muumini na padri

1000 words

Senior Member
Joined
Dec 29, 2012
Posts
169
Reaction score
32
Padri amekaa katika ki-box cha kuungamisha,
kanisani hakuna mtu. Mara muumini mmoja
akaingia,
akapiga magoti upande wa pili na kufanya ishara
ya
msalaba akaanza kuungama.
== "Padri naungama dhambi zangu, leo
nimefanya
dhambi kubwa sana"
"Endelea...."
...
...
== "Bosi wangu aliniita nyumbani kwake
akaniambia amegundua nimeiba shilingi milioni
50,
akasema nisipotoa maelezo ya kutosha
atanipeleka
polisi.
Sasa ukweli mimi naogopa kufungwa na pesa
kweli
niliiba, nikatazama huku na huku nikagundua
tuko wawili peke yetu, nikachomoa bastola
nikamuua.
Nitasamehewa?"
"Utasamehewa...!! " == "Basi wakati nataka
kuondoka nikasikia mlango
unafunguliwa, kutazama loh, mke wa bosi...!!
Akaniuliza nimemfanya nini mume wake.
Kutazama huku na huku nikagundua tuko wawili
peke yetu, nikamuua na yeye. Nitasamehewa na
hiyo?" "Utasamehewa... "
== "Nikatoka nje, nikawasha gari niondoke
lakinimlinzi akakataa kufungua geti akasema
amesikia kama kishindo hivi! Nikaona ananiwekea
kiwingu. Kutazama huku na huku nikagundua
tuko
wawili peke yetu nikamuua. Nitasamehewa?"
"Mmm!! Utasamehewa... ."
== "Nikajifungulia geti mwenyewe nikaenda
nyumbani, wakati napanga kuja kuungama mtoto
wa bosi akabisha hodi nikawaza mambo gani
tena.
Akasema amerudi nyumbani na kukuta
yalotokea,
lakini akanionyesha diary ya baba yake
inayoonesha
kuwa nilikuwa na appointment naye kabla hajafa.
Nikamuuliza nani mwingine anajua, akasema
ameanzia kwangu kisha atakwenda polisi.
Nikatazama huku na huku nikagundua tuko wawili
peke yetu nikamuua. Diary nikaichomamoto.
Nitasamehewa na hilo?"
Kimya........ "Padri, Nitasamehewa kwa hilo?"
Kimya.........
Jamaa kutazama kwenye kibox padri hayupo.
Lakini kwenye kona moja akaona kabati la ngou
za
mapadri kama linatikisika.
Kufungua akamuona Padri kajificha katikati ya
majoho anatetemeka.... .
"Sasa baba mbona umenikimbia?"
Padri kwa taabu akajibu...
"Nilitazama huku na huku nikagundua kuwa tuko
wawili peke yetu........"
 
sijawahi kucheka hata kutabasamu tangu nizaliwe miaka 43 iliyopita lakini leo nimetabasamu kidogo!
 
Hii siyo tamu sana

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Hahaha nimeipenda kali sana

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…