Muongozo wa kununua vifaa vinavyotumia processor za intel

Kwa hii ni kundi gani
Intel(R) Pentium(R) CPU N3540 @ 2.16GHz 2.16GHz

hizi ni processor mpya za braswell zenyewe hazina nguvu sana ila zinatumia umeme mdogo sana kama watts 7 hivi, hivyo kifaa chake kitakuwa kinakaa sana na charge.
 
Computer nyingi tunazonunua huwa zinatumia processor za intel au amd, lakini ni intel ambaye ametawala sana kushinda amd kwenye computer zetu. Leo nimeamua niandike uzi huu kuhusu hizi processor za intel na namna ya kuzichagua ili kuwasaidia watu wanapotaka kununua laptop/desktop mpya wafanye maamuzi sahihi.

Processor ni nini?

Labda utakuwa unajiuliza kwa nini ukitaka kununua laptop mpya unatakiwa uangalie processor? Nini cha muhimu kuhusu hii processor?

-Kwa lugha rahisi processor ni kifaa ndani ya computer yako kinachobeba maagizo ya program za computer. Maagizo hayo yanaweza kuwa ya kimahesabu, kimantiki, maagizo yanayoingia kwenye computer na yanayotoka.

-jinsi processor inavyokuwa na speed kubwa ndio jinsi maagizo yatakavyofanywa haraka na ndio jinsi program za computer zitakavyofanya kazi upesi.
processor_01.jpg


Familia ya processor za intel

Intel wana processor za aina nyingi na ni ngumu kuzitaja kwa pamoja, ila wameturahisishia kwa kuzipanga processor zao kwenye familia. Na hii ndio familia yao.

1. Atom processor- processor hizi hutumika kwenye vimini laptop na tablet ni ndogo kiumbo ndio maana hata vifaa vyake ni vidogo, processor hizi hazina nguvu sana na vifaa vyake hukaa sana na chaji.

2. Celeron processor- Haina tofauti sana na atom ila hii ina afadhali kidogo. Inatumika kwenye vifaa vikubwa kuliko atom kama vile laptop kubwa na desktop

3. Pentium- hii ina speed kuliko celeron na atom pia inatumika kwenye vifaa vikubwa.

4. Core 2 duo- hii ni maarufu kwa perfomance yake ya multitasking, inauwezo wakufanya mambo mengi kwa wakati mmoja ila nyingi ni za kizamani.

5. Core i3- hii ni processor latest za intel ni dual core lakini core zake zina perfomance kubwa na pia inakuwa na thread 2 kwenye kila core, ni nzuri kwa wanaotaka perfomance kubwa kwa bei rahisi.

6. Core i5- ya laptop ni dualcore na ya desktop ni quadcore isiyokuwa na thread, software nyingi kubwa duniani zimekuwa optimized kutumia core kama za i5, ni nzuri sana kwa watu wanaotumia software zinazodemand perfomance lakini hawafanyi multitasking.

7.Core i7- hii inakuwa na quadcore processor na thread 8 kwenye desktop na pia inaweza kuwa dualcore kwenye laptop. Hii ndio processor nzuri zaidi kwa watu wa kawaida na inafanya multitasking hata kama software zinademand sana.

8. Xeon- hii ndio processor yenye speed zaidi kwenye processor za intel lakini imekuwa designed kufanya kazi kwenye computer kubwa kama vile server. Unapohost website processor kama hii ndio inayoprocess webpages.


Generation ya processor(muhimu)

Ni muhimu sana kujua processor inatokea generation ipi kuna processor zenye i7 ya 2010 ambazo zipo slow vibaya mno, na pia kuna uwezekano i3 kuipita i7 kwenye perfomance kama zinatoka generation tofauti. Hivyo eneo hili inabidi uwe makini kuepuka kuuziwa mbuzi kwenye gunia. Hivyo unaponunua laptop/desktop ni lazima ujue ipo generation gani la sivyo upo hatarini na hivi ndio namna ya kujua.

- Processor yenye namba inayoanziwa na elfu nne ni fourth generation(4xxx)
Mfano Intel i3-4130.

- Processor yenye namba inayoanziwa na elfu tatu ni third generation (3xxx)
Mfano i3-3130.

- Processor inayoanziwa na elfu mbili ni second generation(2xxx)
Mfano i3-2140

Sishauri kabisa kununua processor ya first generation, mtu unatakiwa atleast ununue ya second generation na pia bei inatakiwa iwe ndogo kwa hii second compare na third/fourth.

Processor ndogo kama atom na celeron zina generation zake ambazo ni
-clover trail
-bay trail

Processor za zamani za atom zilikuwa mbaya sana na zipo slow ila baytrail ikaja kuzipa nguvu na kuzifanya ziwe na perfomance kubwa, hivyo kama unataka kifaa cha atom/celeron make sure processor yake iwe inatoka generation ya baytrail.


