Sajenti
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 3,651
- 412
Kuna taarifa kuwa serikali ya Zimbabwe imemfukuza balozi wa Libya nchini humo kutokana na kitendo cha balozi huyo kuamua kupandisha bendera ya waasi. Kitendo cha balozi huyo kupandisha bendera ya waasi kimemkasirisha Raisi Mugabe ambaye ni swahiba mkubwa Kanali Qadaffi. Balozi huyo amepewa saa 72 kuondoka nchini humo pamoja na maofisa wote wa ubalozi. Source: BBC.