OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 49,080
- 103,312
Katavi. Waumini wa dini ya Kiislamu mkoani Katavi wametakiwa kuacha tabia ya kupigana majungu kuchafuana wao kwa wao badala yake washirikiane kwa pamoja kudumisha mshikamano, umoja na upendo.
Hayo yamesemwa leo Oktoba 5 na Mufti Mkuu wa Tanzania, Shekhe Abubakar Bin Zuberi amebainisha hayo leo Jumatatu Oktoba 05, 2021 akiwa ziarani mkoani Katavi wakati akihutubia umati wa waislaamu kwenye Msikiti wa Ijumaa uliopo Manispaa ya Mpanda.
“Hatuwezi kupata maendeleo yeyote tusipokuwa na umoja pamoja na mshikamano. Uupweke ni adhabu ukiwa peke yako tu hushirikiani na wenzako, utakosa mambo mengi ambayo ungeyapata kwa wengine,” amesema Mufti.
“Kwahiyo tusijengeane chuki tuambiane kuna jambo halijakaa vizuri lieleze vizuri usikae kando kando kusema sema kwenye vijiwe. Musilaamu hazungumzi kandokando anazungumza waziwazi au moja kwa moja,” amesema Mufti.
Akiwa mkoani Katavi amezindua mradi wa ujenzi wa ofisi ya Bakwata, Mkoa uliogharimu zaidi ya Sh25 milioni zilizotokana na sadaka za waumini, michango ya wadau na serikali.
Pia ametembelea mradi wa ujenzi wa ofisi ya Bakwata Wilaya ya Mpanda, shule ya msingi iliyopo msikiti wa Kasimba pamoja na shamba la korosho lilipo Kakese.
Hayo yamesemwa leo Oktoba 5 na Mufti Mkuu wa Tanzania, Shekhe Abubakar Bin Zuberi amebainisha hayo leo Jumatatu Oktoba 05, 2021 akiwa ziarani mkoani Katavi wakati akihutubia umati wa waislaamu kwenye Msikiti wa Ijumaa uliopo Manispaa ya Mpanda.
“Hatuwezi kupata maendeleo yeyote tusipokuwa na umoja pamoja na mshikamano. Uupweke ni adhabu ukiwa peke yako tu hushirikiani na wenzako, utakosa mambo mengi ambayo ungeyapata kwa wengine,” amesema Mufti.
“Kwahiyo tusijengeane chuki tuambiane kuna jambo halijakaa vizuri lieleze vizuri usikae kando kando kusema sema kwenye vijiwe. Musilaamu hazungumzi kandokando anazungumza waziwazi au moja kwa moja,” amesema Mufti.
Akiwa mkoani Katavi amezindua mradi wa ujenzi wa ofisi ya Bakwata, Mkoa uliogharimu zaidi ya Sh25 milioni zilizotokana na sadaka za waumini, michango ya wadau na serikali.
Pia ametembelea mradi wa ujenzi wa ofisi ya Bakwata Wilaya ya Mpanda, shule ya msingi iliyopo msikiti wa Kasimba pamoja na shamba la korosho lilipo Kakese.