Wapendwa wadau wa Elimu JF,
Inasemekana kuwa serikali kupitia Wwizara yake ya Elimu, imeamua kuwa mtihani wa Hisabati darasa la saba mwaka huu utakuwa na maswali yote ya kuchagua (multiple-choice questions). Haiingii akilini uamuzi huu umefanywa kwa manufaa yapi, sababu katika hali ya kawaida sio rahisi kupata sifuri kwa mwanafunzi yeyote katika mitihani ya namna hii.
Inasemekana shule zimeshataarifiwa, na mimi kama mzazi na mdau wa elimu, nimetembelea shule wanaposoma watoto wangu nikahakikishiwa jambo hili na nikaonyeshwa juhudi za waalimu kuwaanda watoto kwa mitihani hiyo itakayofanyika mwezi Septemba mwaka huu.
Inawezekana uamuzi huu una malengo yafuatayo:
Moja, kulidanganya taifa kuwa kiwango cha ujuzi wa Hisabati kinakua, mara matokeo yatakapotangazwa,
Mbili, kubana matumizi ya serikali inayofilisika kwa kupunguza muda wa usahihishaji wa mihihani hiyo,
Tatu, kutumia wasahihishaji wasio wataalam wa Hisabati, hiyo kama kuwasaidia kwa viposho waweze kujikimu
Vilevile kuna hatari kuwa wanafunzi wengi wasio na uwezo wa kusoma na kuandika watafaulu mitihani hiyo na kuingia sekondari.
Ndugu, kama inawezekana kuzuia upuuzi huu usio na manufaa, tushauriane na tuweze kuuzuia maana ni hatari kwa mustakabali wa taifa linalochipuka.
Nawasilisha
[/LIST]
Inasemekana kuwa serikali kupitia Wwizara yake ya Elimu, imeamua kuwa mtihani wa Hisabati darasa la saba mwaka huu utakuwa na maswali yote ya kuchagua (multiple-choice questions). Haiingii akilini uamuzi huu umefanywa kwa manufaa yapi, sababu katika hali ya kawaida sio rahisi kupata sifuri kwa mwanafunzi yeyote katika mitihani ya namna hii.
Inasemekana shule zimeshataarifiwa, na mimi kama mzazi na mdau wa elimu, nimetembelea shule wanaposoma watoto wangu nikahakikishiwa jambo hili na nikaonyeshwa juhudi za waalimu kuwaanda watoto kwa mitihani hiyo itakayofanyika mwezi Septemba mwaka huu.
Inawezekana uamuzi huu una malengo yafuatayo:
Moja, kulidanganya taifa kuwa kiwango cha ujuzi wa Hisabati kinakua, mara matokeo yatakapotangazwa,
Mbili, kubana matumizi ya serikali inayofilisika kwa kupunguza muda wa usahihishaji wa mihihani hiyo,
Tatu, kutumia wasahihishaji wasio wataalam wa Hisabati, hiyo kama kuwasaidia kwa viposho waweze kujikimu
Vilevile kuna hatari kuwa wanafunzi wengi wasio na uwezo wa kusoma na kuandika watafaulu mitihani hiyo na kuingia sekondari.
Ndugu, kama inawezekana kuzuia upuuzi huu usio na manufaa, tushauriane na tuweze kuuzuia maana ni hatari kwa mustakabali wa taifa linalochipuka.
Nawasilisha
[/LIST]