Mugabe awabwatukia wazungu

Mugabe awabwatukia wazungu

Hawa ndio simba wa afrika;
Nkrumah
Mugabe
Nyerere na wengneo wenye ubavu kama hao
 
Mugabe ndiyo Simba wa afrika, aliyozungumza ni ukweli MTU, ingawa wapigania haki kama vile Bob Marley alishazungumza sana, kuhusu wakina Obama, aliwaita kwa jina la TOP RANKIN ambao wanatumia kimvuli cha demokrasia Kuua viongozi with R.I.P Gadaffi. Hawa mababylon wanapenda kutuona waafrika tukiwa kwenye hali gumu, tukiuana wenyewe kwa wenyewe. Big up Mugabe, ukweli Mugabe anapotoa hutuba yake wazungu wanachukia sana na kutoka nje ya ukumbi, sababu anazungumza ukweli na ukweli unauma.
 
Kwahiyo Zimbabwe nzima hayo anajua yeye tu. Wasomi woote wale haamini hata mmoja!
 
Mugabe bhana.."until God says come to join the other angels"

Hii point ya NGOs ina mantiki kubwa sana .. Serikali zetu ziwe macho... So kila NGO inajileta tu na mambo yake... Kwenye paper za registration wanaonesha malengo A, kwenye real practice wanafanya B.

Kuna lecturer mmoja pale Udsm amekulia US anazichukia NGOs na huziita 'Nothing Going On'... Nlijiuliza sana kwanini... Kugundua NGOs zinechangia sana kubadilisha sociocultural structure ya hii nchi... probably sisi wa hapa hapa tunafumbia macho NGOs, ila ni muda... tuamke.

Mwalimu wako yuko sahihi kabisa, NGO zote zinahitaji uchunguzi mkubwa mno nyingi zinachukua pesa hapa kupelekwa kwa za Kimarekani nouma zaidi. Yaani wametumwa pesa hapa ukisikia MCC imeleta USD 500M ujue nusu inarudi kwao direct inayobaki tunagawana nao 50/50 mara NICRa, wataalam na usishangae fundi bomba US hapa anakuwa Country Director atalipwa mshahara kuanzia spouse mpaka house girl wake. Hizo shule ulizosikoa wanalipa mtoto wa vidudu USD 30,000 kwa mwaka ujue zaidi ya 70% zinalipwa na NGO, kama JPM atakuwa mtundu anaweza fyeka na hiki kichaka ila kina vibaraka hatare. Wanaharakati wanavuta huu mtonyo pia,
 
Hotuba ya Mugabe ni nzuri kwa upande mmoja, upande wa pili ni sisi wa Afrika kubaguana na kuchukiana mno kisiasa! Kunyimana haki wenyewe kwa wenyewe hata pale inapoonekana dhahiri! Tukiachwa wenyewe hatutakuwa salama hata kidogo! Haki za binadamu zitakiukwa kusiko mfano! Wanyonge watanyanyasika mara kumi zaidi na vyama dola vitayateka mataifa mengi!

Wa Afrika tunahitaji usimamizi kuliko ilivyo hivi sasa! Tukiachwa wenyewe kwa wenyewe hatutakuwa mahala salama! Hatujaweza bado kujiongoza wenyewe! Hivyo kwa hakika hatutaweza kuongoza wengine!
Africans unite
 
Mugabe ndiyo Simba wa afrika, aliyozungumza ni ukweli MTU, ingawa wapigania haki kama vile Bob Marley alishazungumza sana, kuhusu wakina Obama, aliwaita kwa jina la TOP RANKIN ambao wanatumia kimvuli cha demokrasia Kuua viongozi with R.I.P Gadaffi. Hawa mababylon wanapenda kutuona waafrika tukiwa kwenye hali gumu, tukiuana wenyewe kwa wenyewe. Big up Mugabe, ukweli Mugabe anapotoa hutuba yake wazungu wanachukia sana na kutoka nje ya ukumbi, sababu anazungumza ukweli na ukweli unauma.
 
makao makuu ya umoja wa mataifa yatahamishiwa Iraq
 
HHakuna cha Simba wa Afrika wala nini hapo,msipowajua viongozi wa Afrika walivyo mtaendelea kuchezewa akili mpaka basi.Mugabe hana jipya analolifanya ktk taifa lake la Zimbabwe, maisha ya Zimbabweans ni duni mno,maelfu ya Zimbabweans wanakimbilia nchi za jirani kutafuta maisha mazuri hasa South Africa na Namibia.
Mugabe anahubiri kuhusu ubaguzi tunaofanyiwa na Wazungu,ni kweli Wazungu ni wabaguzi lkn hata sisi Waafrika wenyewe kwa wenyewe tunabaguana,tawala nyingi za nchi za Africa zimetawaliwa na ukabila zaidi,hata pale Zimbabwe sehemu kubwa ya watawala ni wa kutoka kabila flani.Wandebele na Washona hawaivi kule Zimbabwe.
Anazungumzia kuhusu haki sawa ktk baraza la usalama la UN,ni wazo zuri sana na nakubaliana nalo lkn mbona ndani ya nchi yake ya Zimbabwe Mugabe hawaoni Zimbabweans wengine kama ni watu wenye haki ya kuiongoza Zimbabwe isipokuwa yeye tu?Yaani Ameshajiona kama ni mtu ambaye amezaliwa tayari akiwa na haki ya kuitawala Zimbabwe .Unajua unapomnyoonyeshea mwenzako kidole kumbuka kwamba kuna vidole vingine vinakunyooshea wewe mwenyewe.
Nawashauri viongozi wa Africa waache kufanya siasa za maigizo badala yake watumie muda wao vizuri ktk kuboresha maisha ya wananchi wao.Shujaa kwangu ni yule anayefanya maisha ya wananchi wake kuwa mazuri kiasi,na ktk eneo hili marehemu Gaddafi alifanikiwa sana,huyu ndio Simba wa Africa sasa, achana na hao wengine wanaopiga blah blah blah ili mradi siku ziende.Ndio maana rais Magufuli aliupuuza huo mkutano.
 
Back
Top Bottom