jogi
JF-Expert Member
- Sep 25, 2010
- 25,558
- 25,323
wanajamvi, leo jioni nimeshuhudia mbunge wa iramba magharibi ambaye pia ni muweka hazina wa ccm, Mwigulu madelu nchemba, akikimbia hoja za wapiga kura wake, awali akihutubia wananchi kata ya kyengege alilalamikia suala la vijana kujiunga na chadema kana kwamba haijawafanyia chochote kwacho waiunge mkono, akitumia misamiati ya kinyiramba yenye kejeli aliwaambi alikuwa tayari kuwapatia ngombe wachinje wale ili warudi ccm, kwa jinsi alivyokuwa akilalamika na yeye mwenyewe kukiri kuwa jitihada zake zimegonga mwamba. aidha Mwigulu alitumia muda mwingi kuhutubia badala ya kutoa nafasi iliyosubiriwa kwa hamu kubwa ya maswali kwa muwakilishi huyo, ni kijana mmoja tu aliyelazimisha na kupata nafasi kumtwanga swali lililohusu uwakilishi mbovu bungeni, akijibu swali hilo alidai ni kutokana na tabia ya wapinzani bungeni kupinga kila kitu hivyo akalazimika naye kupinga. kigongo cha swala la katiba mpya na posho akasema muda umekwisha kwani saa 6.00 jioni ilishawadia, wananchi hawakufurahishwa na hilo, wamesikika wakisema