4G LTE
JF-Expert Member
- Aug 4, 2015
- 6,777
- 10,533
Umetisha mkuu mmi Franco nina mix ina nyimbo zake zilizotikisa of 1hr+Mimi za Franco Pekee ninazo Kama 200 hivi
Sent from my SM-G970U1 using JamiiForums mobile app
Umetisha mkuu mmi Franco nina mix ina nyimbo zake zilizotikisa of 1hr+Mimi za Franco Pekee ninazo Kama 200 hivi
Hasahasa Ile ya candidate na bisso de mobutuUmetisha mkuu mmi Franco nina mix ina nyimbo zake zilizotikisa of 1hr+
Sent from my SM-G970U1 using JamiiForums mobile app
NaamDRC, batoto ba Congo.......Mobutu ama (Kuku mbengu wa Zabanga), ni kweli alichukia sana mambo ya kuiga umangaribi, lakini hapo hapo akawa anatamani sana maisha ya Kifaransa!...baada ya kuwaambia bana ba congo kuacha majina ya kikoloni kama vile Franco ama Rochereau...ambao wakati huo ndio walikua wakali wa muziki, Majina ya kabakia Luambo Luanzo Makiadi na Tabu Ley.
Mobutu kapiga kampeini kubwa sana ya kuondoa Ukoloni mambo leo , ndio mpaka sasa Congo Drc kuna Dini na kanisa la ki itikadi ya Kiafrika inayoitwa 'Kimbangiste'..... Makanisa yalibaki kufunza vijana kupiga muziki.....vile vile kwa vile walitawaliwa na Wafransa, kuna kitu kinaitwa ''Assimilation" yaani kuigiza aliekuteka mpaka ufanane nae...ilibidi watafute vyombo na machine za kurecodi za hali ya juu sana, ndipo unaona ngoma zao nyingi ni kali mpaka kesho...rekoding either Paris , belgium ama Us!
Halafu ni "Kimpa kisanga meni" ...ilicharazwa bass gitaa matata sana humo ndani acha hivyo vionjo vingine... Kilitoka 1983. Ukiwa na spika au earphones nzuri sikiza kwa makini Sec. 7 za mwanzoSwela ni mamaake?
Huu wimbo wa kusangameni ninao kwenye gari yangu, franco alikuwa anafika balaa
Kimpa kimsangameni nyimbo tamu mno ya mwaka 1976
Nipo mkuu majukumu tukweli kabisa mkuu, vipi ulipotelea wapi miezi kadhaa hukuonekana humu
Nipo mkuu majukumu tu
Safi sana mkuu...DRC, batoto ba Congo.......Mobutu ama (Kuku mbengu wa Zabanga), ni kweli alichukia sana mambo ya kuiga umangaribi, lakini hapo hapo akawa anatamani sana maisha ya Kifaransa!...baada ya kuwaambia bana ba congo kuacha majina ya kikoloni kama vile Franco ama Rochereau...ambao wakati huo ndio walikua wakali wa muziki, Majina ya kabakia Luambo Luanzo Makiadi na Tabu Ley.
Mobutu kapiga kampeini kubwa sana ya kuondoa Ukoloni mambo leo , ndio mpaka sasa Congo Drc kuna Dini na kanisa la ki itikadi ya Kiafrika inayoitwa 'Kimbangiste'..... Makanisa yalibaki kufunza vijana kupiga muziki.....vile vile kwa vile walitawaliwa na Wafransa, kuna kitu kinaitwa ''Assimilation" yaani kuigiza aliekuteka mpaka ufanane nae...ilibidi watafute vyombo na machine za kurecodi za hali ya juu sana, ndipo unaona ngoma zao nyingi ni kali mpaka kesho...rekoding either Paris , belgium ama Us!
Wakenya hawajui kabisa music mkuu...Swali zuri sana;
Utamaduni wa ndugu zetu wa kongo unaendana sana na Muziki pamoja na kucheza Muziki. Wakiwa wanalima watafanya hivyo iwapo kuna watumbuizaji wa muziki na hata kwenye mazishi huwa wana watumbuizaji wa muziki; na lolote wnalofanya kama jumuia lazima kuwe na muziki. Hii ni tofauti sana na kwetu huku ambako muziki ni burudani tu. Sasa wanamuziki wa Kongo waliamua kuchukua muziki wao kwa next level ili ujulikane ni muziki wa Kongo, na wakafanikiwa sana. Kwa hiyo muziki ni sehemu ya maisha yao na nyimbo nyingi unazojua za kikongo zina asiili muziki wa makabila yao. Tanzania na Uganda hatujawahi kuwa na muziki ambao ni brand ya Tanzania au ya Uganda, huwa tunakopi Kongo tu labda ukitoa ukitoa taarabu. Kenya walijaribu Benga kidogo lakini nadhani nao walifeli.
