Muuundo wa serikali tanzania katika katiba mpya

Muuundo wa serikali tanzania katika katiba mpya

Not man

New Member
Joined
Jul 8, 2013
Posts
2
Reaction score
0
Napendekeza serikali moja katika tatu kama ifuatvyo:
Rais wa jamuhuri ya muungano awe na makamu wawili ambao ni Rais wa zanzibar na makamu wa kwanza wa Rais wa jamuhuri ya muungano, Rais wa Tanganyika na makamu wa pili wa Rais wa jamuhuri ya muungano, Rais wa Zanzibar na makamu wa kwanza wa Rais aendelee kuchaguliwa kama ilivyo sasa. Lakini Rais wa Tanganyika na makamu wa pili wa Rais wa jamuhuri ya muungano atapatikana kama ifuatavyo:-
Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania ateuwe majina mawili toka vyama viwili vitakavyokua vimepata ushindi wa kwanza na wa pili katika uchaguzi mkuu, majina hayo yapelekwe bungeni ili kupigiwa kura ya siri na wabunge wa Tanganyika (Tanzania bara), Mshindi ndiye atakae kua Rais wa Tanganyika na makamu wa pili wa Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania. Rais wa tanganyika ndiye atakua mtendaji mkuu wa serikali ya Tanganyika na atashirikiana na Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania kuunda Baraza la mawaziri 15 wa Tanganyika hivyo kwa nafasi yake cheo cha waziri mkuu kifutwe, Rais wa Jamuuri wa Muungano atateuwa mawaziri watatu toka pande yeyote ya Muungano, kwa wizara zinazoshughurikia muungano ambazo ni wizara ya mambo ya ndani, wizara ya ulinzi na wizara ya mambo ya nje.
Kwa hoja hii gharama za uchaguzi zitakua zimepungua na TANGANYIKA yetu itakua Hai TENA.
 
Rais + Rais + Rais + Rais = ?

Mtazamo wangu:

Mimi napendekeza serikali tatu, yenye muundo wa Rais mmoja tu wa Jamuhuri,

Serikali ya Tanganyika iongozwe na Waziri Mkuu wa Tanganyika,

Na serikali ya Zanzibar iongozwe na Waziri Kiongozi wa Zanzibar!
 
Mimi nimejiundia baraza langu la katiba la mtu mmoja na ninatarajia kupeleka mapendekezo yangu muda mfupi ujao pia nitayaweka hapa jamvini wakati muafaka!
 
Serikali tatu, Marais wawili, Rais mmoja wao atakuwa wa Tanzania kila miaka kumi na mwenzake Makamu wa Rais.
 
mmeishaambiwa serikali 3 zitavunja muungano hamsikii

najua hii statement itanicost, loh!
 
Nasikia mbavu za muungano zinakatika taratiiibu!
 
Rais + Rais + Rais + Rais = ?

Mtazamo wangu:

Mimi napendekeza serikali tatu, yenye muundo wa Rais mmoja tu wa Jamuhuri,

Serikali ya Tanganyika iongozwe na Waziri Mkuu wa Tanganyika,

Na serikali ya Zanzibar iongozwe na Waziri Kiongozi wa Zanzibar!

Mna uhakika mtaipata hiyo tanganyika yenu?sahau zanzbr kuongozwa na waziri kiongozi bali itaongozwa na rais wa jamhuri ya watu wa zanzbr na ataiongoza zanzbr yenye mamlaka yake nnje na ndani ya nchi.
 
Mna uhakika mtaipata hiyo tanganyika yenu?sahau zanzbr kuongozwa na waziri kiongozi bali itaongozwa na rais wa jamhuri ya watu wa zanzbr na ataiongoza zanzbr yenye mamlaka yake nnje na ndani ya nchi.

Ikiwa Zanzibar itapata mamlaka yake ya ndani na nje, hiyo moja kwa moja Tanganyika yetu itafufuka
 
ninachotaka kukijua ni kama Tanganyika ( our motherland ) itarudi ? Baasi , hayo mengine ntafanya kuyavumilia tu .
 
Rudieni kunisimulia mada jamani, nna kiroba cha sita sasa, hapa nilipo hoi!!
 
tuwe na serikali kumi! serikali kuu na serikali nyingine tisa za majimbo. Majimbo manane ya bara na moja la zanzibar. Majimbo yawe na serikali zao na mamlaka kamili isipokuwa fedha, mambo ya nje, mambo ya ndani na ulinzi. Hii itasaidia sana kuondoa uwezekano wa kuvunjika muungano, itaharakisha maendeleo kwa kuleta ushindani miongoni mwa majimbo. Jimbo/nchi ya zanzibar itaendelea kuongozwa na rais ambaye atakuwa ni makamu wa rais na mwenyekiti wa baraza la Magavana. Majimbo mengine yataongozwa na magavana. Mpango huu utaondoa malalamiko kwa upande wa bara kuhusu zanzibar pia hofu ya wazanzibar kumezwa au kutumika kwenye mambo ya Tanganyika itaisha. majimbo yanaweza hata kuongezeka kama ilivyo Kenya wenye majimbo 47!
 
Rais + Rais + Rais + Rais = ?

Mtazamo wangu:

Mimi napendekeza serikali tatu, yenye muundo wa Rais mmoja tu wa Jamuhuri,

Serikali ya Tanganyika iongozwe na Waziri Mkuu wa Tanganyika,

Na serikali ya Zanzibar iongozwe na Waziri Kiongozi wa Zanzibar!

