Mtulia ameacha kumuunga mkono Rais?

MgungaMiba

JF-Expert Member
Aug 28, 2011
999
815
Bw Mtulia alichaguliwa na wananchi wa jimbo la Kinondoni kuwa Mbunge wao. Bw Mtulia akajiuzulu ubunge kwa hiyari yake ili aweze kumuunga mkono Rais Magufuli kwa kazi nzuri anayoifanya. Mimi nilimuelewa vizuri, kwani moja ya kazi za bunge ni kuikosoa na kuidhibiti serikali ili ifanye kazi zake vizuri.

Sasa huyu bwana Mtulia alipoamua kujiuzulu ubunge nikaelewa kuwa aliona hakuna haja ya kuikosoa wala kuidhibiti serikali ambayo yeye anaona Mkuu wake, ambae ni Mh Rais Magufuli, anachapa kazi kiasi cha kumridhisha yeye Mtulia.

Hivyo niliona ni uungwana kwa yeye kujiuzulu kwenye ubunge (ingawa kitendo hicho kilileta maumivu makubwa na vilio kwa waliompigania hadi akashinda) ili ampishe mtu mwingine kwenye nafasi hiyo ili aende akaifanye kazi ya kibunge inavyopasa na yeye akaendelee kumuunga mkono Rais Magufuli kwa njia nyingine atakayoona inafaa isiyokuwa ya kibunge ambayo alijiuzulu.

Ghafla nikashtukia bwana huyu karudi tena kwa watu walewale, wa jimbo lilelile, tena kwa gharama kubwa kutaka tena nafasi ileile ya Ubunge, ndipo nikaona niulize, Je sasa ndio ameghairi kumuunga mkono Rais Magufuli?
 
At
Bw Mtulia alichaguliwa na wananchi wa jimbo la Kinondoni kuwa Mbunge wao. Bw Mtulia akajiuzulu ubunge kwa hiyari yake ili aweze kumuunga mkono Rais Magufuli kwa kazi nzuri anayoifanya. Mimi nilimuelewa vizuri, kwani moja ya kazi za bunge ni kuikosoa na kuidhibiti serikali ili ifanye kazi zake vizuri.

Sasa huyu bwana Mtulia alipoamua kujiuzulu ubunge nikaelewa kuwa aliona hakuna haja ya kuikosoa wala kuidhibiti serikali ambayo yeye anaona Mkuu wake, ambae ni Mh Rais Magufuli, anachapa kazi kiasi cha kumridhisha yeye Mtulia.

Hivyo niliona ni uungwana kwa yeye kujiuzulu kwenye ubunge (ingawa kitendo hicho kilileta maumivu makubwa na vilio kwa waliompigania hadi akashinda) ili ampishe mtu mwingine kwenye nafasi hiyo ili aende akaifanye kazi ya kibunge inavyopasa na yeye akaendelee kumuunga mkono Rais Magufuli kwa njia nyingine atakayoona inafaa isiyokuwa ya kibunge ambayo alijiuzulu.

Ghafla nikashtukia bwana huyu karudi tena kwa watu walewale, wa jimbo lilelile, tena kwa gharama kubwa kutaka tena nafasi ileile ya Ubunge, ndipo nikaona niulize, Je sasa ndio ameghairi kumuunga mkono Rais Magufuli?

Atateuliwa kuwa waziri na kuweza kumsupport haswa.
 
Nini maana ya kujiuzuru then unaitaji tena cheo hikohiko kwa wananchi haohao taifa haliendelei kwa sababu kama hizi
 
Watu wa Kinondoni inabidi wamtose huyu jamaa. Maana ameitia hasara Serikali kwa kuleta gharama zisizohitajika za uchaguzi ambapo pesa hizo zingetumika kuleta maendeleo kwa wananchi wake. Kama alitaka kumuunga mkono raisi jamani si angeweza kumuunga akiwa mbunge wa Chadema. Kwani kulikuwa na ugumu ..?. Mimi naona Kinondoni isipomtosa huyu mtu na wengine wa haina hii. Basi huu mchezo utaelendelea kwenye mikoa mingine kwa kasi. Na kuendelea kuliletea taifa hasara. Ila wakitoswa watu wa haina hii basi wote wanaotaka kutoka kwa njia hii watabidi wajifirikie mara mbili maana watajua hawarudi tena bungeni.
 
Katumia udhaifu wa sheria zetu kumshambulia Mtulia haitobadili chochote tujikite kwenya sheria ibadilishwe kwani kajiuzulu kwa ridhaa yake.
 
Nakumbuka Shibuda alikuwa Mbunge wa Chadema, alikuwa akimuunga mkono Kikwete na CCM lakini hakujiuzulu. Labda sheria irekebishwe ili Mbunge akifa au akihama Chama, basi Chama ndio kijiwekee utaratibu wa kujazia nafasi hiyo.
 
Back
Top Bottom