Mtwara Tunagombania Kivuli..

Tatizo la Mtwara ni ushirikishwaji hafifu na bora uongozi na si uongozi bora .

Kazi kubwa ya kiongozi ni kuwaelimisha anaowaongoza.Ikiwa kiongozi hanakosa sifa ya kuongoza kwa maana ya kuelimisha na kushrikisha anaowaongoza basi huyo hawezi kuitwa kiongozi ni lazima tumtafutie jina lingine linaloendana na matendo yake.

Kwa muda mrefu sasa labda miaka ishirini hizi Tanzania imekuwa dampo la viongozi wasiokuwa na sifa za uongozi,lakini wenye kulazimisha kuitwa viongozi hata kama ni kwa kutumia nguvu za vyombo vya dola kama jeshi la polisi na UWT.Tatizo la viongozi wasiokuwa na sifa za uongozi lipo hata katika vyama vya upinzani.Mfano unakuta kiongozi wa upinzani anajipachika sifa ya ugombea Urais wa kudumu hata kama sifa za kugombea nafasi hiyo zinazidi kuporomoka siku hadi siku.Utashangaa zaidi unakumbana na waziri mzima anafunga safari za mikoani badala ya kuondoa kero za wananchi anaziongeza.

Gesi ya Mtwara na Lindi ni mali ya waTanzania wote.Dhahabu ya Geita ni mali ya waTanzania wote,Tanzanite ya Mererani ni mali ya waTanzania wote,Mlima Kilimanjaro,Hifadhi za wanyama za Serengeti,Manyara,Mikumi,Saadani,Ngorongoro na nk ni mali za waTanzania wote bila kujali unaishi karibu na hifadhi hizo au mbali kiasi gani.Binafsi naishi Arusha lakini utashagaa tatizo la mpaka la ziwa Nyasa linanigusa sana kiasi ikitokea meza ya mazungumzo imeshindikana niko tayari kuitumikia nchi yangu hata ikibidi kwa kumwaga damu.

Tatizo linalotukabili waTanzania wengi sasa ni ukosefu wa uzalendo hasa upande wa uongozi.Wananchi wamekosa imani na uongozi/utawala kwasababu ya ubinafsi.Mikataba ya madini ni kielelezo namna watawala wetu walivyo walafi.Hata hili suala la gesi yamkini watawala wetu wameshaingia mikataba ya hovyo ndiyo maana tunaoana walivyotayari kutumia nguvu nyingi pasipo maelezo na pasipo ushirikiswaji.


Gesi ya Mtwara na Lindi ni mali ya waTanzania wote.Watawala tunahitaji mikataba iliyo ya uwazi na yenye kumnufaisha mTanzania.

Mungi ibariki Tanzania.
 
Lini watu wa Mtwara walisema gesi ni yao tuu? Upotoshaji huu ndio unaoamsha hasira kwao. Maana kwa makusudi mazima serikali (baadhi ya viongozi) wanapandikiza hilo kwa malengo yao na watu wa Mtwara wameshalielewa.
SULUHISHO; Ushauri wa kambi ya upinzani kuhusu kukaa pamoja na wadau wote na kujadili ndio suluhisho pekee.
 
Mimi labda sijaelewa kwani wanamtwara mamesema gesi ni yao....inasikitisha kuona mwandishi mkubwa kama wewe unapotosha...wanamtwara hawajasema gesi ni yao peke yao...ila wanachotaka kujua wao watanufaika vipi na gesi au watakua wanaona bomba la gesi tu linapita bila manufaa kwao..?Ikizingatiwa lile ni eneo mojawapolenye umaskini mkubwa tanzania....NARUDIA TENA TUACHE KUPOTOSHA WANAMTWARA HAWAJASEMA GESI IWE YAO PEKE YAO na kuileta DSM haimaanishi gesi ndo itakuwa ya watanzania wote...
 

'.........
Neno La Leo: Mtwara Tunagombania Kivuli....'