Herufi za mbele ya processor(muhimu)

Kama umechunguza mbele ya processor kunakuwa na herufi mbali mbali hizi pia ni muhimu sana kuzijua kwani usipozizingatia unaweza kujuta.

Mfano processor inaweza kuitwa i5-4000m au i5-4000u au i5-4000y je nini kinatofautisha hizi processor?

1. Herufi kwenye processor za desktop.

Bila herufi – hii inakuwa na speed halisi ya processor mfano i7-4770

K- herufi hii inamaanisha processor ipo unlocked na unaweza kui over clock na kuongeza speeed. Processor yenye 3.5ghz unaweza kui overclock ikafika 4ghz. Jina lake linakuwa mfumo huu i7-4770K. ni nzuri sana kwa wanaocheza magame na kufanya rendering.

R- herufi hii inamaanisha processor hii ni ndogo sana na inaweza kutumika kwenye videsktop vyenye umbo dogo hali ya kuwa ina graphic kubwa kama iris pro. Jina lake linakuwa mfumo huu i7-4770R hii ni nzuri kwa wale wenye ofisi ambazo ni safi hawataki mawaya mengi na desktop kubwa kukaa kwenye meza. angalia picha hapo chini uone desktop ndogo.

brix1_s.gif


S- herufi hii inamaanisha hiyo proceesor wame optimize perfomance mara nyingi wanai underclock kuzuia processor kupata joto sana. Mfano i7-4770 ina 3.4ghz lakini i7-4770S ina 3.1ghz tu, ina maana hapa wamepunguza 300mhz kutoka stock kuja S.

T- herufi hii inamaanisha processor inatumia power ndogo, kwa wale wenzangu wanaotumia luku kama unataka desktop isiokula umeme basi hii ndio yenyewe ila perfomance nayo itapungua kidogo. Mfano wa jina ni i7-4770T

2. Herufi mbele ya processor za laptop(mobile)

Tumeshaona herufi mbele ya desktop, sasa hivi tuangalie herufi mbele ya processor za laptop ambazo pia zinaweza kutumika kwenye home theatre pc (htpc) au wengine wanaita mini desktop.

M- herufi hii inamaanisha hio processor ni mobile, ndio herufi common kwenye processor za laptop mfano i5-4000M

U- herufi hii inamaanisha processor ya laptop inatumia power ndogo hizi processor zinatumika sana kwenye vilaptop vyembamba (ultrabook). Kwa sababu zinakaa na chaji kutokana na kutumia power ndogo, perfomance yake nayo pia ni ndogo. Mfano i5 4250U

Y- hii ni ultra low power yaani inakula umeme mdogo kushinda hata U lakini vile vile perfomance inazidi kushuka nayo mfano i7-4610Y

HQ- herufi hii inamaanisha high perfomance, zinauzwa bei ghali sana na power yake inashindana na desktop. Usije ukajaribu kuieka kwenye mapaja laptop ya design hii maana zinashika moto upesi sana kutokana na quality ya processor. Ni nzuri kwa wale wanaopenda kucheza game, kutumia software kubwa wakiwa kitandani. Mfano ni i7-4700HQ

MQ- herufi hii inamaanisha hio procesor ni quad core. Kama umesoma vizuri juu i5 na i7 za desktop ni quadcore lakini za laptop ni dualcore, hivi processor hii inamaanisha unaweza tumia quadcore kwenye laptop yako kama unataka mfano i7-4900MQ

MX- herufi hii inamaanisha ni xtreme edition, processor hii unaweza kui over clock kama vile K series ya desktop na ina perfomance kubwa sanaaa, ila kuwa makini na mapaja tu.
Mfano i7-4940MX

Huu ndio muongozo wa kununua processor za intel, kama kuna sehemu hujapaelewa unaweza kuuliza nitaelezea zaidi.

Kuna wataalamu wengine wanasema upo ujuzi wa kubadilisha Processor, kwa maana unaweza kutoa ndogo na kuweka kubwa kwenye Laptop au Desktop. Hili likoje.
 