Ndugu Miamia, Tupo Pamoja, Raisi Mmoja Mwawaziri wakuu Wawili, Tena wakuchaguliwa Bungeni kwa Kura za wabunge ikiwezekana kupunguza Gfharama za UchaguZi. Ila ili la kupigiwa kura na wabunge Lina madhara yake maana kwahili ilivyo bongo sasa kuna uwezekano wa Mtu kununua Bunge/wabunge lote.
 
tuwe na serikali kumi! serikali kuu na serikali nyingine tisa za majimbo. Majimbo manane ya bara na moja la zanzibar. Majimbo yawe na serikali zao na mamlaka kamili isipokuwa fedha, mambo ya nje, mambo ya ndani na ulinzi. Hii itasaidia sana kuondoa uwezekano wa kuvunjika muungano, itaharakisha maendeleo kwa kuleta ushindani miongoni mwa majimbo. Jimbo/nchi ya zanzibar itaendelea kuongozwa na rais ambaye atakuwa ni makamu wa rais na mwenyekiti wa baraza la Magavana. Majimbo mengine yataongozwa na magavana. Mpango huu utaondoa malalamiko kwa upande wa bara kuhusu zanzibar pia hofu ya wazanzibar kumezwa au kutumika kwenye mambo ya Tanganyika itaisha. majimbo yanaweza hata kuongezeka kama ilivyo Kenya wenye majimbo 47!

Duh! Kwanini Unaogopa znz kuwa na Mjimbo Mwawili Pemba na Unguja ?

Ila hilo la kenya ni noma, yaji kuna serekali za Majibo 47 ?
 
Nasikia mbavu za muungano zinakatika taratiiibu!

Hiki ndicho wengi wasichokifahamu au wasichotaka kukikubali. Watu wanajadili muundo wa muungano wakati kila dalili zinaonyuesha kuwa wananchi wengu hawautaki muungano

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Mimi nimejiundia baraza langu la katiba la mtu mmoja na ninatarajia kupeleka mapendekezo yangu muda mfupi ujao pia nitayaweka hapa jamvini wakati muafaka!

Ndugu si bora ungeunda la Familia au Mtaani tu ?

Hivi kweli tumeshinda kuunda la kwetu la wanaJF ?
 
Ndugu Miamia, Tupo Pamoja, Raisi Mmoja Mwawaziri wakuu Wawili, Tena wakuchaguliwa Bungeni kwa Kura za wabunge ikiwezekana kupunguza Gfharama za UchaguZi. Ila ili la kupigiwa kura na wabunge Lina madhara yake maana kwahili ilivyo bongo sasa kuna uwezekano wa Mtu kununua Bunge/wabunge lote.
Rais Mmoja tu na Makamu wake anatosha kule Visiwani Aongoze Gavana mmoja na Tz Bara Aongoze Gavana mmoja tu Kama ilivyo huko USA au waige muungano wa UK Yaani ZNZ atawale Waziri Mkuu na Bara atawale Waziri Mkuu Rais awe mmoja tu na ahamie Dodoma asikae Dsm angalau italeta unafuu wa gharama za kuendesha serikari
 
ili Muungano udumu na kuwaepusha wazenji Kuwa Raia wa Nchi Jilan na kulipia Viza na vibali kuishi Tz inapaswa Muungano uendane na wakati (digital ) kwani Nyerere aliasisi muungano akitegemea muungano utakuwa ukijiboresha wenyewe kulingana na wakati .!lakini imekuwa kinyume na matarajio Muungano umeng'ang'ania staili ile ile ya 1964 matokeo yake wizara ya muungano inapewa Bajeti kubwa lakini bado imeshindwa kuziondoa kero za muungano
 
napendekeza kuwepo na jimbo la Tanganyika litakalokuwa na mikoa ya Tabora, kigoma, Rukwa na Katavi. Jimbo la Dar es salaam litakalokuwa na mkoa wa Dar es salaam na wilaya ya Bagamoyao na Kibaha, Jimbo Kilimanjaro litakalokuwa na mikoa ya Tanga, kilimanjaro, Arusha na Manyara. Jimbo la Zanzibar litakalokuwa na nchi ya Zanzibar. Jimbo la Victoria Nyaza litakalokuwa na mikoa ya Mwanza, Kagera, Mara na shinyanga. Jimbo la kati litakuwa na mikoa ya Simiyu na Singida, na Dodoma. Jimbo Nyanda za juu litakuwa na mikoa ya Morogoro, Iringa,Njombe na Mbeya. Jimbo la kusini litakuwa na mikoa ya Ruvuma, Lindi na Mtwara
 
ili Muungano udumu na kuwaepusha wazenji Kuwa Raia wa Nchi Jilan na kulipia Viza na vibali kuishi Tz inapaswa Muungano uendane na wakati (digital ) kwani Nyerere aliasisi muungano akitegemea muungano utakuwa ukijiboresha wenyewe kulingana na wakati .!lakini imekuwa kinyume na matarajio Muungano umeng'ang'ania staili ile ile ya 1964 matokeo yake wizara ya muungano inapewa Bajeti kubwa lakini bado imeshindwa kuziondoa kero za muungano hadi Leo ! Mawazo ya kuludisha Ukoloni wa Mwarabu Zenji ni moja ya tatizo sugu Pia wazenji kutojitambua Kuwa Tz Bara inawabeba sana nalo ni Tatizo kubwa Siku ikitokea Wazenji wakajitambua vizuri na kuomba Kuwa na Serikari moja tu hakika kero za muungano zitabakia Kuwa historia
 
Back
Top Bottom