Muafaka CCM na CUF, pande mbili za shilingi!

Kuna watu hawataki kuamini kuwa chama cha CUF kinaelekea ikulu kutokea upinzani. Silazima iwe kesho au keshokutwa, kwakuwa inaeleweka kuwa demokarasia ina mikondo mingi ya kupita mpaka kufikia ufukweni salama. Nikimkumbuka Abdulaye Wade alivyo suffer na PDS yake tokea mwaka 1974, wakati bado Leopard Sedar Senghor mwenyewa yu hai, Wade kawa mpinzani tokea siku zote hizo, na alishindwa katika chaguzi 4 katika kitu cha urais, mpaka kizazi kipya cha Wasenegal kinafumbua macho na kumuelewa(baada ya kufa au kupoteza dira kwa wahafidhina) mwaka 2000 ndo PDS ya Wade na Wade mwenyewe wanaingia ikulu.
Kwa hiyo kufikia mafanikio kuna taka mipango ya muda mfupi na muda mreefu kama PDS ya Wade na usatahamilivu wa kuwavumilia wananchi katika kipindi cha mpito kuelekea demokarasia ya kweli,ambacho wengine hawajaifahamu hada madhumuni yake na vyama vinavyotawala vinatumia hila na vitimbi kuchezea ridhaa na matakwa ya wananchi walioifahamu hiyo demokarasia ya uchaguzi na wananchi kubakia kimya wakiwaachia viongozi wao wa vyama vya siasa wapege kelele.
Ila kwa kumalizia, chama cha Mapinduzi kisitazamie kutawala nchi hii comfortably miaka yote, kama UNIP ya Kaunda kama KANU ya Moi n.k kuna siku kitapumzishwa na siku zenyewe zinaanza kusogea taratiiibu. time will tell.

Binafsi nilikuwa mmoja wa watu walioamini kwamba Lipumba angeunda serikali ya kitaifa mwaka 2000, na yeye mwenyewe alitangaza hadi Baraza lake la Mawaziri. Wakati huo CUF ilishirikiana na Chadema katika kampeni zake. Baada ya hapo na hasa baada ya matatizo ya CCM/CUF Zanzibar, na hadi mwaka 2005, CUF ikaanza kupoteza mwelekeo na walizidi kuingia katika mtego wa mwafaka wa CCM ambao ni mtego mbaya kama nilivyosema ndege mjanja hunaswa na tundu bovu.

Nimekatishwa tamaa zaidi na kuibuka kwa siri nyingi mbaya za ndani ya CUF ambazo kwa maslahi ya Taifa, si vyema kuzijadili humu jamvini. Kwa kifupi kama hakitabadilika na kugeuka nyuma na kuamua kukataa mambo laini na kufuata mambo magumu, CUF haitoshinda. Walio ndani wanajua, na wanajua nini maana yake.

Mwa maslahi ya Taifa, CUF lazima wabadilike. Warudi kwenye ile CUF yenye kujitegemea na kutegemea zaidi wapenzi wake wa ndani na nje ya nchi na si ilivyo sasa. Hata kama hapo awali (1995-2000) walikua hivi, sasa waache.
 
Nimekatishwa tamaa zaidi na kuibuka kwa siri nyingi mbaya za ndani ya CUF ambazo kwa maslahi ya Taifa, si vyema kuzijadili humu jamvini. Kwa kifupi kama hakitabadilika na kugeuka nyuma na kuamua kukataa mambo laini na kufuata mambo magumu, CUF haitoshinda. Walio ndani wanajua, na wanajua nini maana yake.

Mwa maslahi ya Taifa, CUF lazima wabadilike. Warudi kwenye ile CUF yenye kujitegemea na kutegemea zaidi wapenzi wake wa ndani na nje ya nchi na si ilivyo sasa. Hata kama hapo awali (1995-2000) walikua hivi, sasa waache.
Kweli kuna makosa yamefanyika pengine kwa makusudi ya kupata dhamira fulani au kwa bahati mbaya katika katika kusukuma misimamo na mikakati fulani fulani. Tukubali kuwa wanaongoza chama ni wanachama na viongozi wanasimamia, wote ni binaadamu wana mapungufu yao kama wengine, nakubaliana na ww kabisa kuwa kwa maslahi ya taifa na mageuzi ya kweli ya kidemokrasia hatua za makusudi zinapaswa zichukuliwe na viongozi na wanachama kurudi katika mstari.
 
wanaowabembeleza na kuwalipia hoteli na gharama nyingine, kiulainiii!!!! Ndege mjanja hunaswa na tundu bovu.

