Mtwara kuchele!

Mtwara kuchele!

Mwanagenzi

JF-Expert Member
Joined
Sep 11, 2006
Posts
741
Reaction score
281
Hivi karibuni nilibahatika kutembelea mji wa Mtwara. Kwa kweli nimeshuhudia mabadiliko makubwa. ..
Hivi sasa kuna ujenzi wa nyumba za makazi na majengo ya biashara kwa wingi. BoT wanajenga ghorofa kwa ajili ya ofisi zao. Nimeambiwa waheshimiwa wawili wanaotajwa kugombea urais wanajenga pia mahoteli (ya mmoja imekamilika na ndiyo jengo pekee lenye lift mjini Mtwara!).


Barabara za lami zimeongezeka kutoka nne zilizokuwepo mwaka juzi…Benki ya Dunia walifadhili ujenzi wa barabara kadhaa ambazo mojawapo imeanza kuwekwa taa za barabarani (taa za kwanza barabarani mjini Mtwara!). Hata barabara ya kwenda kwa Mkuu wa Wilaya sasa ina lami…
Nimeshuhudia ujenzi wa barabara kwenda feri (kivuko cha kwenda Msanga Mkuu, sawa na Kigamboni kwa Dar). Nikaambiwa pia uundwaji wa kivuko hicho unaendelea vizuri. Kivuko cha Kilambo kwenye Mto Ruvuma kwenda Msumbiji kimekwishamilika…


Ujenzi wa kiwanda cha saruji cha Dangote umeanza…nimeona Wachina wakiendelea na ujenzi. Upanuzi au uboreshaji wa majengo ya bandari unavutia na unaendelea. Nimeambiwa pia kuna mpango wa upanuzi wa uwanja wa ndege.
Usafiri wa Dar-Mtwara ni wa kutosha na mabasi ya kisasa-Yutong na Higer yanapishana barabarani. Hata barabarani/njiani kati ya Dar na Mtwara (kuanzia Rufiji mpaka Lindi) pameanza kubadilika.
Zuri zaidi, Mtwara hakuna mgao wa umeme kama miji mingi hapa nchini.

Kuna upimaji wa viwanja unaoendelea kwa kasi na hata UTT wamewekeza kwenye mradi wa viwanja. Viwanja mjini vimepanda bei sana…waweza pata kiwanja cha biashara mjini kwa bei ya 800m/-, amini usiamini!

Kuna vituo vitatu vya FM Radio vinavyochangamsha mji…bila kusahau Maisha Club!
Bajaji na Bodaboda ndo usiseme…teksi rasmi ndo hakuna.


Kwa kweli Mtwara ya sasa imeanza kupendeza…Mtwara kuchele! na kwa mwendo huu CCM watashinda tena kwa kishindo huko Mtwara!
 
Mwisho umeharibu! kumbe lengo lako kuandika hapa ni kugambisha tu..

Kasi ya maendeleo Mtwara na Kusini yote kwa ujumla sio yakuridhisha.
 
Mtwara yaweza kuja kuwa zaidi ya Mwanza miaka kumi ijayo

Hivi bado hujapona ule ugonjwa wako? Eti miaka 10 ijayo mtwara itaizidi mwanza! Shame one you. Hiyo miaka kumi unayozungumzia inamaana Mwanza hakutakuwa na shughuli za kiuchumi na hivyo kusitisha maendeleo yake? Ungekuwa unaakiri wewe usingepost ujinga wako. Katafute ripoti ya UN Habitat ujue miji inayokua kwa kasi ukanda wa Afrika mashariki na ndio urudi jamvini...Ukumbuke hapa jamvini hakuna wajinga kama wale uliowalia fedha ya msiba (rambirambi)
 
nani kakwambia kuwa kigezo cha maendeleo ni barabara za rami na majengo marefu?
 
Mwisho umeharibu! kumbe lengo lako kuandika hapa ni kugambisha tu..

Kasi ya maendeleo Mtwara na Kusini yote kwa ujumla sio yakuridhisha.

Hata Roma haikujengwa siku 1, ukweli ni kwamba, Mtwara sasa itakuwa jiji kubwa sana kuliko hata Dar.
 
Asante kwa taarifa zilizotokana na kupita pita kwako. Eti ndugu 'mtafiti' vipi kuhusu wale wana'gesi haitoki' umewatembelea na kujua maendeleo yao? Magorofa, maisha club, dangote, lami, taa za barabarani nk zinawasaidiaje? Wanaridhika na hayo 'maendeleo'?
 
Siyo miaka kumi mitano ijayo tu mtwara will be one of the best city in the country!
 
Good steps ahead.... Maendeleo yatafika na ukuaji utashimiri, Lakini tusitegemee masaa 24 !!
 
Hatuitaki CCM umesikia kilichomkuta DIAMOND juzi

HADI SASA TUNASUBILI YEYEOTE ATAKAE TANGAZA KUGOMBEA CCM APEWE DAWA

kama wewe ni CCM jalibu uone
 
Style ile ile ya kikoloni!
Gawa nguo na shanga chukua DHAHABU!
Kweli CCM ni mkoloni mweusi!
 
