Ni kweli lakini umeielezea kiwepesi sana. Kimsingi unaweza ukatengeneza urafiki na mkeo mkiws tayari ndani ya ndoa.
Urafiki huwa unawezekana mkipunguza mipaka ya kihisia kati yenu.
Unaweza kuta mwanaume hataki kucheka na mkewe kwasababu anahisi atamdharau kulingana malezi amekulia muda wote kanuna ndani ya nyumba, ni mtu wa amri na kukaripia, mwanamke anaishi nae kwa hofu na hawana urafiki but hapendi muona anacheka na jinsia ya kiume.
Lakini pia wapo wanawake mwanaume akiwa too friendly anaanza kujisahau wajibu wake na kuendekeza mizaha na kusahau yupo na mume wake. Kwa kifupi ni kama kuishi na baba yako unaweza cheka nae, piga nae story ila unakuwa na heshima nae kwa kuchunga kauli.
Kimsingi ukitaka mkeo awe best friend wako, invest mazungumzo na vitendo vyenu katika maswala ya kimaendeleo. Tazamieni project za familia yenu. Mfano, kujenga nyumba, kununua gari, kufungua na kusimamia biashara, kuplan namna ya kupata watoto na idadi yao pamoja na kulea ujauzito na kuwakuza na kusimamia malezi yao. Hapo sijaongeza entertainment yaani kutoka out na kadhalika, haya mambo yanaweza chukua 90% ya muda wenu na hiyo 10% ya muda ndio mkashea na ndugu na jamaa.
Shida moja ni unakuta watu wanatumia sehemu kubwa ya muda kufikiria mambo negative, mfano, wanaume/wanawake wanacheat vipi, namna ya kujikinga na mashambulizi ya ukweni na mawifi, ubaya wa marafiki kwenye ndoa, namna ya kununua kiwanja na kujenga bila mume /mke kujua, nitajuaje kama watoto ni wangu ama la, namna ya kuficha mume asijue kuwa amebambikiwa mtoto, namna ya kuimarisha penzi kwa kutumia mkongo, mganga mzuri mwenye dawa za kushika akili ya mume asione wengine, mbinu za kurithi mali za mume bila kusumbuliwa na ndugu haya na mengine ndio taka zinazozunguka katika vichwa vya vijana. Ndio maana they can't be best of friends.