Ngongo
Platinum Member
- Sep 20, 2008
- 21,199
- 37,532
Tatizo la Mtwara ni ushirikishwaji hafifu na bora uongozi na si uongozi bora .
Kazi kubwa ya kiongozi ni kuwaelimisha anaowaongoza.Ikiwa kiongozi hanakosa sifa ya kuongoza kwa maana ya kuelimisha na kushrikisha anaowaongoza basi huyo hawezi kuitwa kiongozi ni lazima tumtafutie jina lingine linaloendana na matendo yake.
Kwa muda mrefu sasa labda miaka ishirini hizi Tanzania imekuwa dampo la viongozi wasiokuwa na sifa za uongozi,lakini wenye kulazimisha kuitwa viongozi hata kama ni kwa kutumia nguvu za vyombo vya dola kama jeshi la polisi na UWT.Tatizo la viongozi wasiokuwa na sifa za uongozi lipo hata katika vyama vya upinzani.Mfano unakuta kiongozi wa upinzani anajipachika sifa ya ugombea Urais wa kudumu hata kama sifa za kugombea nafasi hiyo zinazidi kuporomoka siku hadi siku.Utashangaa zaidi unakumbana na waziri mzima anafunga safari za mikoani badala ya kuondoa kero za wananchi anaziongeza.
Gesi ya Mtwara na Lindi ni mali ya waTanzania wote.Dhahabu ya Geita ni mali ya waTanzania wote,Tanzanite ya Mererani ni mali ya waTanzania wote,Mlima Kilimanjaro,Hifadhi za wanyama za Serengeti,Manyara,Mikumi,Saadani,Ngorongoro na nk ni mali za waTanzania wote bila kujali unaishi karibu na hifadhi hizo au mbali kiasi gani.Binafsi naishi Arusha lakini utashagaa tatizo la mpaka la ziwa Nyasa linanigusa sana kiasi ikitokea meza ya mazungumzo imeshindikana niko tayari kuitumikia nchi yangu hata ikibidi kwa kumwaga damu.
Tatizo linalotukabili waTanzania wengi sasa ni ukosefu wa uzalendo hasa upande wa uongozi.Wananchi wamekosa imani na uongozi/utawala kwasababu ya ubinafsi.Mikataba ya madini ni kielelezo namna watawala wetu walivyo walafi.Hata hili suala la gesi yamkini watawala wetu wameshaingia mikataba ya hovyo ndiyo maana tunaoana walivyotayari kutumia nguvu nyingi pasipo maelezo na pasipo ushirikiswaji.
Gesi ya Mtwara na Lindi ni mali ya waTanzania wote.Watawala tunahitaji mikataba iliyo ya uwazi na yenye kumnufaisha mTanzania.
Mungi ibariki Tanzania.
Kazi kubwa ya kiongozi ni kuwaelimisha anaowaongoza.Ikiwa kiongozi hanakosa sifa ya kuongoza kwa maana ya kuelimisha na kushrikisha anaowaongoza basi huyo hawezi kuitwa kiongozi ni lazima tumtafutie jina lingine linaloendana na matendo yake.
Kwa muda mrefu sasa labda miaka ishirini hizi Tanzania imekuwa dampo la viongozi wasiokuwa na sifa za uongozi,lakini wenye kulazimisha kuitwa viongozi hata kama ni kwa kutumia nguvu za vyombo vya dola kama jeshi la polisi na UWT.Tatizo la viongozi wasiokuwa na sifa za uongozi lipo hata katika vyama vya upinzani.Mfano unakuta kiongozi wa upinzani anajipachika sifa ya ugombea Urais wa kudumu hata kama sifa za kugombea nafasi hiyo zinazidi kuporomoka siku hadi siku.Utashangaa zaidi unakumbana na waziri mzima anafunga safari za mikoani badala ya kuondoa kero za wananchi anaziongeza.
Gesi ya Mtwara na Lindi ni mali ya waTanzania wote.Dhahabu ya Geita ni mali ya waTanzania wote,Tanzanite ya Mererani ni mali ya waTanzania wote,Mlima Kilimanjaro,Hifadhi za wanyama za Serengeti,Manyara,Mikumi,Saadani,Ngorongoro na nk ni mali za waTanzania wote bila kujali unaishi karibu na hifadhi hizo au mbali kiasi gani.Binafsi naishi Arusha lakini utashagaa tatizo la mpaka la ziwa Nyasa linanigusa sana kiasi ikitokea meza ya mazungumzo imeshindikana niko tayari kuitumikia nchi yangu hata ikibidi kwa kumwaga damu.
Tatizo linalotukabili waTanzania wengi sasa ni ukosefu wa uzalendo hasa upande wa uongozi.Wananchi wamekosa imani na uongozi/utawala kwasababu ya ubinafsi.Mikataba ya madini ni kielelezo namna watawala wetu walivyo walafi.Hata hili suala la gesi yamkini watawala wetu wameshaingia mikataba ya hovyo ndiyo maana tunaoana walivyotayari kutumia nguvu nyingi pasipo maelezo na pasipo ushirikiswaji.
Gesi ya Mtwara na Lindi ni mali ya waTanzania wote.Watawala tunahitaji mikataba iliyo ya uwazi na yenye kumnufaisha mTanzania.
Mungi ibariki Tanzania.