ROBINSON NAZARETH
Member
- Oct 14, 2015
- 6
- 0
Binadamu wote ni sawa kwa maana nyingi. Usawa mmoja wapo ni kiasi cha muda ambacho kila mmoja wetu anacho.
Kila binadamu anayo masaa ishirini na mane kwa siku. Masaa yaliyotimia yenye dakika sitini.
Kinacholeta tofauti, ni namna tunavyoyatumia masaa haya kwa faida. Kile tunachofanya katika kila 'lisaa' linalopita mikononi mwetu.
Wakati wapo wanaoweza kupangilia mgawanyo wa muda kwa siku inayofuata, na kutathimini adabu waliyo nayo kwa kile walichopanga, wengi tunajikuta tunafanya yale tusiyoyapanga na hivyo hatuna namna ya kutathmini matendo yetu ya siku.
Watumiaji wazuri wa muda wanao uwezo mzuri wa kusema 'hapana sikupanga hili' wakati watumiwaji wa muda hawana uwezo huo.
Ninaposhindwa kusema hapana mahala ambapo nilipaswa kufanya hivyo, ni namna bora zaidi ya kuteketeza muda.
Ikiwa tutaweza kudhibiti matumizi ya muda, tutakuwa tumeweza kuyadhibiti maisha yetu.
Kila binadamu anayo masaa ishirini na mane kwa siku. Masaa yaliyotimia yenye dakika sitini.
Kinacholeta tofauti, ni namna tunavyoyatumia masaa haya kwa faida. Kile tunachofanya katika kila 'lisaa' linalopita mikononi mwetu.
Wakati wapo wanaoweza kupangilia mgawanyo wa muda kwa siku inayofuata, na kutathimini adabu waliyo nayo kwa kile walichopanga, wengi tunajikuta tunafanya yale tusiyoyapanga na hivyo hatuna namna ya kutathmini matendo yetu ya siku.
Watumiaji wazuri wa muda wanao uwezo mzuri wa kusema 'hapana sikupanga hili' wakati watumiwaji wa muda hawana uwezo huo.
Ninaposhindwa kusema hapana mahala ambapo nilipaswa kufanya hivyo, ni namna bora zaidi ya kuteketeza muda.
Ikiwa tutaweza kudhibiti matumizi ya muda, tutakuwa tumeweza kuyadhibiti maisha yetu.