Mume wake anawamini marafiki kuliko mke wake

Mume wake anawamini marafiki kuliko mke wake

kuna jamaa nae akisafiri anapaki gari kwa dada ake wakati mke yupo na anajua ku drive
watu wengine ni bure kabisa hayafai kwa matumizi ya binadamu

Huwezi jua mke wake anatabia gani, kuna baadhi ya wanawake ni kadeshiani yaani kichwani hakuna kitu.
 
Ila wanaume wa siku hizi they sooo selfish selfish mno hayo mambo yapo ila pia inatrgemewa na umelelewaje kwenu wanaume wengi wanakuaga na roho mbaya sana...cha msingi wanawake tuwaignore tu cha msingi tutafute vya kwetu
 
Mmmmmmmmmmh........umesema Miaka 8???

Sasa kama aliweza kuvumilia yote hayo miaka 8 kinachomfanya ashindwe kuvumilia sasa ni niji???

Walikua wanaishi maisha ya kawaida baada ya mwanaume kujenga na kununua gari ndo izotabia zikajitokeza, alishakaa chini akamwambia mumewe nikiasi gani ilo jambo linavyo muumiza lakini yeye mwanaume aoni kama kunatatizo kumwachia ndugu yake
 
Kwanza kama huna ndoa huwezi elewa ila wanawake wengine wako kwenyendoa kuharibu future ya MTU hawapo kama wanawake wa kujenga familia ni wapangaji tu wakutoa Mali kwa mumewe na kuhamishia kwao
 
kuna jamaa nae akisafiri anapaki gari kwa dada ake wakati mke yupo na anajua ku drive
watu wengine ni bure kabisa hayafai kwa matumizi ya binadamu
Anampenda mkee kupita maelezo hataki apate ajali wakati mumewe anapokuwa safarini. Kupenda bana, sio yote ya ndoa ya mwenzako utayajua hadharani.
 
Aendelee kumwonesha uaminifu na upendo, atabadulika taratibu, kuna wanaume wengine wamejazwa ujinga kuwa usimwamini mke, nao wanakubali bila kujua kuwa ndiye pekee mwenye uchungu na watoto wake, utakuta hata mali nyingine wanaandika ndugu, wakifa watoto wanapata shida, kuondoa mawazo hayo hakuhitaji haraka, aende taratibu

hakika upo sahihi japo nataka nikudodose kitu hapa ndugu Yangu . Mali kuandikwa majina ya ndugu sio sahihi lkn inatokea tu kama sijabahatika kuwa na mtoto hata mmoja , na labda nimeoa kabila flani hivi ambalo wanatamaa sana na Mali na nimeoa wakati hizo mali ninazo lazima zipigwe chata ya ndugu hapo
 
Wakuu nahitaji ushauri ninarafiki yangu ameolewa lakini amekuwa amwelewi mume wake, yaani Mme wake anaamini ndugu zake kuliko mke wake, waga akisafiri funguo za gari anamwachia ndugu yake ambaye ni mdogo wake kodi za wapangaji mdogo wake ndo anapokea, akimwambia kwanini anafanya Ivyo anamwambia kwani alishawai kumlaza njaa!! Kiukweli uyu best yangu ameniomba ushauri nimeshindwa cha kumshauri ndo mana nimeleta kwenu wakuu tushee mawazo kwa pamoja!!

Akunyimaye chakula anakupunguzia ushuzi. Mwambie afurahi tu anakula analala anavaaa, Anamwepusha madhara yanayofuatana na hela hizo kwa kuwa mume anaujua udhaifu wa mkewe juu ya hela.
 
Huyo kazi yake ni kutotoa watoto,hayo mengine hayamuhusu.
Over
 
Sasa kama mwanamke aliolewa akamkuta mdogo mtu yuko kwenye hayo alokabidhiwa na kaka yake...ni ngumu kubadili mfumo haraka haraka jamaa yuko sawa kabisa big up kwake!!
Mwanamke uingie leo utake kila kitu kiwe under control yko hata kwangu haiwezekani jikon tu ndo kutakua under control yake!
 
Anampenda mkee kupita maelezo hataki apate ajali wakati mumewe anapokuwa safarini. Kupenda bana, sio yote ya ndoa ya mwenzako utayajua hadharani.

Uchoyo na ubinafsi....anamuepushia ajali ye ni Mungu?
 
huenda mwanamke alikuwa anaiba mali ya mmewe sasa mme kagundua akaonjia ya kumkomesha ndo hiyo hebu jaribu kulidads hilo kwa huyo rafk yako
 
Mfyuuuu
Si akamuoe dada yake....

Mwanbie mke kama ana gari akisafiri hadi nguo ahamishie kwao....

