Halooooooooo! UKILA NA KIPOFU USIMSHIKE MKONO!
Mapenzi ya wizi sharia yake moja tu, usiwe na wivu wa kisengery!!!!! Wewe wahudumiwa na gari ushanunuliwa (Kama hutojali nipashe ni aina gani ya ndinga?) watimiziwa yooote, pressure ya nini? Wewe tulia kama maji ya mtungi.
Tena ukikutana muulize wife hajambo, watoto shule wanaendeleaje? Muulize shule kaenda kukagua maendeleo ya wanae. Siku ingine jizoe mlimani city ununue tu bag twa ben ten, vimkebe sijui vya micky mouse na vi game umpe awapelekee wanae zawadi. Jikombe bibi na ujikombe haswa haswa! Ulizia wife afya vipi, kaznia anaendelaje. Be on his side and support hio ndoa 100%
Mwanaume anapenda mwanamke anaejua nafasi yake. Na wewe nafasi yako ni Forever Second (Chungu lakini dawa) sasa harakati za kutaka kuchukua Throne na kujitwalia kingdom zitakuponza kweli kweli. Accept ya position na uimiliki kwa nafasi yako, after role mwenzio mlinda nyumba wakati wewe ndo the doll at his side wa kula nae goodtimes.