Hivi karibuni nilibahatika kutembelea mji wa Mtwara. Kwa kweli nimeshuhudia mabadiliko makubwa. ..
Hivi sasa kuna ujenzi wa nyumba za makazi na majengo ya biashara kwa wingi. BoT wanajenga ghorofa kwa ajili ya ofisi zao. Nimeambiwa waheshimiwa wawili wanaotajwa kugombea urais wanajenga pia mahoteli (ya mmoja imekamilika na ndiyo jengo pekee lenye lift mjini Mtwara!).


Barabara za lami zimeongezeka kutoka nne zilizokuwepo mwaka juzi…Benki ya Dunia walifadhili ujenzi wa barabara kadhaa ambazo mojawapo imeanza kuwekwa taa za barabarani (taa za kwanza barabarani mjini Mtwara!). Hata barabara ya kwenda kwa Mkuu wa Wilaya sasa ina lami…
Nimeshuhudia ujenzi wa barabara kwenda feri (kivuko cha kwenda Msanga Mkuu, sawa na Kigamboni kwa Dar). Nikaambiwa pia uundwaji wa kivuko hicho unaendelea vizuri. Kivuko cha Kilambo kwenye Mto Ruvuma kwenda Msumbiji kimekwishamilika…


Ujenzi wa kiwanda cha saruji cha Dangote umeanza…nimeona Wachina wakiendelea na ujenzi. Upanuzi au uboreshaji wa majengo ya bandari unavutia na unaendelea. Nimeambiwa pia kuna mpango wa upanuzi wa uwanja wa ndege.
Usafiri wa Dar-Mtwara ni wa kutosha na mabasi ya kisasa-Yutong na Higer yanapishana barabarani. Hata barabarani/njiani kati ya Dar na Mtwara (kuanzia Rufiji mpaka Lindi) pameanza kubadilika.
Zuri zaidi, Mtwara hakuna mgao wa umeme kama miji mingi hapa nchini.

Kuna upimaji wa viwanja unaoendelea kwa kasi na hata UTT wamewekeza kwenye mradi wa viwanja. Viwanja mjini vimepanda bei sana…waweza pata kiwanja cha biashara mjini kwa bei ya 800m/-, amini usiamini!

Kuna vituo vitatu vya FM Radio vinavyochangamsha mji…bila kusahau Maisha Club!
Bajaji na Bodaboda ndo usiseme…teksi rasmi ndo hakuna.


Kwa kweli Mtwara ya sasa imeanza kupendeza…Mtwara kuchele! na kwa mwendo huu CCM watashinda tena kwa kishindo huko Mtwara!


HUU NI UNAFKI TUNASUBIRI KIUMBE YEYOTE ATAKAE TANGAZA NIA YA KUGOMBEA NAFASI YEYOTE ILE TAARIFA ITAFIKA KILA KONA YA TANZANIA NA DUNIANI KOTE

MUULIZE DIAMOND KAFANYWAJE NI JUZI TU

inarillah waillaillaih Rajiuni
CCM ni MSIBA na ni gundu hatutaki hakika hatuitaki CCM
 
Unafanya maskhara na gesi? Mtwara inaweza kuwa great commercial city next to DSM, ngoja commercial production ya gas ianze ndo utajua vizuri impact ya gas...
 
kwani gesi inatumiwa Ntwara ? si yasifirishwa kwenda kwa wanaojua kutumia gesi, sasa kiwanja cha millioni 800 Ntwara unawekezea nini? huko kupanda kwa viwanja kuko 'realistic' na shughuli za kiuchumi zitakazo kuja kukua Ntwara? au ni 'Intrinsic Price'?
 
Mtwara yaweza kuja kuwa zaidi ya Mwanza miaka kumi ijayo

kwa kufikiria nje ya box!! uko sawa 100%
Ila kosa ni kwamba wapanga miji bado wanachora ramani za kizamani sana!! ila hii ndo ilikuwa nafasi ya kubaidilisha mtwara zaidi hata ya dar na si mwanza tu? maana muda upo, barabara pana, masoko, hospital makazi n.k, ila utajakuta makazi horera na upanuzi wa barabara tena baada ya miaka 5!!

SP
 
Kwa kudodosa kwangu, kiasi fulani watu kadhaa kama wamelegeza kamba msimamo wao wa kupinga ujenzi wa bomba la gesi. Wengi wameanza kujaribu kuchangamkia fursa kulingana na nafasi au uwezo wao.

Nimeona pia kuna benki "nyingi" kwa kulinganisha na "idadi ya watu" au "shughuli za uchumi". Kwa mfano, ukiondoa benki kongwe mjini Mtwara kama NBC, NMB na CRDB, pia kuna Exim, TPB, CBA na BOA. Pia kuna benki fulani (sikuweza kuifahamu) inakarabati jengo ili ifungue tawi lake.
 
Back
Top Bottom