Muziki wa Tanzania

Frumence M Kyauke

JF-Expert Member
Aug 30, 2021
630
1,245
Muziki wa Tanzania ni jina la kutaja muziki wenye asili ya Tanzania ya leo. Kama ilivyokuwa kwa binadamu wengine, wakazi wa eneo ambalo hatimaye limekuwa nchi ya Tanzania, walikuwa na utamaduni wao. Utamaduni huu ulikuwa ukitofautiana kati ya kabila na kabila. Moja ya vipengele ilikuwa muziki. Kiasili, hatukuwa na ‘muziki’ katika makabila yetu kabla ya ujio wa wageni, na hivyo hakuna kabila lenye tafsiri ya neno muziki.

Muziki wa Tanzania, Asili ya utamaduni ni Tanzania
Inapotendeka ni Dar es Salaam

Lakini tuliimba, tulicheza ngoma, tulipiga vyombo mbalimbali, ila tulikuwa na utamaduni mwingine kuhusu kitu hiki tunachokiita siku hizi muziki. Watafiti wanatuambia tulikuwa na ngoma, ambayo tafsiri yake ni kubwa kuliko muziki.

Ngoma ilikuwa ni chombo kile kilichotoa muziki, ngoma ilikuwa shughuli yenyewe, kwa mfano ngoma ya mavuno, ngoma ya mashetani na kadhalika, na pia tulicheza ngoma. Pamoja na kukosekana kwa maandiko yenye kina kuhusu hali ya ngoma katika kipindi hicho lakini tunajua watu waliimba na kucheza ngoma kwa matukio mbalimbali, hali ambayo inaendelea mpaka leo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom