Muda wa kuiponya nchi yetu ni sasa

Muda wa kuiponya nchi yetu ni sasa

Mabibi na mabwana,

Mtanzania mwenzetu aliyeondoka akiwa "mfu", hatimaye amerejea leo salama salimini nyumbani Tanzania.

Jambo la heshima kubwa sana kwetu sisi sote ambao ni wana halisi wa nchi hii na wazalendo.

Tumeshinda!

Tumeshinda sote tuliofanikisha kurejea kwa mwana huyu wa nchi hii salama na kwa amani. Tafsiri halisi ya kuwa sote tu wajenzi wa nyumba moja. Yaani Tanzania.

Kesho inshallah kwa umoja wetu tena, kama Watanzania na tukamuage kwa pamoja Mzee wetu Rais mstaafu Mkapa (RIP) pale Uhuru, ambaye hakubahatika hata kumwona mwana huyu akirejea nyumbani.

Yaliyopita si ndwele, baada ya mazishi tujipange kuganga yajayo.

Kwako mheshimiwa rais wetu: kwa hakika haupo muda mzuri wa maridhiano na kuponya nchi hii kuliko huu.

Sentensi yako moja tu mkuu, itaifanya Tanzania yote akiwamo Mh. Lissu kuripuka kwa vifijo na vigeregere vya:

"Magufuli tosha!"

Kuyatambua madhila aliyoyapitia mja wake mola huyu, kumkaribisha nyumbani na neno moja la "pole" tu, linabeba uchawi wote unaohitajika.

Eeh mola wetu, hebu ukatujalie kuweza kuyaona yasiyoonekana na hasa kuudhihirisha ushindi wetu huu kwa wote wale wasioitakia mema nchi yetu.

Mungu ibariki Tanzania.
Huwa napenda wachangiaji wenye michango chanya na wewe ni mmojawapo. Hongera!
 
Chige ana hoja. Hatujui, pengine Magu kapigwa mkwara na mabeberu? Kwamba kama walioandamana leo wangesambaratishwa kama polisi walivyoahidi, mabeberu wageondoa jina la Tanzania kwenye orodha ya nchi za uchumi wa kati? Imajini hiyo tu ingemuacha wapi Magu?
Lakini pengine waliogopa kuaibika, wageni wengi sasa wanakuja hapa nchini sbb ya msiba.

Yote hayo mkuu hayamsimamishi kwa jahiri aliyekubuhu kufanya yake. Waulize pana vi nchi hapo magharibi yetu.

Kupongeza tunapofanya maendeleo, ni strategy nzuri ya mapambano.

Yasijekuwa yale ya Katiba mpya. Kidogo kidogo hujaza kibaba na Pole pole ndiyo mwendo.
 
Tutangulize nia njema.

Mtanzania mwenzetu karejea kwa amani bila kubugudhiwa, hilo la heri.

Tuupe muda. Tumzike mzee wetu kisha tupange yajayo.

Yaliyopita si ndwele. Tuweke bunduki zetu chini tujenge nchi.

Wanasema ndugu wawili wakigombana chukua jembe ukalime. Siku wakipatana chukua kapu ukavune.

Tuchukue makapu kuvuna, nchi ipone.

Mungu ni muweza wa yote. Hili mbona siyo Corona?

Hili ni utashi tu ambao uko mikononi mwetu?

Yakiwezejana, mbona "Magufuli tosha!"
Awali ya yote, hakutakiwa kabisa kubughudhiwa na kwahiyo kilichotokea sio favor!! Na kwa upande mwingine, hapo hakuna suala la nia njema hapo, kwa sababu hiyo nia mbaya, haitakiwi kuwepo kwa sababu zozote zile!!

Lakini kubwa zaidi, it's too soon tu assume kwamba eti jamaa wamebadilika au kujirudi kwa sababu mazingira yenyewe yaliyopo, ni wapumbavu tu ndie wangefanya move yoyote against TL!

Na kama nilivyosema, I'm certain hata international media zilikuwa zinafuatialia kurejea kwa TL ili kuangalia endapo atapita salama pale airoport!! Any attempt to TL, ingekuwa na international coverage kubwa sana within a short time... utawala walilijua hilo!!!

Mathalani in the next few days ikitolewa hati ya kukamatwa kwake, coverage yake itakuwa tofauti sana na endapo wangefanya hivyo pale airport, wakati iwe amekamatwa airport au baadae, bado ni kitu kile kile kwa upande wa wapenda demokrasia lakini huku ikiwa ni nafuu kwa watawala kufikia lengo lile lile lakini bila mayowe!!

Na kwa upande mwingine, they're not that stupid to wash their dirty linen in public!!

Itoshe tu kusema kwamba, "it's too soon to say it's finally over, they've changed"!
 
Tutangulize nia njema.

Mtanzania mwenzetu karejea kwa amani bila kubugudhiwa, hilo la heri.

Tuupe muda. Tumzike mzee wetu kisha tupange yajayo.

Yaliyopita si ndwele. Tuweke bunduki zetu chini tujenge nchi.

Wanasema ndugu wawili wakigombana chukua jembe ukalime. Siku wakipatana chukua kapu ukavune.

Tuchukue makapu kuvuna, nchi ipone.

Mungu ni muweza wa yote. Hili mbona siyo Corona?

Hili ni utashi tu ambao uko mikononi mwetu?

Yakiwezejana, mbona "Magufuli tosha!"
Kwanini isiwe TL tosha?
 
Awali ya yote, hakutakiwa kabisa kubughudhiwa na kwahiyo kilichotokea sio favor!! Na kwa upande mwingine, hapo hakuna suala la nia njema hapo, kwa sababu hiyo nia mbaya, haitakiwi kuwepo kwa sababu zozote zile!!

Lakini kubwa zaidi, it's too soon tu assume kwamba eti jamaa wamebadilika au kujirudi kwa sababu mazingira yenyewe yaliyopo, ni wapumbavu tu ndie wangefanya move yoyote against TL!

Na kama nilivyosema, I'm certain hata international media zilikuwa zinafuatialia kurejea kwa TL ili kuangalia endapo atapita salama pale airoport!! Any attempt to TL, ingekuwa na international coverage kubwa sana within a short time... utawala walilijua hilo!!!

Mathalani in the next few days ikitolewa hati ya kukamatwa kwake, coverage yake itakuwa tofauti sana na endapo wangefanya hivyo pale airport, wakati iwe amekamatwa airport au baadae, bado ni kitu kile kile kwa upande wa wapenda demokrasia lakini huku ikiwa ni nafuu kwa watawala kufikia lengo lile lile lakini bila mayowe!!

Na kwa upande mwingine, they're not that stupid to wash their dirty linen in public!!

Itoshe tu kusema kwamba, "it's too soon to say it's finally over, they've changed"!



Mkuu, angalia hii comment #419:

IMG_20200727_225709_501.jpg


Comment #419 kwenye uzi huu:

Kwa mliomsikia Tundu Lissu kwenye Hard Talk, unadhani atarejea nchini? Mimi sina hakika na akirejea, atakuwa ni shujaa kuliko hata Nelson Mandela!

Makamanda, vita (mapambano) ni strategy. Strategy ya mapambano ni pamoja na kutokumwaga mchele kwenye kuku wengi.

Kufahamu nini unataka namna gani ukipate ndiyo busara yenyewe.

Tunaweza kuganga yajayo katika namna ambayo ni muafaka zaidi kwa usalama na amani ya kila mtu huku tukiwapongeza na hata kuwashukuru watesi wetu inapobidi.

Wapumzike kwa amani kina Mao, Che, Castro na washupavu wengine.
 
Tutangulize nia njema.

Mtanzania mwenzetu karejea kwa amani bila kubugudhiwa, hilo la heri.

Tuupe muda. Tumzike mzee wetu kisha tupange yajayo.

Yaliyopita si ndwele. Tuweke bunduki zetu chini tujenge nchi.

Wanasema ndugu wawili wakigombana chukua jembe ukalime. Siku wakipatana chukua kapu ukavune.

Tuchukue makapu kuvuna, nchi ipone.

Mungu ni muweza wa yote. Hili mbona siyo Corona?

Hili ni utashi tu ambao uko mikononi mwetu?

Yakiwezejana, mbona "Magufuli tosha!"

Halima amefanya vyema leo kulipongeza jeshi la polisi, si vibaya chama kikatoa shukran rasmi kwa jeshi la polisi, hata kama ni kwa kinafiki. Pia nashauri sana Tundu Lisu ashauriwe kutokwenda kesho msibani. Kwangu bado Lisu ana hasira na lile shambulio, kwa vyovyote atataka kuionyesha serikali na hasa rais Magufuli kuwa amepona. Na mashabiki wake wanaweza kuonyesha furaha iliyopitiliza ambayo itaipa serekali kuchukua maamuzi hasi.

Kwakuwa wamemstahi leo, ni vyema angeachana na huo msiba, kuna nafasi kubwa ya kushindana na ccm. Na kama itawezekana kuanzia sasa Lisu pia ashauriwe asitumie lugha kali za kupandisha hamasa za chuki, bali apambane na ccm kwa sera. Kuna sehemu nyingi sana za kuwazidi ccm, mfano hii rushwa ya juzi kwenye chaguzi zao, ajira, ugumu wa maisha wa wananchi, demokrasia nk. Ni vyema apange vizuri mashambulizi yake kisiasa, kuliko kuonekana anambana na mtu binafsi, kwa ajili ya shambulizi lake binafsi
 
Halima amefanya vyema leo kulipongeza jeshi la polisi, si vibaya chama kikatoa shukran rasmi kwa jeshi la polisi, hata kama ni kwa kinafiki. Pia nashauri sana Tundu Lisu ashauriwe kutokwenda kesho msibani. Kwangu bado Lisu ana hasira na lile shambulio, kwa vyovyote atataka kuionyesha serikali na hasa rais Magufuli kuwa amepona. Na mashabiki wake wanaweza kuonyesha furaha iliyopitiliza ambayo itaipa serekali kuchukua maamuzi hasi.

Kwakuwa wamemstahi leo, ni vyema angeachana na huo msiba, kuna nafasi kubwa ya kushindana na ccm. Na kama itawezekana kuanzia sasa Lisu pia ashauriwe asitumie lugha kali za kupandisha hamasa za chuki, bali apambane na ccm kwa sera. Kuna sehemu nyingi sana za kuwazidi ccm, mfano hii rushwa ya juzi kwenye chaguzi zao, ajira, ugumu wa maisha wa wananchi, demokrasia nk. Ni vyema apange vizuri mashambulizi yake kisiasa, kuliko kuonekana anambana na mtu binafsi, kwa ajili ya shambulizi lake binafsi

Mkuu nakubaliana nawe kwa kiasi kikubwa. Hapana haja ya jazba makamanda.

Ila kesho twende msibani. Twende na Lissu msibani akiweza. Twende kuhani. Ule msiba ni wetu sote.

Tukatoe heshima zetu kwa mzee Mkapa na tukaionyeshe nia njema kwa kuepuka vitendo vyovyote hata kama watakuwapo wasioitakia mema nchi yetu au provocation ya aina yoyote. Hiyo ndiyo maturity wakuu.

Msibani hakuna mwenyewe. Ndiyo uswahili wetu huo tulio barikiwa nao.

Hata hivyo na kwa namna yoyote usalama wa maisha ya Lissu linapaswa kuwa ni kipaumbele haswa na kwa muda wote.
 
Mmh! Sijui kama anaweza kutoa pole. Huyu jamaa siyo mpatanishi by nature, bali ni mpenda shari na visasi. Akitoa pole jua litakoma kuchomoza.

Tusiifunge milango wakuu (ila usitake ncheke). Tanzania ni kubwa kuliko mtu au kikundi cha watu.

Kukiri upungufu mbona ni kitendo cha kiungwana tu. Siyo unyonge.

Kwa mswahili inamgharimu nini kusema "pole."

Tuwe na matumaini.

Obama anasema "the audacity of hope."

Kwa kweli pana mwanga mwisho wa pango.
 
Ngojeni tumalize msiba jamani, camera za dunia zote zimegeukia huku 🤣🤣🤣
 
Chige ana hoja. Hatujui, pengine Magu kapigwa mkwara na mabeberu? Kwamba kama walioandamana leo wangesambaratishwa kama polisi walivyoahidi, mabeberu wageondoa jina la Tanzania kwenye orodha ya nchi za uchumi wa kati? Imajini hiyo tu ingemuacha wapi Magu?
Lakini pengine waliogopa kuaibika, wageni wengi sasa wanakuja hapa nchini sbb ya msiba.
Aisee Kuna logic Fulani hivi.
 
Kabisa huu ni mwanzo mzuri sana kwa siasa za ukombozi za nchi yetu, sikuamini macho yangu kwa namna watanzania walivyojitokeza kumpokea shujaa Lissu. Ni pigo kubwa mno kwa waliokuwa na nia ya kumuua.
Shetani ameshindwa Tena.
 
Mmh! Sijui kama anaweza kutoa pole. Huyu jamaa siyo mpatanishi by nature, bali ni mpenda shari na visasi. Akitoa pole jua litakoma kuchomoza.
Kwa aliyoyaona leo sijui kama keshi Msibani ataenda.
 
Yaani hivi sasa anashaurika kwavile Mkapa hatunae?! Man, you can't be serious!!! Magu isn't that stupid to wash his dirt linen in public! Wait and see kama hujasikia imetolewa hati ya kukamatwa Tundu Lissu... sasa hilo likitokea sijui kutakuwa na tofauti gani na endapo angekamatwa leo, zaidi tu ya endapo wangefanya hivyo leo, ingewachafua sana wao wenyewe!

These people walishafahamu in advance kwamba hata international media zingekuwa zinafuatilia kurejea kwa TL to see what would happen!! Matokeo yake, ingekuwa ni breaking news ambayo ingesambaa kama moto wa kifua throughout the world!!
Kwani Magu anaogopa breaking News?? Jambo la kushukuru Mungu tu. Hapa ni Mkono Wa Rehema wa Yehova umetenda kazi.
 
Back
Top Bottom