Rugas
JF-Expert Member
- Jan 8, 2009
- 1,048
- 197
Hiyo ni serikali moja mkuu..tuwe na serikali kumi! serikali kuu na serikali nyingine tisa za majimbo. Majimbo manane ya bara na moja la zanzibar. Majimbo yawe na serikali zao na mamlaka kamili isipokuwa fedha, mambo ya nje, mambo ya ndani na ulinzi. Hii itasaidia sana kuondoa uwezekano wa kuvunjika muungano, itaharakisha maendeleo kwa kuleta ushindani miongoni mwa majimbo. Jimbo/nchi ya zanzibar itaendelea kuongozwa na rais ambaye atakuwa ni makamu wa rais na mwenyekiti wa baraza la Magavana. Majimbo mengine yataongozwa na magavana. Mpango huu utaondoa malalamiko kwa upande wa bara kuhusu zanzibar pia hofu ya wazanzibar kumezwa au kutumika kwenye mambo ya Tanganyika itaisha. majimbo yanaweza hata kuongezeka kama ilivyo Kenya wenye majimbo 47!
Au ndo unataka tuhesabu mpaka serkali za mitaa!