[/B] Mkuu Halisi..
siku nyingi una maneno kama haya,na niliwahi kujibu matamshi yako,the way ulivo na maneno yako ni tofauti kabisa.. tatizo lako na mafisadi limalize mwenyewe,sijui niseme ni miongoni mwa watu wanaotumiliwa na ccm kukipakazia Cuf kama walivofanya nyuma,walivokuwa wakipakazia ni chama cha udini,cha warabu na mengineo sasa unaleta propaganda nyengine..sawa mkuu wasaidie hao ccm,lkn huna ushahidi na unaloongea.. lkn kaka yangu siko unapokwenda,rudi kwa Mola wako...
 
Kusema mwafaka basi kumetokana na chenga kali ya mwili waliofanya CCM ya kutaka suala lipigiwe kura na wananchi. Hadi leo hii nyonga ya Profesa haijarudi sawasawa!
 
Hawa Jamaa wanakuja kukaa tena mwafaka baada ya uchaguzi 2010, tutaona kama kweli wameacha na kusema basi
 
Hawa Jamaa wanakuja kukaa tena mwafaka baada ya uchaguzi 2010, tutaona kama kweli wameacha na kusema basi
Huwezi kuwa jiwe kama jambo lenyewe linahusu maisha ya watu...Mandela alikaa na Washenzi makaburu baada ya kumtesa for over 25 years "kwanini CUF wasikae na CCM kama jambo lenyewe ni kwa faida ya nchi yetu kwa ujumla.
Kwa taarifa yako hata Chadema hawana ubavu wa kukataa kukaa na CCM in case scenario kama ile itatokea, so i see no harm kwa viongozi kuchukua maamuzi magumu kama walivyofanya CUF. Upinzani Tanzania una miaka 10-15 na chama cha CUF ndio kilichopata misukosuko haswa ya upinzani chadema subirini rafu 2010 ndio tuone busara zenu ...wewe tu comment zako baada biharamulo (kulazwa chini zinaashiria kukataa tamaa). Leadership during the crisis determines what type of leader you are wa shari au wa heri..I entirely support CUF leaders ilikuwa ni option sahihi lakini za mwezi arobaini wananchi wameshafahamu sasa kwamba CCM wanadanganya watawaunga mkono for any move unlike before!!!
 
Chama cha CUF ndio kilichopata misukosuko haswa ya upinzani ,chadema subirini rafu 2010 ndio tuone busara zenu ...wewe tu comment zako baada biharamulo (kulazwa chini zinaashiria kukataa tamaa). Leadership during the crisis determines what type of leader you are wa shari au wa heri..I entirely support CUF leaders ilikuwa ni option sahihi lakini za mwizi arobaini wananchi wameshafahamu sasa kwamba CCM wanadanganya watawaunga mkono for any move unlike before!!!
Yaani hapo umeua kabisa ,ile kashkashi ya kubadilishwa matokea Chadema wameanza kubwaga manyanga :D. Hapa nilisema siasa za Chadema na kulipua mabomu hazina mshiko ni siasa ambazo zina muda mfupi tu kama nyimbo za kivita.Chadema hawajasema hadi leo vipi watamuendeleza mwananchi zaidi ya kuwashika mashati na kuwavuta ukosi mafisadi ,hapa imeonesha jinsi Lipumba alivyomwaga sera za Chama na bado ,tunahitaji pigo la mwisho ambalo ni kuondoa kodi za kibabe. ZIpo na nitawasiliana na uongozi wa juu wa CUF kuziwakilisha kodi hizi ziwe katika agenda ya sera za uchaguzi.
 
