Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
Kuna jamaa alikuwa kashakolea bangi yake ndani ya Mwezi huu wa Ramadhani. Akipita katika safari zake, akatokezea msikitini pana darsa baada ya sala ya Alasiri. Akamsikia Sheikh anasema, "Kila unaposema Subhanna Llah, basi unapandiwa bustani peponi". Jamaa kusikia hivyo, akauliza, "Sheikh sasa ukizisoma sana si itakuwa kwanza kichaka halafu itakuwa pori?" Jamaa wote msikitini wakawa hoi bin taaban unaambiwa hata mtoa darsa nae ilibidi aombe maji ya kunywa ,ila akakumbushwa kuwa ni mwezi wa funga, Ramadhan Kareem