Mtume Paulo alikuwa mkorofi sana

mimiamadiwenani

JF-Expert Member
Mar 9, 2022
5,411
7,016
Hali? Kuna watu wanadhani ni ajabu na kuwa watumishi wa Mungu wakigombana ujue ni wa shetani na hawatoki kwa Mungu. Siyo kweli. Kugombana HATA kwenye kazi ya Mungu, ni kawaida SANA.

Paulo mtume aligombana na mtume mwenzake Barnaba kufikia mpaka hatua ya kutengana na kila mtu kuangalia biashara zake, huku kisa kikiwa ni kazi hiyo hiyo ya Mungu.

Paulo aligombana na kumchana wazi wazi Petro ambaye ndiye alikuwa kiongozi wa kanisa muda huo. Paulo hakujali cheo, alimuumbua Mtume Petro mbele ya kadamnasi. Leo hii nani angethubutu?

Achilia mbali visa hivyo hapo juu, kuna vingine vingi zaidi vya Mtume Paulo kugombana na mitume wenzake.

Achilia mbali ile ya kumkataa mtume Marko asiongozane nao... Paulo hakuwa anasamehe kirahisi. Alikuwa mkali sana.
Hakuwa na mizaha wala itifaki kwenye kusem ukweli.

Pamoja na hayo yote, na bado alikuwa na roho mtakatifu. Unajiuliza mtu mwenye hulka ya Paulo anawezaje kuwa na roho mtakatifu?

Leo makanisani ukiwa kama Paulo utaambiwa bado Yesu hajaumbika ndani yako, utaambiwa bado una dhambi, utaambiwa hujaokoka kiukweli, na maneno kadha wa kadha.

Hivyo ugomvi kwenye injili ni kawaida mno, na hiyo haimaanishi kuwa watumishi ni wa uongo kwa kuwa wanagombana. Kanisa la leo limepotosha mno kwa makusudi, mafundisho ili ku favor upande wa viongozi na wachungaji.

Ukiwa na tabia za Paulo wewe si rafiki wa makanisa YOTE ya leo, ya kiprotestanti na katoliki yote. Hata kutengwa utatengwa.

Ndipo hapa tulipofika?? Nahuzunika mno!
 
Hawa ndiyo watume wetu

Mbona hata mtume Muhamad

1. Alioa binti wa miaka 9 (huu ni ubakaji). Hapa alikuwa anaona raha gani kumuingilia mtoto wa miaka 9? Angekuwepo wakati huu alikuwa anafungwa miaka 30 jela.

2. Alikuwa hajui kusoma na kuandika.

3. Alioa mtu aliyemzidi umri (Marioo).

Ongezea na nabii Tito
 
Mungu anatujua na anatupenda pamoja na madhaifu yetu...
Paulo mpaka leo hii baadhi ya wachungaji wameshaanza kumkataa kwa sababu mbali mbali. Makanisa ya leo yanataka uwe lofa. Huko ndiko wanaita kuumbika kwa Kristo ndani yako. Uwe kondoo mtiifu, usiyehoji wala kuuliza.

Ukiwa kama Paulo, utaambiwa hujaokoka bado, hujampokea Roho mtakatifu. 99% sasa hivi ni uoga ndiyo waumini wamejengewa. Hofu!.
 
Upanga ukatao kuwili huo. Kama mchungaji analeta za kuleta kwa nini asiambiwe ukweli? Ila wakati mwingine biblia inaonya kuhusu kumnyoshea kidole mpaka mafuta wa Bwana, rejea kisa cha yule mtumishi wa Mfalme Sauli alimpomfikishia Daudi habari za kifo cha Mfalme Sauli.

Hata hata hapa nchini kuna wachungaji wakubwa na maarufu walianzisha makanisa yao/huduma kutokana na migogoro na wenzao na kupelekea kujitenga.

Tunayajua makanisa hayo, ila ni kazi nzuri ya Mungu kupanua kazi yake kwa mataifa kuliko wangerundikana pamoja tu huku kuna wengine wanahitaji kufikiwa na nuru ya injili ya Yesu Kristo
 
I
Hali? Kuna watu wanadhani ni ajabu na kuwa watumishi wa Mungu wakigombana ujue ni wa shetani na hawatoki kwa Mungu. Siyo kweli. Kugombana HATA kwenye kazi ya Mungu, ni kawaida SANA...
INgia Youtube andika; mchungaji Magembe.

Huyu ana misimamo ya Paulo, hapendwi hata na wachungaji wenzake.

Huyu mzee anawachana maaskofu mbele yao bila ganzi.
 
Upanga ukatao kuwili huo. Kama mchungaji analeta za kuleta kwa nini asiambiwe ukweli? Ila wakati mwingine biblia inaonya kuhusu kumnyoshea kidole mpaka mafuta wa Bwana...
Hiyo ya kutomnyooshea kidole masihi wa Bwana Paulo aliikataa. Na bado Mungu alimpa roho wake. Kuna watu ni wake Mungu ila wewe hutojua kuwa ni wa kwake. Anawajua yeye TU.
 
Back
Top Bottom