Kejeli kama hizo hapo kwenye kichwa cha habari, ndio zinazoamsha hasira za wana-Mtwara.
Juzi juzi waziri wa nishati aliwaita wana-Mtwara kuwa ni chura..!!
Kwa nini ?? kwa sababu wanapigania haki yao ya kufaidika na gesi inayochimbwa huko Mtwara..!!

Ulichoandika hapo kwenye blue, ni uwongo mkubwa wa shetani...
Wana-Mtwara hawajawahi hata siku moja kusema kuwa gesi ni yao peke yao..!!
Wanachotaka ni kufaidika na gesi hiyo inayochimbwa Mtwara.

Wewe mleta mada maggid unashiriki kwenye udhalimu wa serikali..!!
Sera ya CCM inasema kuwa raslimali za nchi ziongezewe thamani pale pale zinapozalishwa..!!
Sasa kwa nini gesi isiongezewe thamani kule Mtwara..??
Mleta mada upo hapo ..??

Mleta mada unaandika kama vile wewe ni msemaji wa serikali..!!
Unawaponda wana-Mtwara kuwa wanapigana na kivuli..!!

Kwako wewe mtu kudai haki ya maendeleo ni kupigana na kivuli..!!
Kwako wewe mleta mada, mikataba mibovu ya gesi ni bora kuliko haki ya wana-Mtwara..!!

Umelaaniwa wewe mleta mada maggid pamoja na wale wote wanaoendeleza udhalimu dhadi ya wana-Mtwara.
Mungu ibariki Tanzania.
 
Mu Israel,
Asante,
Lakini nawe unashiriki kupotosha kwa nia ovu kile nilichokiandika kwa nia njema. Inasikitisha.
Maggid

 
Embu tuzungumze ukweli gesi ni ya wana mtwara. Ni mali yao kwakuwa wamezaliwa na kukulia hapo kwenye ardhi ambayo ni yao lakini kwakuwa sisi ni jamhuri na ni nchi moja ni lazima mali za taifa zitumike katika maslahi ya pamoja. Kitu cha msingi hapa ni kwa serikali kuacha percent Fulani kwaajili ya maendeleo ya mtwara. Watu wa mtwara wamejifunza kutoka SHINYANGA, MWADUI na sehemu nyingine rasilimali zinapochimbwa. Kusema gesi si ya wana MTWARA ni uvivu wa kufikiri wana haki nayo ni yao. Ni lazima tufikie muafaka kwa mazungumzo kwakuwa tunajenga nchi moja.
 
Hivi gesi ya Songo Songo-Kilwa, mkoa wa Lindi, nani anaifaidi kama siyo ile Kampuni inayoiuzia Tanesco kwa dola za kimerikani badala ya Tshs wakati ni maliasili yetu!
 

Kwa muda mrefu sasa, nimekuwa ni msomaji wa makala za Bwana Majjid Mjengwa hasa katika gazeti la raia mwema, lakini kadiri siku zinavyoenda nimejikuta naanza kuzipuuza na hata kufikia hatua naziruka tu na kusoma mambo mengine.

Ndugu Majjid ameamua kukengeuka na kuacha weledi na kukubali kutumika katika propaganda nyepesi nyepesi ambazo hazija tija.

Kinachoniuma zaidi ni upotoshaji wa makusudi unaofanywa na watu kama akina Majjid.

Mfano mmojawapo ni pale juu nilipopapaka rangi nyekundu,

Ni lini wanamtwara wamedai kuwa gesi iwe ni ya wanamtwara tu?, Kwa uelewa wa Majjid, kudai kuwa iwanufaishe wana mtwara ndio kumaanisha kuwa iwe ni ya wanamtwara tu?

Ina maana wanavyotaka kuisafirisha kupeleka Dar es salaama itakuwa ni ya wana Dar es salaama tu?.

Acha kutumika bwana Majjid.
 