Ufafanuzi makini sana huu mkuu1. Walijua mapema kwamba muziki ni kazi na siyo starehe tu.
2. Walichanganya vionjo vya kongo na vile vyenye asili ya Cuba ambavyo zama hizo asili yake ilikuwa kongo basin
3. Walijenga mapema zaidi matumizi ya lugha yao kimuziki na kwa nguvu kubwa
4. Mabepari wa kigiriki walifungua "nyumba" za muziki na kuajiri session musicians kutoka DRC, Brazza, Angola etc na kujenga mashindano makali. Santuri zilitengenezwa na kuuzwa nje. Bendi zote kuu African Jazz, Rock A Mambo pamoja na OK Jazz etc zinahusika hapa.
5. Gitaa za umeme ziliingia mapema zaidi fuatilia midundo ya Orch. Watam na ilivyobadilika hadi OK Jazz miaka ya hamsini
6.Kuwa na wanamuziki wachache ambao walikuwa na ubunifu wa hali ya juu sana mmoja wapo akiwa Franco the Genius aliyejaribu kujiongeza kila idara, alihahakisha ngoma zake zinaendana na midundo ya kiafrica. African Jazz ilikuwa ya kisomi zaidi na OK Jazz ilikuwa ya mtaani. Kwa mfano OK Jazz na baadae TP OK Jazz ingawapo wengi wetu wanamjua Franco tu, lakini ilikuwa na nguzo kali kama Vicky Longomba (Baba yake Awilo) na huyu ndiye alikuwa sauti ya OK Jazz 1956-1971 na mtunzi mahiri (Co-president wa OK Jazz), Simaro Masiya Lutumba (1961-1993), Chef d'Orchestre, mpiga rythm mashuhuri, mtunzi bora wa OK Jazz na TP OK Jazz (The Poet),Vice President na President wa bendi baada ya Luambo kufariki na bila kumsahau Kiambukuta Londa Josky (1973-1993) mtungaji bora, muimbaji bora kabisa wa TP OK Jazz-kama Vicky alikua sauti ya OK Jazz basi Josky ndiye sauti ya TP OK Jazz (Comandant du Bord) alikuwa Vice President wa TP OK Jazz baada ya kufariki Luambo.
7. Nidhamu ya hali ya juu na mazoezi ya kufa mtu ili kutoa kitu kinachoeleweka.
8. Mobutu alisaidia lakini kikubwa zaidi ni wanamuziki wenyewe kujituma.
9. Bendi za DRC zilisafiri sana ndani na nje ya nchi na hivyo kueneza muziki wao
10.Baada ya wagiriki kuachana na muziki wazawa kama Verckys wa Maison Veve na Luambo waliingia sana kwenye biashara ya santuri na kufanya Kenya kwa Afrika mashariki kuwa kituo kikuu cha kutolea santuri zao (ASL) na hivyo kupatikana muziki wao wkwa urahisi zaidi.
11. Mpangilio wao wa mziki: mfano mzuri ni matumizi ya magitaa manne kwa wakati mmoja ambayo nafikiri ni Afican Jazz/Fiesta ndio walianza lakini Franco aliposhika hii kitu akaipaisha kwa namna ambayo haijatokea na kila gitaa likisikika kikamilifu na kwa kiwango bora zaidi na ndio maana haitarajiwi tena kutokea bendi kama TP OK Jazz.
12. Mwisho wa yote-hizo ni sababu zilizochangia wenzetu hao kuja na mirindimo bora ya kiafrica na kuisambaza kwa hamasa kubwa na kukubalika na waafrica wengi.
Rhumba huwa Ni nzuri mnoo
Asante sana kaka mkubwadvj nasmiletz- RHUMBA CONGOLESE VOL 1
Listen to dvj nasmiletz- RHUMBA CONGOLESE VOL 1 by Dvj Nasmiletz on hearthis.at | Otherhearthis.at
Thanks bossdvj nasmiletz- RHUMBA CONGOLESE VOL 1
Listen to dvj nasmiletz- RHUMBA CONGOLESE VOL 1 by Dvj Nasmiletz on hearthis.at | Otherhearthis.at
Good brotherdvj nasmiletz- RHUMBA CONGOLESE VOL 1
Listen to dvj nasmiletz- RHUMBA CONGOLESE VOL 1 by Dvj Nasmiletz on hearthis.at | Otherhearthis.at
Thanxs..karibuGood brother
Kaka upo?Thanxs..karibu
Soja vipi? Usharudi mtaani?Kaka upo?
Yes mkuu. Sasa nipo JF ninasikilizia shindano la stories of change. Sijui nitaambulia chochote kitu au nitakosa kabisa.Soja vipi? Usharudi mtaani?