Chachu Ombara
JF-Expert Member
- Dec 11, 2012
- 5,897
- 10,358
Kaimu RPC wa mkoa wa Mtwara, ACP Nicodemus Katembo amesema kuwa Jeshi la Polisi Mkoani humo, linamshikilia Shaibu Kuselela 58, mkazi wa kijiji cha Lipalwe halmashauri ya wilaya ya Tandahimba Mkoani Mtwara, kwa tuhuma za kumuua mkewe kisha kumzika shambani.
====================
ACP Nicodemus Katembo alisema tukio hilo lilitokea Februari 28, mwaka huu, ambapo mwanamume huyo alifanya unyama wa mauaji hayo ya mkewe Amina Mtausi (40) kwa kutumia kitu kinachodaiwa kuwa na ncha kali.
Alieleza baada ya kutekeleza mauaji hayo aliuchukua mwili wa marehemu na kwenda kuufukia katika shimo shambani kwao kisha kuchukua mpunga na kuupanda juu ya shimo hilo.
Pia, baada ya kutekeleza azma yake alitoweka kusiko kujulikana kutokana na kuhofia kukamatwa na vyombo vya sheria na chanzo cha mauaji hayo hakijajulikana.
ACP Katembo alisema tukio hilo liligundulika baada ya mdogo wa mtuhumiwa huyo, Omari Saidi alipokuwa akienda kisimani kuchota maji katika shamba hilo na kubaini harufu isiyo ya kawaida.
Alisema alipofuatilia kujua ni kitu gani ambacho kilikuwa kikitoa harufu aliona baadhi ya viungo vya marehemu huku sehemu ya mwili ukiwa umefukiwa ndani ya shimo.
ACP Katembo alisema, Said alitoa taarifa kwa vyombo husika kwa ajili ya kufuatilia tukio hilo kwa kina zaidi.
Pia soma > Atuhumiwa kuua mke na kumzika, juu ya shimo apanda mpunga
====================
ACP Nicodemus Katembo alisema tukio hilo lilitokea Februari 28, mwaka huu, ambapo mwanamume huyo alifanya unyama wa mauaji hayo ya mkewe Amina Mtausi (40) kwa kutumia kitu kinachodaiwa kuwa na ncha kali.
Alieleza baada ya kutekeleza mauaji hayo aliuchukua mwili wa marehemu na kwenda kuufukia katika shimo shambani kwao kisha kuchukua mpunga na kuupanda juu ya shimo hilo.
Pia, baada ya kutekeleza azma yake alitoweka kusiko kujulikana kutokana na kuhofia kukamatwa na vyombo vya sheria na chanzo cha mauaji hayo hakijajulikana.
ACP Katembo alisema tukio hilo liligundulika baada ya mdogo wa mtuhumiwa huyo, Omari Saidi alipokuwa akienda kisimani kuchota maji katika shamba hilo na kubaini harufu isiyo ya kawaida.
Alisema alipofuatilia kujua ni kitu gani ambacho kilikuwa kikitoa harufu aliona baadhi ya viungo vya marehemu huku sehemu ya mwili ukiwa umefukiwa ndani ya shimo.
ACP Katembo alisema, Said alitoa taarifa kwa vyombo husika kwa ajili ya kufuatilia tukio hilo kwa kina zaidi.
Pia soma > Atuhumiwa kuua mke na kumzika, juu ya shimo apanda mpunga