. maggid, Who is next after David Mwangosi? RIP. maana swwaiba kamuhanda amesema kuna wandishi 7 watakufa Iringa, vipi umemuanda yupi baada ya Mwangosi?
Vipi leo Jogging?
Nilikuwa nimekasirishwa sana na upotoshaji wa huyu ndugu lakini baada ya kusoma komenti yako nimecheka sana.
Unaulizia hadi jogging?, nadhani ilikuwa ni siku ile ya vurugu za polisi kuwaonea machinga ndio aliamua kufanya jogging, teh teh teh!
 
Mjuni,
Asante,
Katika dunia hii hakuna nyeusi tu wala nyeupe tu. Kama unaukana ukweli huo basi ni vigumu pia kujadili zaidi hapa. Na katika dunia hii kuna wenye kusikia wanavyopenda kusikia, kuna wenye kusoma wanavyopenda kusoma, na kuna wenye kuona wanavyopenda kuona. Wanadamu hawa huwa hawana mengi mapya ya kujifunza zaidi ya yale wanayodhani wanayajua. Sasa hilo ni tatizo la wenye matatizo hayo. Natumaini wewe si mmojawapo.
Maggid,
Iringa.
 

Wewe unapata ujumbe gani kutoka kwa Masoud?



 
Very logical. you are a Great Thinker (GT).
 

Kwamba ni kweli Mtwara na sehemu nyingine za nchi zimekuwa nyuma sana kimaendeleo. Na leo tunaposikia Mtwara kuna gesi, nakubaliana na Rais Jakaya Kikwete, kuwa gesi hiyo haiwezi kuwa ni ya WanaMtwara tu. Ni gesi ya Watanzania wote.

Hata wana Mtwara wamelikubali Hilo, Kila Mtanzania Mwenye akili Timamu analijua Hilo
Manufaa yataokanayo na Gesi ni Kwa Ajili ya Wa Tanzania wote,
Haina Haja ya Rais Kusema Ndo watu waelewe, Hilo liko Very Obviousy.


Hakuna aliyesema Kuwa Gesi iliyoko Mtwara ni Ya wana Mtwara na Kwa ajili ya Wana Mtwara.
Hapa ndo Mnapokosea na Kupandisha Hasira Za Wa Tanzania wa Mtwara, mnawalisha Maneno ambayo hawajasema.
Wao kilio Chao ni Gesi iwe Processed Mtwara From the Beggining na Products zake zisambazwe Nchi Nzima.
Sisi hatutaki Kula Gesi, tuna Kula Products za Gesi na Wana Mtwara wameridhia Hilo.

How come Msumbiji waseme Gesi liyo Mtwara ni Yao???
Kwani Mtwara ni sehemu ya Msumbiji, acha Kujenga Hoja Dhaifu na Mfu kwa Masuala yenye Kuhitaji Kufikirisha Kichwa.

Naam, ya kule Mtwara isije ikawa yale yale ya kugombania kivuli.

Unaposema Kugombania Kivuli Unamaana gani with Refference to what is Happeing in Mtwara.

My Take.
Wewe ni Mmoja ya Wachumia Tumbo ambao Mko tayar kusema Kijani ni Nyekundu for the sake ya Mkono Kwenda Kinywani.
Mnajitahidi sana Kujaribu Kupotosha Madai ya Wana Mtwara.
Kwanini Serikali yako ya CCM haitaki Kusema Kutakuwa na Hasara Kiasi gani kama Hiyo Gesi ikiwa Processed Mtwara na Products zake kuwa Distributed
Al over the Country?????????????
Hii ndo Point ya Msingi ya Wana Mtwara.

Kwenye Masuala yenye Kuhitaji Kufikirisha Kichwa kama Haya Ni Bora ukawa unakaa Kimya
 

unataka wakae pamoja mala ngapi pinda alienda kukaa nao wakamuona katuni sasa leo unatka washilikishwe nini.si busala kupotosha watu.
 
kama wananchi wa mtwara wangekuwa na nia ya dhati hayo mabomu waliyatoa wapi kama wanahitaji tu kushirikishwa,inakuwaje watu wamejiandaa kivita kabisa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…