Mijanaume anbayo haijakomaa akili sijui kwa nini inaoa
Yani acha tu, teh kwanza hata kabla hajalinunua hakumtaarifu wife
kila siku linalala kwa jirani akisafiri linalala kwa dada
wife akagundua after two months mme ana gari
ntasutwa!!! Ila wanaume wengine ni wakushauri warudi kwa mama zao tu...wana ndevu ila ni watoto
 
Don't rush into one-sided judgemental opinion kwa vile tu anaefanyiwa hivyo ni mwanamke mwenzako. Huwezi kujua ni nini/nani chanzo cha hiyo behavioural action which appears likely to be a 'mistreatment' kwa mkewe. Better you could hear the other side of the story so as to know the real shits popping-up in such marriage.
Uchoyo ubinafsi that's all
 
Jamani msiwe wepesi wa kuhukumu mambomkama hayo,,
Kwani sababu anazijua mume na mke
Mfano nakumbuka nilivyo kuwa darasa la nne baba angu mdogo alikuwa ameowa ila hela ya matumizi alikuwa anamwachia dada wa kazi..
Akisafiri funguo za gari anaacha kwa jirani..
Matumizi yote dada wa kazi..kumbuka hapo wife hana kazi
Tatizo lilikuwa nguvu za giza..
Mke wake alikua anaingiwa na nguvu flani kiasi kwamba anafanya vitu vingi vya ovyo then akirudi katika hali ya kawaida anakuwa hakumbuki maisha alio ishi nyuma..
Ilifikia hatua akiwa unsound mind akawa anaficha mali za mmewe mfano sim funguo za gari
Nk..ikafikia hatua hela zikawa hazikai ndani mfano budget ya mwezi..mke akipewa zinapotea katika mazingira ya utata...
Mke alikuwa akiambiwa unafanya hili na lile akawa haamini,, mpa wamrekodi video..
Sasa mme alifanya maamuzi ambayo mke alikuwa anaumia then analalamika kwa majirani...
So tusiwe wepesi wa kuhukumu..
 
Hilo janaume ni lichoyo na libinafsi

Na dawa ya mijanaume michoyo ni mke kutafuta vyako tu.......

Nunua kiwanja then unamwambia nimenunua kiwanja hati anahifadhi mama/sista/baba

Nunua gari ukisafiri peleka kweny ikishindikana safiri na funguo gari laza ccm...

Miezi 2 tu atanyooka maana mchoyo ukimlipizia roho inamuuma.

Kuna jirani yangu mmoja alinunua kiwanja na kujenga halafu akamuandikisha dada yake urithi......alichofanya mke akanunua kiwanja chake...mwanaume alihangaika hadi kwa padri ili mwanamke amuweke kwenye kiwanja.....
Mfyuuuu za michoyo na mibinafsi



Yani acha tu, teh kwanza hata kabla hajalinunua hakumtaarifu wife
kila siku linalala kwa jirani akisafiri linalala kwa dada
wife akagundua after two months mme ana gari
ntasutwa!!! Ila wanaume wengine ni wakushauri warudi kwa mama zao tu...wana ndevu ila ni watoto
 
Mmmmmh bajeti dada wa kazi?????


Jamani msiwe wepesi wa kuhukumu mambomkama hayo,,
Kwani sababu anazijua mume na mke
Mfano nakumbuka nilivyo kuwa darasa la nne baba angu mdogo alikuwa ameowa ila hela ya matumizi alikuwa anamwachia dada wa kazi..
Akisafiri funguo za gari anaacha kwa jirani..
Matumizi yote dada wa kazi..kumbuka hapo wife hana kazi
Tatizo lilikuwa nguvu za giza..
Mke wake alikua anaingiwa na nguvu flani kiasi kwamba anafanya vitu vingi vya ovyo then akirudi katika hali ya kawaida anakuwa hakumbuki maisha alio ishi nyuma..
Ilifikia hatua akiwa unsound mind akawa anaficha mali za mmewe mfano sim funguo za gari
Nk..ikafikia hatua hela zikawa hazikai ndani mfano budget ya mwezi..mke akipewa zinapotea katika mazingira ya utata...
Mke alikuwa akiambiwa unafanya hili na lile akawa haamini,, mpa wamrekodi video..
Sasa mme alifanya maamuzi ambayo mke alikuwa anaumia then analalamika kwa majirani...
So tusiwe wepesi wa kuhukumu..
Evelyn Salt njoo uone
 
Last edited by a moderator:
Uchoyo ubinafsi that's all
U wanna tell me kwamba kwenye ndoa zoooote zinazoenda hovyo hovyo na kuyumba, ni wanaume pekee ndo causatives??!!! Nyie wanawake ni malaika eeh? Hakuna wanawake ambao ni wachoyo & selfish kwenye ndoa na huwanyanyasa waume zao?

As long as we are human beings, provided that IMPERFECTION was inherited by all humans, then any spouse (me au ke) can mess up in their marriage! Jenga hoja, na sio kutoa 'majibu rahisi'. BTW... mekumiss mpk nakonda moyo. Unajua dada nakotogirwe sanaaa
 
Back
Top Bottom