kuwatetea, maana kabla hili halijaisha wanaibua lingine kiasi kwamba unakuwa ujui uanzie wapi kuwatetea. waeleze ukweli wapunguze japo kidogo.

Mbona unampa kichwa namna hiyo? Hawa jamaa hata kama ni mafisadi lakini najua wana akili kidogo. Hawawezi kumtuma kada kuwatetea kada anajipendekeza tu. Si umemwaona mwingine ana lawyer USA.

Huyu kada asiyeweza hata kujenga hoja anaweza kutumwa na nani, nimejaribu kufikiria ... hata Makamba sidhani. Ila nachojua ni kwamba kada anatafuta kazi kwa hawa mafisadi ila bahati mbaya ndiyo hivyo tena hana quality wanazozitaka. Je we unafikiri ingekuwa mtu kama mwanakijiji au FM ( au mimi) kwa njisi wanavyoweza kujenga hoja, wangekuwa tayari kwenye payrol za hao mafisadi. Lakini wamechagua lililo jema

Ushauri wangu kwa kada, ongeza bidii kidogo ili at least makamba akuone
 
Natoa wito; kama Rostam unaamini una hoja SIMAMA JITETEE NA JIELEZE usikubali kufungwa na Ibara ya 15:1 ya Katiba ya CCM

Lakini swali kubwa ni Rostam ana nini ambacho kinampa nguvu ya kutia mwashawasha Bungeni? Je anatikisha kiberiti kuona kama kimejaa

Hawezi tena kujieleza. Ameshasema kuwa anakiheshimu chama (Ibara ya 51?) na pia analiheshimu Bunge.
 
Nidhamu ya cham imerudi.Mie nilijua kwanini Jk aliamua kumpa Pinda Kuwa WAziri Mkuu.Pinda amekuwa Senior officer wa TISS kwa muda wa miaka kumi achan an utumishi wake katika Taasisi hiyo.

Mie nina uhakika jambo lolote ambalo linaweza kuhatarisha usalama wa nchi basi halitapewa nafasi tena na wamekuwa makini hasa ya baada ya EL kujiuzuru na kusababisha khali ya Usalama Kuyumba.

Suala la RDC linawahusu watu wengi sana na kama RA akiamua kulisemea basi imani kwa wanachi juu ya serikali itapungua na JK hayuko tayari kwa hilo tena
 
Nidhamu ya cham imerudi.Mie nilijua kwanini Jk aliamua kumpa Pinda Kuwa WAziri Mkuu.Pinda amekuwa Senior officer wa TISS kwa muda wa miaka kumi achan an utumishi wake katika Taasisi hiyo.

Mie nina uhakika jambo lolote ambalo linaweza kuhatarisha usalama wa nchi basi halitapewa nafasi tena na wamekuwa makini hasa ya baada ya EL kujiuzuru na kusababisha khali ya Usalama Kuyumba.

Suala la RDC linawahusu watu wengi sana na kama RA akiamua kulisemea basi imani kwa wanachi juu ya serikali itapungua na JK hayuko tayari kwa hilo tena


usalama wa nchi uliyumba vipi wakati kitendo cha EL kujiuzulu ni kitendo cha Kikatiba? Hata Rais akijiuzulu kesho au kwa namna fulani akashindwa kuendelea na majukumu yake kwanini usalama wa nchi uwe mashakani?

Kuhusu EPA wametuambia hawawezi kuwakamata kwa sababu ya usalama wa nchi,

na sualala Rostam nalo ni la usalama wa nchi.

Kwanini wasituambie tu kuwa tuwaachie nchi yaishe... ?
 
wewe akinyamaza kinakuhusu nini? chama chetu kina nidhamu na nidhamu yake inamfunga mtu yoyote ambaye ni mwanachama hata kama ana kimbelembele namna gani. Endelea na mambo yako haya ya CCM tuachie wenyewe kwani wenyewe ni "sisi".

thanks!
 
wewe akinyamaza kinakuhusu nini? chama chetu kina nidhamu na nidhamu yake inamfunga mtu yoyote ambaye ni mwanachama hata kama ana kimbelembele namna gani. Endelea na mambo yako haya ya CCM tuachie wenyewe kwani wenyewe ni "sisi".

thanks!

Hivi swala la Richmond ni la CCM pekee au la nchi nzima, siamini kama limebakia la CCM pekee, na RA aliombwa na Bunge( la Jamhuri ya muungano wa Tanzania) na sio kamati kuu, hivyo kutoongea kwa RA ni mambo ya Taifa na sio CCM
 
Yawezekana katika utetezi wake RA akaweka ukweli ambao hata tume ya HM haikuuona,ikimaanisha kwamba kuna mafisadi ambao tume haikuwaona lakini RA katika utetezi wake akawataja......Hilo laweza kusababisha woga kwa wahusika na kama kawa wakasingizia issues za usalama kulikwepa
 
Nahisi utetezi wa RA ungehusisha sera na ilani ya uchaguzi wa CCM na RDC, EPA na uozo mwingine ule.

Anajiamini mno huyu tajiri ndiyo maana kila kukicha anaambiwa si raia lakini yeye kakaa kimya wala hajishughulishi kujitetea.

Richmond alimuuzia biashara Dowans, naye Dowans amemwajiri Caspian (kampuni ya RA).

Bunge linamgwaya, alkini pia naye RA ye anatikisa kiberiti kwani kama anona bunge halijamtendea haki SI AJE KWA WANANCHI AKAJITETEE?
 
Back
Top Bottom