Bi mdogo;
Kuna mambo mawili matatu naweza kukusaidia kutokana na maelezo yako.
Moja;
Hivi, biashara yenu imechanua zaidi? Je, Hapo anapofanyia hiyo biashara kuna mazingira yanayo mfanya atumie akili na nguvu nyingi za mwili? Hayo humchosha mtu saana na anapokuja nyumbani anajikuta bado anawaza ya shughuli.
Pili;
Una mtoto mchanga, kumbuka ana hitaji saana usafi. Ni jambo ambalo ni jipya kwako. Una usafi? Mtoto awe msafi, weye uwe msafi, kitanda kiwe kisafi?? Utashangaa, chumba kinajaa nepi chafu au pampas zilizotumila au hata ambazo hazijatumika zinazagaa kila kona ya nyumba.
Mumeo, hili ni jipya kwake.
Tatu;
Sijui weye ni kabila gani, lakini kuna makabila wanapenda kuwatunza wake zao kwenye kipindi hiki cha uzazi. Unaweza ulibugia uji zaidi ukanenepeana, harufu ile ya maziwa yanayovuja etc. Je, upo sawa hapo? Chunga hayo na ujiweke fit. Usijiachie ukajikuta umechepuka