Musoma: Tujikumbushe 1980 - 1990

Musoma: Tujikumbushe 1980 - 1990

metatron

JF-Expert Member
Joined
Sep 26, 2016
Posts
552
Reaction score
275
Kwanza kabisa wasalamu wanajumia hapa Jukwaani, baada ya kamaliza mfungo na Kisha sikuu ya Eid tunarejea kama kawaida.

Kwa vijana wa sasa ambao tumezaliwa Mkoani Mara katika wilaya ya Musoma Miaka ya 1980,1990. Kuna baadhi ya radha tulizipata kupitia mkoa wetu pendwa pamoja na matukio mengine ya kusitikitisha na kufurahisha kipindi hicho. Kwa kweli huwa nikikumbuka mpangangilio wa zile shule za msingi pale Musoma mjini huwa napata stajabu na kuwapa hongera waliofanya ubunifu ule.

1. Shule ya msingi Azimio
2. Shule ya msingi Mwembeni
3. Shule ya msingi Iringo
4. Shule ya msingi Mkendo.

Ukirudi katika viunga vya mji kwa wakati huo tuko wadogo Mida ya Jioni mitaa ya Iringo hapa kuna soko jioni unaenda kujipatia kichwa cha samaki sangara kwa Jina maarufu "Spika" Hahaha kwa kweli ilikuwa raha sana.

Kwa upande wa majina maarufu kipindi hicho MAMAS HOTEL, TAJIRI PANJU, SHARIFU (Sasa marehemu), KAKINDA, SULTAN (hapa walikuwa wanauza koni), JUMBA LA SINEMA, MILANGO MMOJA, KITAJI, CHAMBIRI, MSETI, MUSOMA BUS (na mengineyo utaweka unalokumbuka)

Sehemu za kutisha kipindi hicho ilikuwa ni makoko huko tuliambiwa kuna mtego wa Nyuki na huko ndio mafagio yalikuwa yanatoka. Habari mbaya nayokumbuka ilikuwa ni ajali ya Boti kuzama na iliua karibia watu wote waliokuwa wanaenda kuchukua Dagaa vizingani kama sikosei ilikuwa 1992 au 1993 maiti zikaletwa pale Mwigobole Mji mzima ulikuwa ni vilio tupu.

KAMA KUNA KITU UNAKUMBUKA UNAWEZA KUWEKA HAPA TUJIKUMBUSHE NA MUSOMA YETU.
 
Mimi Binafsi niliishi Kenedy Street na Shule nilisoma Mwembeni Shule ya msingi.
 
Mbona sijaona tajiri Nyakiteri hapo??
Nimemsikia sana huyu pia ana jengo la Ghorofa pake kitaji
 
farai coach
mikate ya united
watoto kuvuka barabara ya ndege/runway kwa miguu. shotcut ya watu wanaotokea mwisenge kuja kwenye hizo shule

matengere
mazara
nakumbuka siku tunamuaga mwinyi pale uwanjani
umitashumta
mitihani ya ujirani mwema mnabeba madawati kwenda shule jirani.
maloko.
sangara kule aliitwa chengu.
matani.
mcc.
mchakamchaka.
siku ikija ile ndege kubwa ya jeshi au airtanzania mnawahi kushangaa. au ile foka au ndege ya buyoya alipokuwa anakuja kupata darasa kwa nyerere.
beach...
litungu wakura wakitahiriwa.

mitunge
 
Aisee katika wote uliowataja wa enzi hizo umemsahau yule Bubu Kaswamila! na enzi hizo tukienda kucheza michezo mbali mbali pale "Diocese" siku hizi ni mwembeni sec. Na kule kwenye jumba la sinema kwa wakina Meb! Musoma ya enzi hizo raha sana!
 
[QLweye, post: 21892139, member: 22915"]Aisee katika wote uliowataja wa enzi hizo umemsahau yule Bubu Kaswamila! na enzi hizo tukienda kucheza michezo mbali mbali pale "Diocese" siku hizi ni mwembeni sec. Na kule kwenye jumba la sinema kwa wakina Meb! Musoma ya enzi hizo raha sana![/QUOTE]

Unamkumbuka Sang'e wa Mjini. Wachezaji mpira kina Chamwenyewe, Idd wa Mara Spurs. Bend ya Mara Jazz na mtindo wao wa Sensera na mengineyo mengi
 
Mbona sijaona tajiri Nyakiteri hapo??
Nimemsikia sana huyu pia ana jengo la Ghorofa pake kitaji
Eeeeh mkuu ni Kweli ghorofa lina muda mrefu Sana pale Kitaji, Mama Nyakiteri heshima kwake
 
farai coach
mikate ya united
watoto kuvuka barabara ya ndege/runway kwa miguu. shotcut ya watu wanaotokea mwisenge kuja kwenye hizo shule

matengere
mazara
nakumbuka siku tunamuaga mwinyi pale uwanjani
umitashumta
mitihani ya ujirani mwema mnabeba madawati kwenda shule jirani.
maloko.
sangara kule aliitwa chengu.
matani.
mcc.
mchakamchaka.
siku ikija ile ndege kubwa ya jeshi au airtanzania mnawahi kushangaa. au ile foka au ndege ya buyoya alipokuwa anakuja kupata darasa kwa nyerere.
beach...
litungu wakura wakitahiriwa.

mitunge
Kweli kabisa mkuu dah umenikumbusha mbali Sana hakika wewe ni Musoma Legendary.
 
