Baija Bolobi
JF-Expert Member
- Feb 25, 2009
- 1,093
- 1,737
KINGUNGE NA KIKWETE: Tujikumbushe
Nilikuwa Dodoma mwaka 2005 wakati wa vikao vya kuteuamgombea urais kwa CCM.
Mzee Mkapa aliingia Dodoma saa saba mchana. Alipokelewa uwanjani katikati ya mvutano mkubwa wa wagombea. Dodoma ilikuwa inazizima nyuma ya Jakaya Kikwete.
Na Mzee Mkapa aliingia Dodoma akiwa amepania kulikata jina la Kikwete kwa kile alichodai, "Kijana huyu ana kiburi, anawezaje kudai akikatwa CCM itapasuka?". Mkapa alipania kulikata jina lake na kama CCM inapasuka ipasuke.
Alipoingia White House Dodoma aliendewa na wazee wakiongozwa na Mzee Kingunge. Bila kupepesa macho, Mzee Kingunge alimwambia Mzee Mkapa maneno mazito. Alisema, mgombea ni Jakaya. Aliongeza kuwa, Zamu kati ya Wazanzibari na Wabara haina shida tena, Wazanzibari wanamkubali Jakaya. Zamu za Wakristo na Waislamu; sasa ni zamu ya Waislamu na wamesema wanamtaka Jakaya.
Mzee Mkapa hakujibu. Aliondoka kwenda kupata taarifa za usalama na kamati ya maadili. Yaliyotokea baadaye wote mnakumbuka. Hotuba ya Mkapa ilibadilika. Aliokuwa ameishawaambia kuwa atakata jina la Jakaya walibaki midomo wazi. Wengine wakadai amerogwa. Wengine wakasema ametishwa, na mengine mengi.
Sasa nimwulize Nape Nnauye: Huyu Mzee Kingunge mwaka 2005 alipomuunga mkono mgombea mmoja, Jakaya, hakukigawa chama? Kumuunga mkono Lowassa ndipo amekigawa chama?
Uungwana ni kukubali ukweli kuwa kuondoka kwa mzee Kingunge ni pigo, kisha tuendelee na safari.
Nilikuwa Dodoma mwaka 2005 wakati wa vikao vya kuteuamgombea urais kwa CCM.
Mzee Mkapa aliingia Dodoma saa saba mchana. Alipokelewa uwanjani katikati ya mvutano mkubwa wa wagombea. Dodoma ilikuwa inazizima nyuma ya Jakaya Kikwete.
Na Mzee Mkapa aliingia Dodoma akiwa amepania kulikata jina la Kikwete kwa kile alichodai, "Kijana huyu ana kiburi, anawezaje kudai akikatwa CCM itapasuka?". Mkapa alipania kulikata jina lake na kama CCM inapasuka ipasuke.
Alipoingia White House Dodoma aliendewa na wazee wakiongozwa na Mzee Kingunge. Bila kupepesa macho, Mzee Kingunge alimwambia Mzee Mkapa maneno mazito. Alisema, mgombea ni Jakaya. Aliongeza kuwa, Zamu kati ya Wazanzibari na Wabara haina shida tena, Wazanzibari wanamkubali Jakaya. Zamu za Wakristo na Waislamu; sasa ni zamu ya Waislamu na wamesema wanamtaka Jakaya.
Mzee Mkapa hakujibu. Aliondoka kwenda kupata taarifa za usalama na kamati ya maadili. Yaliyotokea baadaye wote mnakumbuka. Hotuba ya Mkapa ilibadilika. Aliokuwa ameishawaambia kuwa atakata jina la Jakaya walibaki midomo wazi. Wengine wakadai amerogwa. Wengine wakasema ametishwa, na mengine mengi.
Sasa nimwulize Nape Nnauye: Huyu Mzee Kingunge mwaka 2005 alipomuunga mkono mgombea mmoja, Jakaya, hakukigawa chama? Kumuunga mkono Lowassa ndipo amekigawa chama?
Uungwana ni kukubali ukweli kuwa kuondoka kwa mzee Kingunge ni pigo, kisha tuendelee na safari.