Mume wake anawamini marafiki kuliko mke wake

Mume wake anawamini marafiki kuliko mke wake

wakuwin

Member
Joined
Sep 6, 2015
Posts
12
Reaction score
1
Wakuu,

Nahitaji ushauri ninarafiki yangu ameolewa lakini amekuwa amwelewi mume wake, yaani mme wake anaamini ndugu zake kuliko mke wake, waga akisafiri funguo za gari anamwachia ndugu yake ambaye ni mdogo wake kodi za wapangaji mdogo wake ndo anapokea.

Akimwambia kwanini anafanya hivyo anamwambia kwani alishawai kumlaza njaa!Kiukweli uyu best yangu ameniomba ushauri nimeshindwa cha kumshauri ndo mana nimeleta kwenu wakuu tushee mawazo kwa pamoja!
 
Mwambie aje atueleze Ndoa yao ina mda gani, je hapo kabla ya ndoa hali ilikuaje?
Je mahusiano yake namumewe yako katika hali gani?
 
kuna jamaa nae akisafiri anapaki gari kwa dada ake wakati mke yupo na anajua ku drive
watu wengine ni bure kabisa hayafai kwa matumizi ya binadamu
 
Kuna shida kwenye hiyo ndoa. Always it is not advisable kutoa conclusive judgement kwa kusikiliza upande mmoja tu. Ndoa ni voluntary union kati ya watu wawili. Putting into account kwamba HUMAN BEINGS (male/female) are complex animals by nature, then kuna haja ya kusikiliza na upande wa pili pia. So dada rubii's insights (above) are well hinted.
 
Last edited by a moderator:
Ndoaaaaaa!!!
Ni taasisi pekee inayotoa Vyeti kabla,,, ingekuwa vinatolewa baada ya kuishi hata kwa only 2yrs wengi tusinge graduate,,
 
Kyoma maelezo yako ni sahihi kabisa!

hili suala ni baya lakini cha ajabu watu wengine wanaonekana kuliunga mkono. Labda nao wana vyeti vya aina hiyo!

Ninakubalina na wewe kuwa hao wangeliweza tu kuchaguliwa hata bila kununa hizo elimu feki. Kama mtu anasema ana phD na wakati ni amepata cheti na elimu ya juu mtu wa aina hiyo anachaguliwa kuwa waziri na inapotokea anakwenda kwenye argument na maziri wenzanke wkenye intenationa argument, he/she will always flop.
Prof Msolla aleisema lakini kuanzia hapo yuko kimya!

kundelea kubishana na anayetetea hili suala la vyeti ni kupoteza muda kama naye ana cheti cha aina hiyo!!

Aisee!!! Umesema jambo msingi sana.
 
kuna jamaa nae akisafiri anapaki gari kwa dada ake wakati mke yupo na anajua ku drive
watu wengine ni bure kabisa hayafai kwa matumizi ya binadamu

Don't rush into one-sided judgemental opinion kwa vile tu anaefanyiwa hivyo ni mwanamke mwenzako. Huwezi kujua ni nini/nani chanzo cha hiyo behavioural action which appears likely to be a 'mistreatment' kwa mkewe. Better you could hear the other side of the story so as to know the real shits popping-up in such marriage.
 
Binadamu wengine ni malimbukeni sana wakipata mali au madaraka lkn all in all kuna shida hapo
 
Mfyuuuu
Si akamuoe dada yake....

Mwanbie mke kama ana gari akisafiri hadi nguo ahamishie kwao....

Mijanaume anbayo haijakomaa akili sijui kwa nini inaoa


kuna jamaa nae akisafiri anapaki gari kwa dada ake wakati mke yupo na anajua ku drive
watu wengine ni bure kabisa hayafai kwa matumizi ya binadamu
 
Aendelee kumwonesha uaminifu na upendo, atabadulika taratibu, kuna wanaume wengine wamejazwa ujinga kuwa usimwamini mke, nao wanakubali bila kujua kuwa ndiye pekee mwenye uchungu na watoto wake, utakuta hata mali nyingine wanaandika ndugu, wakifa watoto wanapata shida, kuondoa mawazo hayo hakuhitaji haraka, aende taratibu
 
Wakuu nahitaji ushauri ninarafiki yangu ameolewa lakini amekuwa amwelewi mume wake, yaani Mme wake anaamini ndugu zake kuliko mke wake, waga akisafiri funguo za gari anamwachia ndugu yake ambaye ni mdogo wake kodi za wapangaji mdogo wake ndo anapokea, akimwambia kwanini anafanya Ivyo anamwambia kwani alishawai kumlaza njaa!! Kiukweli uyu best yangu ameniomba ushauri nimeshindwa cha kumshauri ndo mana nimeleta kwenu wakuu tushee mawazo kwa pamoja!!
Kwani alienda kuolewa au kushika funguo za gari na kupokea kodi za nyumba!!??
 
Labda anamuona mpenda mali mno. ..gold digger
Hilo neno. Naamini kwa mwanaume anayefanya vile jua mke wake anafuja mali au ana mtindo wa kupeleka fedha au mali nyingine kwa ndugu zake kwa kificho. Ili kuepusha mtikisiko katika familia, ni bora ukamwachia mapato mtu baki.
 
Tabia zingine ni ubinafsi sana. Kweli mwenza wako unaweza mfanyia vitu kama hivyo?
Hata kama anamapungufu flani lakini sio kufikia hatua ya kumuweka chini ya ndugu zako au mtu mwingine baki.
Ndoa zetu huwa tuna zialibu sisi wenyewe kabla ya majirani.
 
ameshaujua udhaifu wa mkewe ndio maana akafanya ivo. hebu mhoji vizuri uyo rafiki yako
 
Kuna shida kwenye hiyo ndoa. Always it is not advisable kutoa conclusive judgement kwa kusikiliza upande mmoja tu. Ndoa ni voluntary union kati ya watu wawili. Putting into account kwamba HUMAN BEINGS (male/female) are complex animals by nature, then kuna haja ya kusikiliza na upande wa pili pia. So dada rubii's insights (above) are well hinted.

Yah!! Wakujage Tuu Wote Hapa Ndio Tujue Shida Iko Wapi.
 
Last edited by a moderator:
Don't rush into one-sided judgemental opinion kwa vile tu anaefanyiwa hivyo ni mwanamke mwenzako. Huwezi kujua ni nini/nani chanzo cha hiyo behavioural action which appears likely to be a 'mistreatment' kwa mkewe. Better you could hear the other side of the story so as to know the real shits popping-up in such marriage.




Mwambie aje atueleze Ndoa yao ina mda gani, je hapo kabla ya ndoa hali ilikuaje?
Je mahusiano yake namumewe yako katika hali gani?

Ndoa yao inamiaka nane na wana watoto watatu
 
kuna jamaa nae akisafiri anapaki gari kwa dada ake wakati mke yupo na anajua ku drive
watu wengine ni bure kabisa hayafai kwa matumizi ya binadamu[/QUOTE
Duuh hiyo kali hapo unatafuta hela hata za kuhongwa unanunua la kwako..
 
Back
Top Bottom