Aisee katika wote uliowataja wa enzi hizo umemsahau yule Bubu Kaswamila! na enzi hizo tukienda kucheza michezo mbali mbali pale "Diocese" siku hizi ni mwembeni sec. Na kule kwenye jumba la sinema kwa wakina Meb! Musoma ya enzi hizo raha sana!
Hahaha kweli kabisa Kaswamila nadhani nae kwa Sasa ni marehem ila Musoma ya zamani Raha Sana mkuu.
 
[QLweye, post: 21892139, member: 22915"]Aisee katika wote uliowataja wa enzi hizo umemsahau yule Bubu Kaswamila! na enzi hizo tukienda kucheza michezo mbali mbali pale "Diocese" siku hizi ni mwembeni sec. Na kule kwenye jumba la sinema kwa wakina Meb! Musoma ya enzi hizo raha sana!

Unamkumbuka Sang'e wa Mjini. Wachezaji mpira kina Chamwenyewe, Idd wa Mara Spurs. Bend ya Mara Jazz na mtindo wao wa Sensera na mengineyo mengi[/QUOTE]
Mkuu nakumbuka pia mtaa WA mkendo Kati pale kulikuwa na wachezaji mpira wakina CHUMILA nadhani walicheza Simba na Yanga ya enzi hizo.
 
[QLweye, post: 21892139, member: 22915"]Aisee katika wote uliowataja wa enzi hizo umemsahau yule Bubu Kaswamila! na enzi hizo tukienda kucheza michezo mbali mbali pale "Diocese" siku hizi ni mwembeni sec. Na kule kwenye jumba la sinema kwa wakina Meb! Musoma ya enzi hizo raha sana!

Unamkumbuka Sang'e wa Mjini. Wachezaji mpira kina Chamwenyewe, Idd wa Mara Spurs. Bend ya Mara Jazz na mtindo wao wa Sensera na mengineyo mengi[/QUOTE]
Mkuu nakumbuka pia mtaa WA mkendo Kati pale kulikuwa na wachezaji mpira wakina CHUMILA nadhani walicheza Simba na Yanga ya enzi hizo.
 
Well, memory zangu ni za late 90s. Nimesoma mwisenge primary na baadae kuhamia mtakuja primary kwa sababu ili kufika mwisenge kirahisi ilikua lazima tuvuke mto. Sasa kipindi cha mvua kubwa ilikua risky sana.

Nakumbuka tulikua tunaenda kutafuta mifagio kule milimani nyamiongo, kiwandani bukanga mpaka kwenye kambi ya jeshi sometimes.

Wakati nasoma mwisenge nlikua napenda sana lile suala la kwenda ulinzi jioni maana tulikua tunacheza mpira na mwishoni kwenda kuogelea ziwani pale karibu na bwalo la polisi

Pia usafiri wa daladala ulianza kwa gari mbili tu moja inaitwa lake side na nyingine sarafina kutoka mjini kwenda makoko

Matajiri niliokua nawafahamu kipindi kile ni Hafidh, Panju, Ndomi.. Wengine siwakumbuki vizuri.
Hapo kwa Hafidh ilikua geti kali sana lakini tuliingia ndani mpk sebleni kipindi Mwl JK Nyerere ameaga dunia.. Tukaenda kuangalia matangazo ya live.

Daaah i wish i could share more.. Nimetoka huko mwaka 2002 nikiwa darasa la 6.
 
Well, memory zangu ni za late 90s. Nimesoma mwisenge primary na baadae kuhamia mtakuja primary kwa sababu ili kufika mwisenge kirahisi ilikua lazima tuvuke mto. Sasa kipindi cha mvua kubwa ilikua risky sana.

Nakumbuka tulikua tunaenda kutafuta mifagio kule milimani nyamiongo, kiwandani bukanga mpaka kwenye kambi ya jeshi sometimes.

Wakati nasoma mwisenge nlikua napenda sana lile suala la kwenda ulinzi jioni maana tulikua tunacheza mpira na mwishoni kwenda kuogelea ziwani pale karibu na bwalo la polisi

Pia usafiri wa daladala ulianza kwa gari mbili tu moja inaitwa lake side na nyingine sarafina kutoka mjini kwenda makoko

Matajiri niliokua nawafahamu kipindi kile ni Hafidh, Panju, Ndomi.. Wengine siwakumbuki vizuri.
Hapo kwa Hafidh ilikua geti kali sana lakini tuliingia ndani mpk sebleni kipindi Mwl JK Nyerere ameaga dunia.. Tukaenda kuangalia matangazo ya live.

Daaah i wish i could share more.. Nimetoka huko mwaka 2002 nikiwa darasa la 6.
Pamoja Sana mkuu, kweli kabisa hafidhi niliisahau kumuweka hapo.
 
Back
Top Bottom