GHIBUU
JF-Expert Member
- Jan 13, 2011
- 4,432
- 3,006
Chanzo chake : Mzalendo.net
Dr.Harith Ghassany,
Suala la kujiuliza "tunautaka Muungano wa aina gani"? Muhimu ni kukubaliana juu ya aina ya Muungano tunaoutaka Wazanzibari. Lakini kabla ya hilo ni lazima kwanza tukubaliane kuzaliwa kwa Tanganyika kwa sababu kama Tanganyika haikuzaliwa tutakuwa na Muungano na nani?
Wala si muhimu kwa hivi sasa kujiuliza na kujibu vipi Tanganyika itazaliwa tena. Tukubaliane juu ya mtizamo kuwa Tanganyika izaliwe na ikae tena na Zanzibar kama ni mshirika alie sawa sawa na Tanganyika, na kuamua juu ya mfumo wa Muungano baada ya kukubaliana kuwepo kwa nchi ya Zanzibar na ya Tanganyika zenye sifa zake kamili za Kitaifa na za Kimataifa.
Tuweze kufika hapo kwanza na tutakapofika hapo tutaweza kuzungumza kwa pamoja juu ya aina za taasisi za Muungano wa nchi mbili zilizo sawa, na aina ya executive organ kama itakuwa ni Supreme Council of Heads of Government, i.e. Presidents of Zanzibar, Tanganyika, Kenya….
Kisichotakiwa na cha kuvunjwa ni "general approach" ilionayo Tanzania Bara juu ya Muungano uliopo ambayo ni "approach" iliozoweleka yenye kutumia "force" "domination", kibri na dharau juu ya Zanzibar na Wazanzibari. Approach ndio kitu asasi na muhimu. Ile approach ya miaka 47 ya Tanganyika na baadae Tanzania kutumia ubabe, ni lazima ivunjike na badala yake uje mtazamo mpya wa Muungano unaotokana na ridhaa (consent) ya Wazanzibari.
Wazanzibari wanafahamu fika kuwa Muungano wa mabavu hautakiwi na umeshavunjika na unafaa uvunjwe. Lakini huu wa ridhaa pia hatutoupata bila ya kwanza kuzaliwa Tanganyika. Hili ndilo la msingi. Tuwe na jazba dhidi ya Muungano wa mabavu na wenye kuidhalilisha Zanzibar.
Lakini baada ya jazba ya halali yenye kuukataa Muungano wa kimabavu, tukubaliane juu ya "general approach" ya kuzaliwa kwa Tanganyika kwanza na baadae tujadili mfumo wa Muungao wa ridhaa. Tukiikamata njia hii basi tutajua wapi tunataka Zanzibar na Tanganyika zielekee na katika mfumo wa aina gani.
Nchi za Ulaya si zile pale zimo katika European Union? Ndio zimechukuwa muda mrefu kufika zilipofika lakini zisingeliweza kufika hapo zilipofika kama wangelikuwa hawana "the right approach" na kutizamana kwa spirit ya usawa baina yao. Si wana Ufaransa, Ujerumani, nk, lakini si kila nchi ina chake na wana mashirikiano ya kiuchumi na kuyatatua matatizo ya pamoja? Lakini hakuna ujanja, wala dharau, wala majungu!
La kama tunataka kuanza kwa kusema tuuvunje Muungano bila ya kwanza kudai Tanganyika izaliwe na kudai Muungano wa ridhaa wenye mfumo wa nchi mbili zilizo huru na zenye sifa za Kitaifa na za Kimatifa, wa basi tutaonekena ni vichwa maji na si watu wa maana.
Tutaonekana Wazanzibari ni watu wenye kujuwa tusichokitaka lakini hatukijui tunachokitaka!
Dr.Harith Ghassany,
Suala la kujiuliza "tunautaka Muungano wa aina gani"? Muhimu ni kukubaliana juu ya aina ya Muungano tunaoutaka Wazanzibari. Lakini kabla ya hilo ni lazima kwanza tukubaliane kuzaliwa kwa Tanganyika kwa sababu kama Tanganyika haikuzaliwa tutakuwa na Muungano na nani?
Wala si muhimu kwa hivi sasa kujiuliza na kujibu vipi Tanganyika itazaliwa tena. Tukubaliane juu ya mtizamo kuwa Tanganyika izaliwe na ikae tena na Zanzibar kama ni mshirika alie sawa sawa na Tanganyika, na kuamua juu ya mfumo wa Muungano baada ya kukubaliana kuwepo kwa nchi ya Zanzibar na ya Tanganyika zenye sifa zake kamili za Kitaifa na za Kimataifa.
Tuweze kufika hapo kwanza na tutakapofika hapo tutaweza kuzungumza kwa pamoja juu ya aina za taasisi za Muungano wa nchi mbili zilizo sawa, na aina ya executive organ kama itakuwa ni Supreme Council of Heads of Government, i.e. Presidents of Zanzibar, Tanganyika, Kenya….
Kisichotakiwa na cha kuvunjwa ni "general approach" ilionayo Tanzania Bara juu ya Muungano uliopo ambayo ni "approach" iliozoweleka yenye kutumia "force" "domination", kibri na dharau juu ya Zanzibar na Wazanzibari. Approach ndio kitu asasi na muhimu. Ile approach ya miaka 47 ya Tanganyika na baadae Tanzania kutumia ubabe, ni lazima ivunjike na badala yake uje mtazamo mpya wa Muungano unaotokana na ridhaa (consent) ya Wazanzibari.
Wazanzibari wanafahamu fika kuwa Muungano wa mabavu hautakiwi na umeshavunjika na unafaa uvunjwe. Lakini huu wa ridhaa pia hatutoupata bila ya kwanza kuzaliwa Tanganyika. Hili ndilo la msingi. Tuwe na jazba dhidi ya Muungano wa mabavu na wenye kuidhalilisha Zanzibar.
Lakini baada ya jazba ya halali yenye kuukataa Muungano wa kimabavu, tukubaliane juu ya "general approach" ya kuzaliwa kwa Tanganyika kwanza na baadae tujadili mfumo wa Muungao wa ridhaa. Tukiikamata njia hii basi tutajua wapi tunataka Zanzibar na Tanganyika zielekee na katika mfumo wa aina gani.
Nchi za Ulaya si zile pale zimo katika European Union? Ndio zimechukuwa muda mrefu kufika zilipofika lakini zisingeliweza kufika hapo zilipofika kama wangelikuwa hawana "the right approach" na kutizamana kwa spirit ya usawa baina yao. Si wana Ufaransa, Ujerumani, nk, lakini si kila nchi ina chake na wana mashirikiano ya kiuchumi na kuyatatua matatizo ya pamoja? Lakini hakuna ujanja, wala dharau, wala majungu!
La kama tunataka kuanza kwa kusema tuuvunje Muungano bila ya kwanza kudai Tanganyika izaliwe na kudai Muungano wa ridhaa wenye mfumo wa nchi mbili zilizo huru na zenye sifa za Kitaifa na za Kimatifa, wa basi tutaonekena ni vichwa maji na si watu wa maana.
Tutaonekana Wazanzibari ni watu wenye kujuwa tusichokitaka lakini hatukijui tunachokitaka!