cocochanel
Platinum Member
- Oct 6, 2007
- 26,793
- 73,544
Wanaume wengi wanao oa wasichana na kutenda hayo ya kulala na ndugu za mwanamke bila kujali huwa wameoa kwa ajili ya kitu.
Sijui juu yake ila kama kwenu mna uwezo zaidi ya alipotoka basi ndicho alichofata na ameamua kufanya hayo anayofanya.
Unaweza kuta walianza kulala pamoja tangu umemtambulisha kwa mama yako,na yeye kukuacha isingewezekana ili awe na mama yako ambaye lazima amemuhakikishia maisha mazuri na labda anamuhonga juu.
Hivyo kukuoa wewe sababu alikuona kwanza ndio imekuwa rahisi juu yao kuwa pamoja hadi leo. Na umegundua sababu za mwizi ni arobaini.
Una babu yako na ndugu wengine kaongee nao, huyo mwanaume hakufai. Ukikaa chini ukitulia sasa hivi jipe siku chache utakumbuka matukio yaliyotokea na sababu hukujua ndio utagundua kweli ulikuwa gizani huku yao yanaendelea.
Kama mfano wao pia kutaka kujua upo wapi ili wajipange n.k. kiukweli sitaki hata kuingiza kichwani mimi na mama yangu aliyenizaa kulala na mtu mmoja. Pole sana ila mwanaume hakupendi na mama yako amamfurahisha zaidi na I guess mali na kumtunza vinachangia kiaina. Sipati picha ukiwasamehe utaishije nao, kamwe hautawaamini tena tena na wataendelea upende usipende.
Labda uache sasa kumnyenyekea na kumuonyesha una maisha na muombe Mungu akuongoze. Usijishushe kuwapa raha.
Umaweza kuwa umejiweka kama vile yeye ndie mwisho wa reli, pia sababu kubwa ulikosa kukua na baba yako(RIP). Jipe muda utaona matukio yanakujia ndipo utaona kweli hakufai. Kama una ndugu wa karibu unaweza kwenda kumuona leo nenda hata ukalale huko.
Mama yako amefanya kitendo kibaya sana na cha aibu usikimbilie kumbembeleza muache ajute akijua, ukimwonyesha upo weak ataendelea hata kwa bwana mwingine utakayepata.
Usimtukane bali mshushie vipande haswa vimuingie amekutenda vibaya sanaaaaa, umesoma umeishi nje unajua naongelea nini. Hana penzi au anajuta kuzaa mapema labda kumemkosesha maisha fulani, sorry ila hiii utokea labda atakuambia ukweli. Wengine upelekea wamama kuwa na wivu na hivyo kutaka kuingilia kila kitu ili nawe usile raha kihivyo sababu alikosa raha. Sasa kaa fikiria utaona kuna mavitu maishani mwako kuonyesha mama yako yukoje kwako.
Kila la kheri katika maisha yako na uamuzi...ila mumeo sio mume una umri mdogo fikiria.
Sijui juu yake ila kama kwenu mna uwezo zaidi ya alipotoka basi ndicho alichofata na ameamua kufanya hayo anayofanya.
Unaweza kuta walianza kulala pamoja tangu umemtambulisha kwa mama yako,na yeye kukuacha isingewezekana ili awe na mama yako ambaye lazima amemuhakikishia maisha mazuri na labda anamuhonga juu.
Hivyo kukuoa wewe sababu alikuona kwanza ndio imekuwa rahisi juu yao kuwa pamoja hadi leo. Na umegundua sababu za mwizi ni arobaini.
Una babu yako na ndugu wengine kaongee nao, huyo mwanaume hakufai. Ukikaa chini ukitulia sasa hivi jipe siku chache utakumbuka matukio yaliyotokea na sababu hukujua ndio utagundua kweli ulikuwa gizani huku yao yanaendelea.
Kama mfano wao pia kutaka kujua upo wapi ili wajipange n.k. kiukweli sitaki hata kuingiza kichwani mimi na mama yangu aliyenizaa kulala na mtu mmoja. Pole sana ila mwanaume hakupendi na mama yako amamfurahisha zaidi na I guess mali na kumtunza vinachangia kiaina. Sipati picha ukiwasamehe utaishije nao, kamwe hautawaamini tena tena na wataendelea upende usipende.
Labda uache sasa kumnyenyekea na kumuonyesha una maisha na muombe Mungu akuongoze. Usijishushe kuwapa raha.
Umaweza kuwa umejiweka kama vile yeye ndie mwisho wa reli, pia sababu kubwa ulikosa kukua na baba yako(RIP). Jipe muda utaona matukio yanakujia ndipo utaona kweli hakufai. Kama una ndugu wa karibu unaweza kwenda kumuona leo nenda hata ukalale huko.
Mama yako amefanya kitendo kibaya sana na cha aibu usikimbilie kumbembeleza muache ajute akijua, ukimwonyesha upo weak ataendelea hata kwa bwana mwingine utakayepata.
Usimtukane bali mshushie vipande haswa vimuingie amekutenda vibaya sanaaaaa, umesoma umeishi nje unajua naongelea nini. Hana penzi au anajuta kuzaa mapema labda kumemkosesha maisha fulani, sorry ila hiii utokea labda atakuambia ukweli. Wengine upelekea wamama kuwa na wivu na hivyo kutaka kuingilia kila kitu ili nawe usile raha kihivyo sababu alikosa raha. Sasa kaa fikiria utaona kuna mavitu maishani mwako kuonyesha mama yako yukoje kwako.
Kila la kheri katika maisha yako na uamuzi...ila mumeo sio mume una umri mdogo fikiria.