Just Pray
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 2,142
- 4,779
Rais wa chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) Wakili Boniface Mwabukusi amesema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ameahidi kushughulikia mambo mbalimbali aliyoyawasilisha kwake alipozungumza nae Ikulu Dodoma.
Akijibu swali kuhusu majibu ya Rais Samia kama alizungumza na kuhusu kesi ya Tundu Lissu, Mwabukusi alisema kuwa jambo hilo aliliwasilisha na Rais Samia alimuahidi kulishughulikia katika namna ambayo hawataingilia taratibu za Mahakama.
"Na nilitoa taarifa kama tumezungumza na Rais alisema wanalishughulikia, ametusikiliza na aliniambia kuna wengine walifika mbele yake aliwasikiliza na watalifanyia kazi bila kuingilia utaratibu unaoendelea Mahakamani," alisema Mwabukusi
Aidha Wakili huyo aliendelea kusema kuwa, katika mazungumza hayo na Rais Samia hawakuzungumza tu suala la Lissu, bali yapo mambo mbalimbali waliyawasilisha kwake ikiwemo watu kupotea na Demokrasia na Utawala bora.
"Suala la Lissu ni moja ya mambo tuliyoyawakikisha kwa Rais, sio Lissu tu yapo mambo ya Demokrasia na utawala Bora, Sheria za uchaguzi na kanuni zake, suala la watu kupotea na suala la msomi Wakili Tundu Antipas Lissu," alisema Wakili Mwabukusi
Mwabukusi ameyasema hayo alipozungumza na waandishi wa Habari, alipofika Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Dar es Salaam kufuatilia kesi ya Uhaini inayomkabili Tundu Lissu.
Akijibu swali kuhusu majibu ya Rais Samia kama alizungumza na kuhusu kesi ya Tundu Lissu, Mwabukusi alisema kuwa jambo hilo aliliwasilisha na Rais Samia alimuahidi kulishughulikia katika namna ambayo hawataingilia taratibu za Mahakama.
"Na nilitoa taarifa kama tumezungumza na Rais alisema wanalishughulikia, ametusikiliza na aliniambia kuna wengine walifika mbele yake aliwasikiliza na watalifanyia kazi bila kuingilia utaratibu unaoendelea Mahakamani," alisema Mwabukusi
Aidha Wakili huyo aliendelea kusema kuwa, katika mazungumza hayo na Rais Samia hawakuzungumza tu suala la Lissu, bali yapo mambo mbalimbali waliyawasilisha kwake ikiwemo watu kupotea na Demokrasia na Utawala bora.
"Suala la Lissu ni moja ya mambo tuliyoyawakikisha kwa Rais, sio Lissu tu yapo mambo ya Demokrasia na utawala Bora, Sheria za uchaguzi na kanuni zake, suala la watu kupotea na suala la msomi Wakili Tundu Antipas Lissu," alisema Wakili Mwabukusi
Mwabukusi ameyasema hayo alipozungumza na waandishi wa Habari, alipofika Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Dar es Salaam kufuatilia kesi ya Uhaini inayomkabili Tundu Lissu.