Mwiba,Tumain yaani hivo vitu si mchezo.. mwenye macho haambiwi tizama,ila tambueni tu kuwa ccm inaandaa mikakati mizito tena sana ikishirikiana na baadhi ya vyama vya upinzani ili kuimaliza Cuf,sasa waheshimiwa fikisheni ujumbe juu huko,hakuna kulala,tusije tukapigwa bao na safari hii,tumechoka na ccm wazeee...
 
[/I][/B] Mkuu Halisi..
siku nyingi una maneno kama haya,na niliwahi kujibu matamshi yako,the way ulivo na maneno yako ni tofauti kabisa.. tatizo lako na mafisadi limalize mwenyewe,sijui niseme ni miongoni mwa watu wanaotumiliwa na ccm kukipakazia Cuf kama walivofanya nyuma,walivokuwa wakipakazia ni chama cha udini,cha warabu na mengineo sasa unaleta propaganda nyengine..sawa mkuu wasaidie hao ccm,lkn huna ushahidi na unaloongea.. lkn kaka yangu siko unapokwenda,rudi kwa Mola wako...

Siwezi na sijawahi kutumiwa na chama chochote cha siasa ikiwamo hiyo CCM. Nafahamu unajua hata CUF haijawahi kunitumia na hata pale nilipofanya kazi za CUF, CCM, Chedema, NCCR-Mageuzi, TLP, TADEA, nilifanya hivyo ikiwa ni sehemu ya majukumu yangu ya kawaida. Hivyo ndivyo ilivyo JF. Hoja za msingi ni kwa CUF kusafisha hizo kelele kuhusiana na matatizo ya ndani ambayo si vyema yakatumika kukichafua. Najua maneno ya ufadhili yamekera lakini nimegusia nikijua mulio ndani mutaelewa na kusafisha hizo tuhuma ikiwa ni pamoja na zile za mpakani.

Kimsingi CUF ikijipanga inaweza lakini ijiepushe sana na watu wanaojifanya kuwa ni wema kwao, hasa wale wenye mikono michafu na umekiri mwenyewe kwa kusema, "tatizo lako na mafisadi limalize mwenyewe", pamoja na kufumba kwako, najua umelenga nini na hii inanitia faraja kwamba umenielewa. Bila kusema hatuwezi kujirekebisha na bila CUF yenye nguvu hakutakuwa na mageuzi ya kweli katika nchi hii. CCM imekuwa makini sana kupenyeza agenda za kuua nguvu za upinzani. Wametumia mbinu za kubeba ajenda ya ufisadi ya kina Dk SLaa na Hamad Rashid, wameibua hoja ya kujifanya Bunge la wabunge wengi wa CCM lina nguvu, yote ni kupoteza mwelekeo kabla ya 2010 na kuwanyang'anya hoja wapinzani. Huko Zanzibar nako wameibuka na kubeba hoja ya mafuta ambayo Maalim Seif amekuwa akiimba miaka yote, leo imekuwa hoja ya Karume na shemeji yake Mansoor na CUF wanashangilia. Lazima muamke.

Kama ulivyosema "mafisadi ni tatizo langu" ikiwa na maana ya kuwa halikuhusu, narudi tena kwenye hoja yangu ya pili kwamba CUF isipopima upepo unavyokwenda itaendelea kupoteza mwelekeo na labda iwekeze kuelekea 2015 ama 2020 na si 2010.

Kumbukeni niliyowahi kusema kuhusu "Operesheni ZInduka ya CUF" kuhusiana na jinsi watakavyoipeleka. Wameanza vyema na sasa tumeona Lipumba ameanza kumsafisha Lowassa kama ambavyo aliwahi kumtetea Rostam. Inawezekana isionekane hivyo lakini kwa kusema kwamba uamuzi wa Richmond ni wa Baraza la Mawaziri lote chini ya Kikwete ambaye naye aliridhi, ina maana sasa Lowassa alionewa> Hata kama ni kweli (jambo ambalo siamini) kisiasa si CUF wa kuliweka hilo. Wangejiepusha nalo. Itachukua muda (si 2010) kwa wananchi (wapiga kura) kuwaelewa CUF kwa kuibua suala la Richmond kwa staili yao. TAFAKARI
 
Back
Top Bottom