Museveni: Mali za mafisadi zitaifishwe

Museveni: Mali za mafisadi zitaifishwe

EMT

Platinum Member
Joined
Jan 13, 2010
Posts
14,477
Reaction score
15,347
Rais Yoweri Museveni wa Uganda amesema kuwa mali za maafisa wote watakaobainika kujihusisha na vitendo vya rushwa inapaswa zitaifishwe. Akizungumza na wajumbe wa chama tawala cha NRM katika Ikulu ya Entebbe, amesema ni tabia inayokera kwa maafisa wa serikali ya Uganda kuomba rushwa kutoka kwa wawekezaji.

Kwa mujibu wa Museveni, mizizi ya tabia ya rushwa inapaswa kung’olewa kwa sababu inapoteza rasilimali za taifa na kuchelewesha mabadiliko ya kiuchumi kwa wananchi wa Uganda. Rais Museveni amesisitiza kuwa ili hilo liweze kutekelezeka, inatakiwa serikali kuhakikisha inasimamia Sheria ya Uongozi kipengele cha 35.(a).

MO BLOG – RAIS WA UGANDA AWA MBOGO ATAKA MALI ZA MAFISADI KUTAIFISHWA.
 
Aanze kutaifisha mali zake kwanza.

walau kaonyesha njia mkuuu inaonekana hapendi uwizi wa mali za uma mwambie na jk aseme hivyo basi, siyo afanye aseme tuu!
 
TOFAUTI YA UGANDA NA tANZANIA NI KWAMBA TZ WANAAMINI ZAIDI KWENYE CHAMA WAKATI UGANDA WANAAAMINI ZAIDI KWA MSEVENI
 
Back
Top Bottom