Kuna wataalamu wengine wanasema upo ujuzi wa kubadilisha Processor, kwa maana unaweza kutoa ndogo na kuweka kubwa kwenye Laptop au Desktop. Hili likoje.

yap processor inabadilishwa
1.kwa desktop nafikiri zote zinabadilishika
2. kwa laptop inabidi ufungue halafu uangalie kama ipo socketed (inachomoka) kuna nyengine zinachomelewa humo humo huwa hazitoki.

kwa desktop unaangalia tu aina ya motherboard mfano motherboard inaitwa lga-1150 basi hii inakubali processor zote za haswell (4th generation) iwe ni pentium, i3, i5, i7, xeon nk zote zitakubali cha muhimu tu uwe na cooler (feni) ambalo litapulizia vizuri. mfano computer ilikua na processor ya pentium ambayo thermal design power (TDP) yake ni 54 watts na kafeni kadogo ukabadili ukaeka i7 ambayo TDP yake ni 88W basi kale kafeni hakatapuliza vizuri hii i5 na computer itapata moto sana itabidi ueke feni kubwa kubwa

kwa laptop kubadilisha sio tu unaangalia motherboard bali pia unatakiwa uangalie na TDP (sababu huwezi kubadilisha mafeni ya laptop ukaeka makubwa) kuna processor za aina mbili hapa ambazo unatakiwa uzijue
-zinazoishiwa na u mbele
-zinazoishiwa na m mbele

hizi zinazoishiwa na u mbele nyingi zina TDP ya 15w zinatumia umeme mdogo hivyo ukibadili processor yake itabidi utafute u mwenzake. mfano unabadili i3 4010u kwenda i7 4600u

zinazoishiwa na m mbele nyingi zina TDP ya 35-37w ambayo ni kubwa kwa laptop hivyo ukibadilisha processor yabidi utafute yenye m kwa mbele. mfano i3 4000m ibadili iwe i7 4600m.

si kazi ngumu sana ni rahisi sana,
 
yap processor inabadilishwa
1.kwa desktop nafikiri zote zinabadilishika
2. kwa laptop inabidi ufungue halafu uangalie kama ipo socketed (inachomoka) kuna nyengine zinachomelewa humo humo huwa hazitoki.

kwa desktop unaangalia tu aina ya motherboard mfano motherboard inaitwa lga-1150 basi hii inakubali processor zote za haswell (4th generation) iwe ni pentium, i3, i5, i7, xeon nk zote zitakubali cha muhimu tu uwe na cooler (feni) ambalo litapulizia vizuri. mfano computer ilikua na processor ya pentium ambayo thermal design power (TDP) yake ni 54 watts na kafeni kadogo ukabadili ukaeka i7 ambayo TDP yake ni 88W basi kale kafeni hakatapuliza vizuri hii i5 na computer itapata moto sana itabidi ueke feni kubwa kubwa

kwa laptop kubadilisha sio tu unaangalia motherboard bali pia unatakiwa uangalie na TDP (sababu huwezi kubadilisha mafeni ya laptop ukaeka makubwa) kuna processor za aina mbili hapa ambazo unatakiwa uzijue
-zinazoishiwa na u mbele
-zinazoishiwa na m mbele

hizi zinazoishiwa na u mbele nyingi zina TDP ya 15w zinatumia umeme mdogo hivyo ukibadili processor yake itabidi utafute u mwenzake. mfano unabadili i3 4010u kwenda i7 4600u

zinazoishiwa na m mbele nyingi zina TDP ya 35-37w ambayo ni kubwa kwa laptop hivyo ukibadilisha processor yabidi utafute yenye m kwa mbele. mfano i3 4000m ibadili iwe i7 4600m.

si kazi ngumu sana ni rahisi sana,

Sawa elimu tosha hii.
 
chief, samahani. hivi kuna uwezekano wa kubadili mashine yako kutoka grade moja kwenda nyingine? mfano unakuta mashine yako ni i3 then una upgrade to i5 na je vipi kama utabadili pamoja na ram kutoka 1g kwenda zaidi
 
chief, samahani. hivi kuna uwezekano wa kubadili mashine yako kutoka grade moja kwenda nyingine? mfano unakuta mashine yako ni i3 then una upgrade to i5 na je vipi kama utabadili pamoja na ram kutoka 1g kwenda zaidi

Yap inawezekana kabisa
 
Mkuu Chief-Mkwawa, nina simu ya Zenfone 5 (ASUZ) Intel Atom Z2580, Dual core 2ghz. Unaweza kuilinganisha na processor gani ya snapdragon?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Chief-Mkwawa, nina simu ya Zenfone 5 (ASUZ) Intel Atom Z2580, Dual core 2ghz. Unaweza kuilinganisha na processor gani ya snapdragon?

Kama snapdragon 600 hv. Lakin intel yupo vizuri cpu tu na kwenye simu cpu tupu haina maana inatakiwa soc nzima iwe ya ukweli vitu kama gpu, bluetooth, modem za network, wifi nk
 
Last edited by a moderator:
Kama snapdragon 600 hv. Lakin intel yupo vizuri cpu tu na kwenye simu cpu tupu haina maana inatakiwa soc nzima iwe ya ukweli vitu kama gpu, bluetooth, modem za network, wifi nk

Mkuu naomba unijulishe hii processor iko kundi gani na pia vipi inaweza stahimili game nzito(maana mi ni mpenzi wa gaming)

PROCESSOR : AMD A4 - 3300 APU with Radeon(tm) HD Graphics 1.9 Ghz

RAM : 4.00 GB (2.24 GB usable)

SYSTEM TYPE : 32-bit operating system, x64-based processor
 
Mkuu naomba unijulishe hii processor iko kundi gani na pia vipi inaweza stahimili game nzito(maana mi ni mpenzi wa gaming)

PROCESSOR : AMD A4 - 3300 APU with Radeon(tm) HD Graphics 1.9 Ghz

RAM : 4.00 GB (2.24 GB usable)

SYSTEM TYPE : 32-bit operating system, x64-based processor

kabla hatujaenda kuangalia hii processor unatakiwa ubadili windows kwenye hii machine eka 64bit windows ili uweze kutumia ram yako yote na perfomance itaongezeka.

kuhusu nguvu ya processor nikukatishe tu tamaa hii processor ni dhaifu, utaweza cheza game ndogo ndogo kama za mpira ila ukija games nzito itachemka. ila zipo games za zamani siku zote hivyo hutakosa games za kucheza
 
kabla hatujaenda kuangalia hii processor unatakiwa ubadili windows kwenye hii machine eka 64bit windows ili uweze kutumia ram yako yote na perfomance itaongezeka.

kuhusu nguvu ya processor nikukatishe tu tamaa hii processor ni dhaifu, utaweza cheza game ndogo ndogo kama za mpira ila ukija games nzito itachemka. ila zipo games za zamani siku zote hivyo hutakosa games za kucheza

Ahsante mkuu VP huwa kuna uwezekano wa kubadili processor na kuweka ambayo iko more powerful? Kama inawezekana vp gharama zake zikoje?
 
Ahsante mkuu VP huwa kuna uwezekano wa kubadili processor na kuweka ambayo iko more powerful? Kama inawezekana vp gharama zake zikoje?

kwanza inavyoonekana cpu yako ni a4 3300m na sio 3300.

ipo kwenye kifaa gani hio cpu? laptop au desktop?

mara nyingi cpu za laptop kubadili inakuwa ngumu zipo zinazokubali na zipo zisizokubali
 
kwanza inavyoonekana cpu yako ni a4 3300m na sio 3300.

ipo kwenye kifaa gani hio cpu? laptop au desktop?

mara nyingi cpu za laptop kubadili inakuwa ngumu zipo zinazokubali na zipo zisizokubali

Hii ipo kwenye laptop mkuu .na nashukuru kwa elimu yako
 
kwanza inavyoonekana cpu yako ni a4 3300m na sio 3300.

ipo kwenye kifaa gani hio cpu? laptop au desktop?

mara nyingi cpu za laptop kubadili inakuwa ngumu zipo zinazokubali na zipo zisizokubali

Mkuu naomba unifahamishe unapoamua kununua RAM au processor ili uireplace ile ya mwanzo ,unanunua tu yeyote au kuna vitu vya kuzingatia? ukizingatia pia zina kuwa na muonekano na size tofautitofauti kdogo sasa je mafundi huwa wanazifix vipi katika kifaa chako?
 
Mkuu naomba unifahamishe unapoamua kununua RAM au processor ili uireplace ile ya mwanzo ,unanunua tu yeyote au kuna vitu vya kuzingatia? ukizingatia pia zina kuwa na muonekano na size tofautitofauti kdogo sasa je mafundi huwa wanazifix vipi katika kifaa chako?

njia rahisi zaidi ni kwenda website ya kifaa chako kilipotengenezewa halafu uangalie full specification ya hicho kifaa, hapo ndo utajua ni ram za aina gani na processor za aina gani unaweza badili.

ram za computer so far zipo kuanzia ddr1, ddr2, ddr3 na ddr4 hivyo kuna chance kubwa computer yako inatumia moja wapo kati ya hizo, lakini huishii hapo hizo ddr nazo zimegawanyika hasa kwa vifaa ambavo si desktop kama simu,tablet, laptop, mini desktop nk zenyewe viram vyake vinakuwa vidogo huwezi tu ukaweka ukubwa wa kawaida hivyo tunarudi pale pale juu itabidi ukaangalie specs za mashine yako

na processor nayo ni motherboard ndio itakayoamua unaweza kuweka processor gani, ili kuijua motherboard yako itabidi uangalie specs zake kwa manufacture, pia itabidi uifungue uangalie kama processor inatoka au imechomelewa, kama imechomelewa hakuna njia ya kui upgrade
 
vipi kuhusu bei kama ya processor za i5 na i7 kwa Dar zinakuwa ni kiasi gani?
 
Back
Top Bottom